Nimependa siasa za Lowassa

Nimependa siasa za Lowassa

Watu wanasema ukweli halafu ninyi eti mnasema vijembe.

Huyu Lowassa ni fisadi na mgonjwa sana.

Unataka ajibu nini wakati anaambiwa ukweli.



Heri yako usie iba, wala kujua rushwa ..
 
Last edited by a moderator:
Lowassa ni master mind,

...kama James Hadley Chase. Ukianza kusoma kitabu chake huwachi. Sasa haya ma-CCM yameshaingizwa mkenge yanazungumza Lowassa kila kona wakati kwenye ilani ya kitengo hakuna japo neno 'Lowassa'
 
Ukifuatilia kwa makini siasa za mh Edward Lowassa utaona tofauti kubwa sana kati yake na wanasiasa wengine, lowassa amekuwa mhanga wa matusi, kebehi, kashfa na siasa za maji taka.

Lakini kinachonifurahisha kuhusu huyu bwana, hakuna hata siku utamamsikia akimjibu mtu, akimtupia dongo, akimuongelea mtu. Lakini wanasiasa wengine hasa wa ccm, wamesahau kunadi sera zao na kubaki wakimjadili yeye tu na kusahau sera ya vyama vyao. Mtego huo ameingia na magufuli, amebaki akitumia muda mwingi akimuongelea lowassa!! Wakati lowassa anaongelea wakulima wasikopwe, wazee wapewe pension nk.

Nimependa siasa za Lowassa, hasa kwa sababu hamjadili mtu anajadili issues.

CCM hawana kitu kingkne ziadi ya lowassa...yaaan hakuna sera wala kuzungumza watafanya nn kuhusu wananchi wao....wao ni lowassa tu...lowasaa tu... yaani wamedata kabisa....!!
 
Watanzania bwana hizo sera anazozisema kwa dakika kumi ni zipi?ulishaona wapi katika chaguzi barani africa tu mgombea ananadi sera dakika kumi?na hata kwa nchi zilizoendelea ulishawahi ona mgombea anaongea dakika kumi kunadi sera?tuache ushabiki hata kama unahitaji mabadiliko angalia hayo mabadiliko yanapatikanaje sio alimradi mabadiliko.
Siyo kila kitu lazima uige jitahidi kubuni cha kwako.

Staili ya kampeni ya Lowassa ni ya aina yake, juzi Jangwani alieleza vipaumbele vitano Elimu, Afya, Miundombinu, Kilimo na Utawala bora, ilitosha sana kwa mkutano mmoja.

Jana akiwa Iringa ameanza kufafanua vipaumbele vyake, kasema ataondoa ushuru kwa wakulima, mazao yao yakikopwa yalipwe na riba nk, hii nayo ilitosha kwa mkutano mmoja leo tena atafafanua kingine, huwezi kumaliza kila kitu kwa mkutano mmoja.

Kimsingi dk.10-20 zinatosha sana ukizingatia kampeni itachukua siku 60.
 
Watu wengine bana, kila siku kumuongelea Lowassa Lowassa Lowassa. Ivi kwann wasi deal na yao ??

Ukiona maadui wana ku discuss sanaa ujue they fear you.
 
Ni mfano wa watu kupambana na kutokata tamaa

Hakika. The winning spirit. Nimejifunza kumbe binadamu tunajichosha sana kwa kuhangaika kujibu juu ya watu wanakuwaza nini na kusema nini juu yako, unaacha kuconcentrate na mambo ya msingi. Lowassa hapotezi muda kuhangaika na mtu. Na hii inawauma sana ccm, maana walitegemea awe anawajibu ili wafanye siasa za mipasho. Kiufupi kawapoteza!!
 
Acha kukariri...Hata Obama ukimfuatilia sio mzungumzaji sana..... Maneno yake ni machache na yenye kueleweka. Siku zote ukweli hauna maneno mengi....
 
Kwani umemsikia magufuli akimtukana mtu? Analysisi yako ni mbovu. Unamuongelea Lowasa vis a vis CCM wote. Mbona humuongelie Lowasa na Ukawa nzima vis a vis CCM yote. Matusi ya Mbowe, Hiza hukuyasikia?
Magufuli kaongopa ukawa hawana ilani..
 
Lowasa akiongea anakwenda straight kwenye points nandio maana hutasikia akibwabwaja hovyo na kumuongelea mtu.
 
