Nimepewa million 20 mkononi, niifanyie nini?

Nimepewa million 20 mkononi, niifanyie nini?

liverman

New Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
4
Reaction score
1
naomba ushauri. personally nafikiria kuanzisha butcher. mwenye ushauri please
 
Njoo kwenye gold inalipa .unatoa huku na kupeleka dar
 
naomba ushauri. personally nafikiria kuanzisha butcher. mwenye ushauri please
MaGU anataarifa na hiyo 20m ? anza kuinYwa fasta kabla haijabadilishwa matumizi yake kwenda kununua madawa hospitalini au madawati shuleni.
 
hela ya namna hiyo itakucost koz hata hujajipanga...njoo tu nikuuzie magunia ya mpunga utunze ndani ukisubiri bei ipande uuze utapata faida sna hasa msimu huu wa siku kuu...lakini pia utakuwa umefanya akili yako iseto na kupata akili ya wazo sahihi ya nn ufanye
 
Ndugu cha kwanza cha kuelewa.

Huwezi kufanya kila biashara, hata kama mtaji unao, yaani inahitaji mtaji wa Millioni 20.

Kukupa ushauri inahitaji mambo kadhaa. Ingawa hujasema mengi , nitashauri kufuatana na machache uliyosema.

1. Umepewa 20 MLN. kwamba huu si mkopo toka benki na hauna riba. Pengine ni mkopo tu utarudisha hela kamili baada ya kipindi fulani.
2. Wewe binafsi una uzoefu kwenye biashara gani? Je umewahi kuajiriwa katika eneo fulani na hivyo unajua mzunguko wa biashara hiyo hivyo kwa kuangalia uzoefu wako unaweza unaanzisha kitu fulani.
3. Angalia biashara zilizopo na uchunguze kwa makini ni eneo gani unaweza kuingia , ukafanya biashara kwa njia tofauti , au ukatibu tatizo fulani lililoko kwenye eneo hilo kwa kufanya biashara .
4. Lenga kufanya biashara ambayo unaweza ukaanza kidogo na halafu ikawa na uwezo wa kupanuka na isihitaji usimamizi wako kwa karibu. Biashara ambazo inaweza kuwa na automation system au checking system, ambazo ukienda unaweza ukacheki vizuri.
5. Unaweza kuanzisha biashara ambayo kama wewe huna uzoefu , basi unaweza ukawapata wazoefu ukawaajiri na hapo hapo ukiendelea kujifunza pole pole.

6. Anzisha biashara kufuatana na haiba yako. Ukijiangalia mwenyewe , je unaweza kukidhi vigezo vya kufanya biashara katika eneo husika. Mfano, unataka kuanzisha biashara ya udalali wa matunda na mboga mboga - Sokoni Kariakoo. Hapa unahitajika kuamka mapema karibu saa tisa ya usiku kila siku. Je unaweza kuamka muda huo kila mara.



Baada ya kusema hayo wewe mwenyewe utajipima na kuangalia ni eneo gani moyo wako upo tayari kufanya na kuendelea kukuza biashara yako.

Angalia biashara zilizopo na uamue kufanya kitu kipya na umaanishe unaweza kufanya biashara.

Kwa msaada wa mawazo . Aanzisha biashara za huduma, lakini zinazolenga kutoa bidhaa halisi.

Mfano. Unaweza kuanzisha fast food ya gharama ndogo - Unahitaji majiko ya kisasa na mandhari nzuri na uwe karibu na barabara ambapo wateja wanaweza kufika kwa urahisi. Halafu tizama majirani wanaokuzunguka, kama kuna taasisi zozote , shule binafsi, lenga kuwapelekea chakula maofisi . Ukianzia vitafunwa, chakula cha mchana . Hapa utakuwa na masoko mawili, wale wanaokuja kula pale kwenye mgahawa na wale utakaokuwa unapelekea outside catering .

Kufanya outside catering, huitaji hela nyingi. Kuna bodaboda kibao , unampa tenda au unanunua ya kwako unafanya delivery kwa urahisi kabisa.
 
subiria pm za watoto wakare, tangazo limemalizika.
 
NAKUSHAURI NUNUA MASHAMBA IRINGA AU NJOMBE, OTESHA MITI YA MIAKA 5 KAMA NGUZO AU MIAKA KUMI ya mbao @ mti kwa mwaka huu ni 50,000/= miti 1000 INALIPA je kwa miaka kumi ijayo itakuwaje

KUHUSU BUCHERY NADHANI MILION 3 TU ZINATOSHA yani kujenga, friji, na kununua nyama kwa jumla machinjioni,

au

NUNUA KIWANJA UJENGE FREM, NA BUCHERY UKIKODISHIA ITAKULIPA KIDOGO kidogo

au

nunua kiwanja mjini uje ukiuze baada ya mwaka utakuwa ushapata jibu la wapi uwekeze

KUMBUKA DHAMANI YA HELA YA LEO SI SAWA NAYA KESHO
 
fungua fixed account ya mwezi weka ela yote tulia Fanya utafiti ufanye nini mwezi unatosha wewe kujua cha kufanya na utakuwa una wenge la kutaka kufanya kila kitu
 
Nenda maeneo ya kabuku, tafuta shamba wangalau la ekari tano kila ekari utapata kwa laki moja itategemea na speed yako ya mapatano. Hakikisha unapata shamba lenye bonde. Nenda kodisha dozer tanroads uchimbe lambo la maji. Hilo dozer kwa siku 2 litakugharimbu wangalau 5 milioni. siku ya kwanza chimba lambo siku ya pili, litumie kusafisha shamba zima. Baada ya hapo miti iyokatwa kama matokeo ya kusafisha shamba tumia kuchomea matofali ya kuchoma. Wangalau tofali moja la kuchoma litakugharimu sh. 100. Wangalau matofali 20,0000 ni kama milioni mbili hivi. Tumia kama milioni 5 kujenga mabanda ya kuku na wangalau nyumba ndongo ya vyumba viwili na choo ili uweze kuishi. Nunua kuku wangalau 200 chotara, kifaranga 2500@. Wangalau kwa mahesabu hayo utakuwa umetumia karibia 15m. Utabakiwa na 5m kwa ajili ya gharama ndogondogo za uendeshaji na kujikimu.

