Nimependa siasa za Lowassa

Nimependa siasa za Lowassa

Watanzania bwana hizo sera anazozisema kwa dakika kumi ni zipi?ulishaona wapi katika chaguzi barani africa tu mgombea ananadi sera dakika kumi?na hata kwa nchi zilizoendelea ulishawahi ona mgombea anaongea dakika kumi kunadi sera?tuache ushabiki hata kama unahitaji mabadiliko angalia hayo mabadiliko yanapatikanaje sio alimradi mabadiliko.


kwani kuongea sana ndo kutekeleza? mbona mkuu wa kaya huwa anaongea hata masaa matatu nini kinafanyika?
 
Kumbukumbu zinaonyesha;
  • mwaka 1995 ilani ya ccm ilikuwa na kurasa 300
  • mwaka2000 kurasa 350
  • mwaka 2005 kurasa 380
  • mwaka 2010 kurasa 430 na
  • Mwaka huu ilani ya ccm ina kurasa 450
Ilani ya chadema kupitia ukawa ina kurasa 30 ikiwa na vipaumbele si zaidi ya 16
Lowassaa na Mabadiliko

Ilan ya ukawa nimeipenda sana ni nzuri na haichoshi kusoma si kama za wenzetu wamezoea ngonjera nani atasoma pgs 450 sana sana ukinipa hilo likitabu nitawashio moto jiko la mkaa.
 
Hivi ninyi nani aliyewaroga. Hamjui kuwa huyo mzee kachoka sana na hana uwezo wa kuongoza. Kachoka mwili hadi fahamu ndo mana anarudiarudia sera za ccm
Mtaongea sana wakuu, ila ukweli ni kuwa busara za huyu jamaa zinawafanya hata CCM wanabaki kutojua pa kushika, mtukaneni, msimangeni na mseme yote yaliyojaa mioyoni mwenu, ila ukweli jamaa anatufundisha siasa, hajibu matusi....yeye anataka kuhakikisha mkulima hakopwi na akikopwa alipwe na riba, muiteni mgonjwa, yeye hajibu......maneno yake anataka vijana wasome bure.....dakika kumi zinatosha kumuelewa.......kwa support anayopata kila anapopita, inabidi mjiulize pamoja na yote hayo lkn wananchi wanaye tu, kunani?
 
Mimi kwa kweli nafatilia sana siasa ila sijasikia sera muhimu za lowasa anasemaga elim elim basi mwisho anasema pipooz pipooz dakika tano tu kisha akatoa tovuti ya chama kwa kweli simuelewi kabisa ungemsikia jana zito ungekosa la kuandika leo
 
Ilan ya ukawa nimeipenda sana ni nzuri na haichoshi kusoma si kama za wenzetu wamezoea ngonjera nani atasoma pgs 450 sana sana ukinipa hilo likitabu nitawashio moto jiko la mkaa.

Hahaha mkuu umefunika!!
 
Mfalme Suleiman alifundisha namna ya kuishi na kutenda ili uonekane, utambulike na uheshimike kama mtu muungwana na mwenye busara. Aliandika katika kitabu cha Mithali 26:4 "Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; usije ukafanane naye". Kwa Kiingereza inaeleweka vizuri zaidi: "Don't answer the foolish arguments of fools, or you will become as foolish as they are". Ni dhahiri Lowassa analielewa hili.
 
Watanzania bwana hizo sera anazozisema kwa dakika kumi ni zipi?ulishaona wapi katika chaguzi barani africa tu mgombea ananadi sera dakika kumi?na hata kwa nchi zilizoendelea ulishawahi ona mgombea anaongea dakika kumi kunadi sera?tuache ushabiki hata kama unahitaji mabadiliko angalia hayo mabadiliko yanapatikanaje sio alimradi mabadiliko.

Kwahio kutishia watu nchi kua kama Libya, ndo sera? Wapo watangulizi wanaonadi sera na yeye anamalizia. Watakanabwabwaje vitu gani? Watanzania tulio wengi we just need a change. Tuone mawaziri wapya wenye fikra chanya. Sio watu utafikiri waliajiliwa kuwa mawaziri miaka nenda rudi. Lowassa tosha!
 
Sterlling hafi kwenye filamu. Lowassa ndo sterlling wa siasa za mwaka huu. Kila moja kutoka ccm ana haha. Kila anapokwenda anafagia. Mpaka magufuli naye anasema peopleeeeees! Mwaka huu mutaweweseka sana ma sisiem
 
Kwahio kutishia watu nchi kua kama Libya, ndo sera? Wapo watangulizi wanaonadi sera na yeye anamalizia. Watakanabwabwaje vitu gani? Watanzania tulio wengi we just need a change. Tuone mawaziri wapya wenye fikra chanya. Sio watu utafikiri waliajiliwa kuwa mawaziri miaka nenda rudi. Lowassa tosha!

Mahaba ya namna hii ni ugonjwa
 
chuki ni ishara hamaki au kuchanganyikiwa, lakini kubwa zaidi ni kutanguliza mbele maslahi binafsi au uchu wa kulinda mafaili
 
Mahaba ya namna hii ni ugonjwa

Mbona hata wewe mwenyewe una mahaba na chama tawala. What you should do ni kunishawishi kwanini niivhague ccm tena? Of which hamna tena huo ushawishi kwa wengi. Ndomaana ccm wanaona hawajibu shutuma, kebehi, matusi, yupo bize. Sawa mwatwambia ni fisadi, kwani kwenye urodha ya watu 11, alikua wa 9, hawa kumi wako wapi? Mbona hamuwasemi? Kwanza nani msafi ndani ya chama chakijani? Hakuna! Kwahio tusidanganyane hapa, akichaguliwa atakua na safu yake ya uongozi na atafanya kazi. Kwanza, nani ameandika ccm itawale milele? Walibweteka hawakusoma nyakati ndo maana sasa wana msumbua bure magufuli. Kazi ipo kweli mwaka huu. Tabia ya ccm ya business as ussual ndo leo hii inawatokea puwani.
 
Watu wanasema ukweli halafu ninyi eti mnasema vijembe.

Huyu Lowassa ni fisadi na mgonjwa sana.

Unataka ajibu nini wakati anaambiwa ukweli.



TAKUKURU wanafanya kazi gani kama yeye ni fisadi na bado yuko huru? Mnajazwa ujinga na mnakubali tu.
 
Last edited by a moderator:
Namkubari lowassa anayofanya ndiyo raha ya siasa. Siasa cyo kupanda jukwaan na kuropoka ropoka tu juu ya upinzan
 
Wewe bisha ila huo ndio ukweli, wapi lowasa kamtukana mtu pamoja na matusi yote anayorushiwa, Magufuli binafsi nilimuona wa maana ila naye kaingia kulekule, sera zimeisha au.........

Unaweza kubainisha matusi japo mawili tu alilotukanwa Lowassa
 
Lowasa safi sana...Tena Kwa ile ilani....Akitimiza mambo manne tu...Tanzania itakuwa Level Nyingine
 
Na wajiandae kisaokolojia kwani sympathetic votes inaweza kufikia milion moja mpaka sasa kura ambayo kisiasa si rahisi kuiona athari yake. Endeleeni kutukana huku mkiwaonyesha watz nini maana ya mti wenye matunda.
 
Back
Top Bottom