Nimependa utaratibu huu wa Kenya, Umwinyi utaturudisha nyuma Watanzania

Nkobe

JF-Expert Member
Feb 17, 2013
2,204
3,277
Nimependa sana utaratibu wa Kenya. Kule unaishi kwa jasho lako, hali ya soko au demand inaachwa iongee yenyewe, hakuna chombo cha kupanga bei ya Nauli ya bus au daladala. Kule nauli inabadilika kadri ya mahitaji ya wakati huo, mfano asubuhi unaweza kupanda daladala kwenda kilomita 15 kwa Tsh 1500, lakini mchana urefu huo huo ukasafiri kwa Tsh 500.
Mimi nimependa sana namna hii ya uchumi, kwamba inawafanya watu wafanye kazi kwa bidii bila kusubiri serikali kuwatetea kwa kupenda "cheap life". Haiwezekani mtu kajituma, kanunua Hiace yake, halafu umpangie nauli kuwa ni shilingi 300. Hii tabia ya serikali yetu kuingilia biashara za watu inajenga tabia ya uzembe na umwinyi. Kuna kituko kingine nimesikia eti wananchi wanataka serikali itoe bei elekezi ya nyumba za kupanga, kwa mfumo huu wa umwinyi itatuchukua muda mrefu kuwa na fikra za kujitegemea ikizingatiwa kuwa dunia siyo kisiwa. Tuache soko liongee, watoa huduma wakikosa wateja watashusha wenyewe bei, kama ambavyo Wakenya wanashusha bei wenyewe kwa kutegemea nyakati
 
Sasa unafikiri Wakenya wengi wana maisha mazuri? Ni wachache wako vizuri. Asilimia kubwa wana maisha ya shida. Tanzania tuko vizuri kimaisha mtu yoyote anaweza miliki ardhi. Kenya subutu ni matajiri tu

Ukitaka kujua ugumu wa maisha angalia per capital income ulinganishe na sisi
 
Ukitaka kujua ugumu wa maisha angalia per capital income ulinganishe na sisi
Tupe hiyo analysis mkuu ila kwa mtazamo tu utaona sis afadhali, Umeshawahi kuona kuna slam Tanzania? Kenya inayo slum, slum inashiria kuwa kuna maisha magumu sana kwa watu wa chini. Wakatu huo huo kuna wachache ndio wanafaidi
 
Sasa unafikiri Wakenya wengi wana maisha mazuri? Ni wachache wako vizuri. Asilimia kubwa wana maisha ya shida. Tanzania tuko vizuri kimaisha mtu yoyote anaweza miliki ardhi. Kenya subutu ni matajiri tu

Uporini utakuwa unakusumbuwa wewe, sidhani hata Kakamenga umewahi kufika wewe. Kenya ni nchi ya UCHUMI WA KATI (Middle Income Country ). Tanzania ni Highly Indebted Poor Country (HIPC).

Kenya inazidi Tanzania kwa vigezo vyote vya kiuchumi vinavyotambulika duniani. BTW Amani Utulivu Mshikamano na Muungano sio vigezo vya kiuchumi.

Muwe mnapenda kujielimisha badala ya kuwa brain washed na wanasiasa uchwara. Ukitoka nje ukaongea maneno hayo utachekwa hata Juha.
 
Uporini utakuwa unakusumbuwa wewe, sidhani hata Kakamenga umewahi kufika wewe. Kenya ni nchi ya UCHUMI WA KATI (Middle Income Country ). Tanzania ni Highly Indebted Poor Country (HIPC).

Kenya inazidi Tanzania kwa vigezo vyote vya kiuchumi vinavyotambulika duniani. BTW Amani Utulivu Mshikamano na Muungano sio vigezo vya kiuchumi.

Muwe mnapenda kujielimisha badala ya kuwa brain washed na wanasiasa uchwara. Ukitoka nje ukaongea maneno hayo utachekwa hata ****.
Povu la nini dada?
 