Watanzania bwana hizo sera anazozisema kwa dakika kumi ni zipi?ulishaona wapi katika chaguzi barani africa tu mgombea ananadi sera dakika kumi?na hata kwa nchi zilizoendelea ulishawahi ona mgombea anaongea dakika kumi kunadi sera?tuache ushabiki hata kama unahitaji mabadiliko angalia hayo mabadiliko yanapatikanaje sio alimradi mabadiliko.

Watu wengine bwana tabu tupu. Mtu anaonge saa zima kwenye hilo saa zima ya maana dakika tano tu. Sasa si bora mtaalam Lowassa dakika 10 na zote ni mambo ya msingi. Tuache kupenda porojo.
 
Jana kampeni Meneja wa ACT Wazalendo mbele ya watu alisema kwamba UKAWA wamesimamisha mgombea mgonjwa, hata ugonjwa anaoumwa haujulikani sijui ni degedege au kifafa!

Pamoja na kwamba Zitto alimuombea msamaha kiana kwamba bado ni mtoto katika siasa.

Lakini mimi nasubiri kuona NEC itachukuwa hatua gani? Kama itanyamaza kama ilivyo munyamazia Mkapa.

Basi UKAWA wakianza kujibu mapingo ya matusi hayo NEC ibebe lawama zote.

Maana dawa ya moto ni moto.

BTW, hivi adhabu ya chama kinachokiuka maadili ya kampeni iliyosainiwa na vyama vyote ni nini?

Mwenye kufahamu ninaomba anielimishe.
 
Ukifuatilia kwa makini siasa za mh Edward Lowassa utaona tofauti kubwa sana kati yake na wanasiasa wengine, lowassa amekuwa mhanga wa matusi, kebehi, kashfa na siasa za maji taka.

Lakini kinachonifurahisha kuhusu huyu bwana, hakuna hata siku utamamsikia akimjibu mtu, akimtupia dongo, akimuongelea mtu. Lakini wanasiasa wengine hasa wa ccm, wamesahau kunadi sera zao na kubaki wakimjadili yeye tu na kusahau sera ya vyama vyao. Mtego huo ameingia na magufuli, amebaki akitumia muda mwingi akimuongelea lowassa!! Wakati lowassa anaongelea wakulima wasikopwe, wazee wapewe pension nk.

Nimependa siasa za Lowassa, hasa kwa sababu hamjadili mtu anajadili issues.

Awe mungwana asiwe mungwana Ikulu ataisikia tu namipango yake yote ya Fujo ipo Wazi mtakimbiaaa wote nchi itabaki salama
 
Ukifuatilia kwa makini siasa za mh Edward Lowassa utaona tofauti kubwa sana kati yake na wanasiasa wengine, lowassa amekuwa mhanga wa matusi, kebehi, kashfa na siasa za maji taka.

Lakini kinachonifurahisha kuhusu huyu bwana, hakuna hata siku utamamsikia akimjibu mtu, akimtupia dongo, akimuongelea mtu. Lakini wanasiasa wengine hasa wa ccm, wamesahau kunadi sera zao na kubaki wakimjadili yeye tu na kusahau sera ya vyama vyao. Mtego huo ameingia na magufuli, amebaki akitumia muda mwingi akimuongelea lowassa!! Wakati lowassa anaongelea wakulima wasikopwe, wazee wapewe pension nk.

Nimependa siasa za Lowassa, hasa kwa sababu hamjadili mtu anajadili issues.
Ni mwanasiasa mkomavu sana. Ndiyi sababu kura yangu anaipata mapema sana asubuhi oct 25
 
kama unauzika,hoja na sera zako zinakubalika,una mvuto na unapendwa na watu kwa mahaba yote,.,.,hasira,matusi na jazba zitatoka wapi??
 
Umeona mkuu jogi eeh? Anavyoisoma taratibu ndio tunamuelewa.
Zile papara za Magufuli hadi anasema Watanzania wakichagua upinzani nchi itageuka kama Libya ndio sifa?
Taratibu ndio mwendo, na Lowassa anachanja mbuga hana muda na taarab za majukwaani.

Taratibu na tunafika
 
Last edited by a moderator:
Watu wanasema ukweli halafu ninyi eti mnasema vijembe.

Huyu Lowassa ni fisadi na mgonjwa sana.

Unataka ajibu nini wakati anaambiwa ukweli.



Bibi yako, babu yako, mama yako,na baba yako wewe pia hamjawai kuumwa?
 
Last edited by a moderator:
Lowassa fundi wa siasa? Mahaba niue

Wewe bisha ila huo ndio ukweli, wapi lowasa kamtukana mtu pamoja na matusi yote anayorushiwa, Magufuli binafsi nilimuona wa maana ila naye kaingia kulekule, sera zimeisha au.........
 
Back
Top Bottom