huo ndio ubaya wa pesa kuanzia mkononi badala ya kichwani. ili uweze kushika na kuendeleza pesa ni lazima pesa ianze kuonekana kichwani. unapanga na kujiridhisha mfano nitanunua mbuzi mtera iringa kwa 40,000@ nitawafikisha pugu kwa gharama ya 5000@ nitawauza kwa 60.000 mpaka 70,000@ nakuibuka na faida ya 10,000 mpaka 20,000@.
kama kweli umepata hiyo 20ml kainunulie vipande vya mfuko wa uwekezaji au kuna watu na mashirika meeeengi wanakopesha pesa kwa wafanyabiashara kwa riba ya 20%, 30% 50%, 60% per month. kuna ndugu zangu na marafiki zangu wana biashara hizi.. kubaliana uwekeze kwenye mfuko mtagawana kadri mtakavyokubaliana. kuna soko la fedha linazidiwa uhitaji(demand ni kuubwa saana kuliko supply). wakati huo uwe unajitathmini unapenda uweje katika maisha yako; kuwa mfanya biashara au mwekezaji?