Jamani sio kila kitu akifanya jirani unaiga, kuna mengine kwetu mazuri . Hii inaondoa uwezekano wa wafanyabiashara kukaa na kupanga bei na kufanya super profit. Kwa hili wachaa waendelee na utaratibu wao.
 
Tupe hiyo analysis mkuu ila kwa mtazamo tu utaona sis afadhali, Umeshawahi kuona kuna slam Tanzania? Kenya inayo slum, slum inashiria kuwa kuna maisha magumu sana kwa watu wa chini. Wakatu huo huo kuna wachache ndio wanafaidi
Hivi unajua maana ya slum? Dar es salaam zaidi ya nusu ni slum .
 
Sasa unafikiri Wakenya wengi wana maisha mazuri? Ni wachache wako vizuri. Asilimia kubwa wana maisha ya shida. Tanzania tuko vizuri kimaisha mtu yoyote anaweza miliki ardhi. Kenya subutu ni matajiri tu
Haya mambo ya kusema kila mtu ana uwezo wa kumiliki ardhi kuna haja ya kuyatathmini upya. Ni kweli Kenya utajiri unahodhiwa na kikundi kidogo lakini swali la msingi ni, ....waliipataje!?
Nature inatufundisha kwamba 'the fittest always win', na ukienda na hiyo principle ni kwamba 'the weaker will strive to become better' ili kuwaondoa hao so called fittest.
Ndio maana Ulaya ardhi inamilikiwa na wachache lakini wana uwezo wa kuitumia kwa manufaa ya wengi (kulima chakula cha kuwatosheleza wote). Tumeona hata Zim walijaribu kuwagawia ardhi watu wasioelewa maana ya kuimiliki na wameishia kukumbwa na njaa. Na tatizo kubwa hapa katika 'ugawaji ardhi kwa usawa' ni kwamba wale wanaosimamia hili zoezi (maofisa wa serikali) wana ubinafsi na roho mbaya kuzidi hata wale wanaotaka kuimiliki kwa uhalali.
Tukumbuke tu kuwa ardhi ipo na sote tutaiacha hivyo uwezekano wa asiyekuwa nayo leo kuwa nayo kesho ni mkubwa. Kama mambo ya kutaifisha bila umakini ardhi yasingefanyika naamini miji yetu mingi ingelikuwa katika mpangilio mzuri na vurugu za wakulima na wafugaji zingelikuwa kidogo. Tz sera zetu za ardhi zimebeba matatizo makubwa kwa siku za mbeleni na atakayekuwepo atakubaliana na maneno haya!
 
Uporini utakuwa unakusumbuwa wewe, sidhani hata Kakamenga umewahi kufika wewe. Kenya ni nchi ya UCHUMI WA KATI (Middle Income Country ). Tanzania ni Highly Indebted Poor Country (HIPC).

Kenya inazidi Tanzania kwa vigezo vyote vya kiuchumi vinavyotambulika duniani. BTW Amani Utulivu Mshikamano na Muungano sio vigezo vya kiuchumi.

Muwe mnapenda kujielimisha badala ya kuwa brain washed na wanasiasa uchwara. Ukitoka nje ukaongea maneno hayo utachekwa hata ****.
Upori labda unakusumbua wewe. Usione jina nalotumia hapo ukafikiri mluga mluga i am international nimeshakaa dunia ya kwanza miaka mingi sana. Anyway jiulize swali moja pamoja matakwimu yako ambayo hayana reference kwa nini Wakenya wanakimbilia Tanzania, na sisi hatuendi huko kwao?
 