Mvua zatakapoaanza maji yataingia kwenye lambo anza kulima mbogamboga kama hoho, nyanya, tango tikiti nk kuzunguka lambo. Maji hayohayo utayatumia kunyweshea mifugo na mbogamboga. Ndani ya miezi 6-7 utaanza kuokota mayai, unaweza kununua wangalau kuku kama 10 wa kienyeji kwa ajili ya kuatamia mayai kwani kuku machotara sio wazuri sana kwenye kuatamia na ninadhani kwa hapo kabuku kuweza kupata incubator ni shida juu ya umeme. Kumbuka ndani ya hiyo miezi 6 wangalau maji yatakuwa yameingia kwenye bwawa ambalo utakuwa ukilima mboga mboga. Kuanzia hapo maisha yako yatatengamaa na unaweza kugeuka kuwa mjasiriamali mzuri kama utakuwa mchapakazi na usipokuwa mfuja hela. Kama uko serious hiyo 20m inaweza kukupitisha kwa mchanganuo huo na ndani ya miezi 6 utaanza kurudisha hela yako taratibu na kuneemeka.

CC: Liverman
 
fungua fixed account ya mwezi weka ela yote tulia Fanya utafiti ufanye nini mwezi unatosha wewe kujua cha kufanya na utakuwa una wenge la kutaka kufanya kila kitu

Mkuu kwa 'Experience' yako hiyo 20M kwa mwezi mmoja anaweza kupata Interest rate ya kiasi gani?
 
Yani 20M unawaza cha kufanya...kaweke heshima bar😛oa
 
Ndugu cha kwanza cha kuelewa.

Huwezi kufanya kila biashara, hata kama mtaji unao, yaani inahitaji mtaji wa Millioni 20.

Kukupa ushauri inahitaji mambo kadhaa. Ingawa hujasema mengi , nitashauri kufuatana na machache uliyosema.

1. Umepewa 20 MLN. kwamba huu si mkopo toka benki na hauna riba. Pengine ni mkopo tu utarudisha hela kamili baada ya kipindi fulani.
2. Wewe binafsi una uzoefu kwenye biashara gani? Je umewahi kuajiriwa katika eneo fulani na hivyo unajua mzunguko wa biashara hiyo hivyo kwa kuangalia uzoefu wako unaweza unaanzisha kitu fulani.
3. Angalia biashara zilizopo na uchunguze kwa makini ni eneo gani unaweza kuingia , ukafanya biashara kwa njia tofauti , au ukatibu tatizo fulani lililoko kwenye eneo hilo kwa kufanya biashara .
4. Lenga kufanya biashara ambayo unaweza ukaanza kidogo na halafu ikawa na uwezo wa kupanuka na isihitaji usimamizi wako kwa karibu. Biashara ambazo inaweza kuwa na automation system au checking system, ambazo ukienda unaweza ukacheki vizuri.
5. Unaweza kuanzisha biashara ambayo kama wewe huna uzoefu , basi unaweza ukawapata wazoefu ukawaajiri na hapo hapo ukiendelea kujifunza pole pole.

6. Anzisha biashara kufuatana na haiba yako. Ukijiangalia mwenyewe , je unaweza kukidhi vigezo vya kufanya biashara katika eneo husika. Mfano, unataka kuanzisha biashara ya udalali wa matunda na mboga mboga - Sokoni Kariakoo. Hapa unahitajika kuamka mapema karibu saa tisa ya usiku kila siku. Je unaweza kuamka muda huo kila mara.



Baada ya kusema hayo wewe mwenyewe utajipima na kuangalia ni eneo gani moyo wako upo tayari kufanya na kuendelea kukuza biashara yako.

Angalia biashara zilizopo na uamue kufanya kitu kipya na umaanishe unaweza kufanya biashara.

Kwa msaada wa mawazo . Aanzisha biashara za huduma, lakini zinazolenga kutoa bidhaa halisi.

Mfano. Unaweza kuanzisha fast food ya gharama ndogo - Unahitaji majiko ya kisasa na mandhari nzuri na uwe karibu na barabara ambapo wateja wanaweza kufika kwa urahisi. Halafu tizama majirani wanaokuzunguka, kama kuna taasisi zozote , shule binafsi, lenga kuwapelekea chakula maofisi . Ukianzia vitafunwa, chakula cha mchana . Hapa utakuwa na masoko mawili, wale wanaokuja kula pale kwenye mgahawa na wale utakaokuwa unapelekea outside catering .

Kufanya outside catering, huitaji hela nyingi. Kuna bodaboda kibao , unampa tenda au unanunua ya kwako unafanya delivery kwa urahisi kabisa.

The best Post for me.
Ubarikiwe mkuu,
 
naomba ushauri. personally nafikiria kuanzisha butcher. mwenye ushauri please

Ningekushauri kitu, ila sema umekuwa na maelezo
mafupi sana yasiyo na uchambuzi wa vitu kadhaa
vinavyotakiwa kutolewa ufafanuzi.
 
Back
Top Bottom