Hivi unajua maana ya slum? Dar es salaam zaidi ya nusu ni slum .
Inawezekana wewe ndio ujui maana ya slums. Tanzania hakuna slums ipo Kenya Kibira google utajua nazungumzia nini? Nyingine ipo India na Nigeria majina nimeyasahau. Watu wanaishi katika mazingira magumu sana wanaokota vitu jalalani ili kuweza kukidhi mahitaji ya kila siku. Sisi bado hatujafikia hali hiyo hata Tandale kwa Mtogole hawaishi hivyo
 
Nimependa sana utaratibu wa Kenya. Kule unaishi kwa jasho lako, hali ya soko au demand inaachwa iongee yenyewe, hakuna chombo cha kupanga bei ya Nauli ya bus au daladala. Kule nauli inabadilika kadri ya mahitaji ya wakati huo, mfano asubuhi unaweza kupanda daladala kwenda kilomita 15 kwa Tsh 1500, lakini mchana urefu huo huo ukasafiri kwa Tsh 500.
Mimi nimependa sana namna hii ya uchumi, kwamba inawafanya watu wafanye kazi kwa bidii bila kusubiri serikali kuwatetea kwa kupenda "cheap life". Haiwezekani mtu kajituma, kanunua Hiace yake, halafu umpangie nauli kuwa ni shilingi 300. Hii tabia ya serikali yetu kuingilia biashara za watu inajenga tabia ya uzembe na umwinyi. Kuna kituko kingine nimesikia eti wananchi wanataka serikali itoe bei elekezi ya nyumba za kupanga, kwa mfumo huu wa umwinyi itatuchukua muda mrefu kuwa na fikra za kujitegemea ikizingatiwa kuwa dunia siyo kisiwa. Tuache soko liongee, watoa huduma wakikosa wateja watashusha wenyewe bei, kama ambavyo Wakenya wanashusha bei wenyewe kwa kutegemea nyakati
We jamaa umepata pesa zako za kuuza shamba la urithi ukanunua ki hiace chako na vyumba vyako viwili uswahilini choo cha nje umejiona mjanja,eti nawe unaona utaratibu wa Kenya mzuri !!!!!!!!!
 
Inawezekana wewe ndio ujui maana ya slums. Tanzania hakuna slums ipo Kenya Kibira google utajua nazungumzia nini? Nyingine ipo India na Nigeria majina nimeyasahau. Watu wanaishi katika mazingira magumu sana wanaokota vitu jalalani ili kuweza kukidhi mahitaji ya kila siku. Sisi bado hatujafikia hali hiyo hata Tandale kwa Mtogole hawaishi hivyo
Tanzania hakuna slums? Hivi unajua sehemu yoyote iliyojegwa holela na kuna msongamano wa watu ni slums? Dar es salaam iliyopimwa ni kiasi gani?
 
Haya mambo ya kusema kila mtu ana uwezo wa kumiliki ardhi kuna haja ya kuyatathmini upya. Ni kweli Kenya utajiri unahodhiwa na kikundi kidogo lakini swali la msingi ni, ....waliipataje!?
Nature inatufundisha kwamba 'the fittest always win', na ukienda na hiyo principle ni kwamba 'the weaker will strive to become better' ili kuwaondoa hao so called fittest.
Ndio maana Ulaya ardhi inamilikiwa na wachache lakini wana uwezo wa kuitumia kwa manufaa ya wengi (kulima chakula cha kuwatosheleza wote). Tumeona hata Zim walijaribu kuwagawia ardhi watu wasioelewa maana ya kuimiliki na wameishia kukumbwa na njaa. Na tatizo kubwa hapa katika 'ugawaji ardhi kwa usawa' ni kwamba wale wanaosimamia hili zoezi (maofisa wa serikali) wana ubinafsi na roho mbaya kuzidi hata wale wanaotaka kuimiliki kwa uhalali.
Tukumbuke tu kuwa ardhi ipo na sote tutaiacha hivyo uwezekano wa asiyekuwa nayo leo kuwa nayo kesho ni mkubwa. Kama mambo ya kutaifisha bila umakini ardhi yasingefanyika naamini miji yetu mingi ingelikuwa katika mpangilio mzuri na vurugu za wakulima na wafugaji zingelikuwa kidogo. Tz sera zetu za ardhi zimebeba matatizo makubwa kwa siku za mbeleni na atakayekuwepo atakubaliana na maneno haya!

Umeongea vitu vya maana sana...
 
Back
Top Bottom