Ahmet
JF-Expert Member
- Oct 15, 2019
- 1,537
- 3,404
Heshima kwenu wakuu,
Bila kupoteza muda, Mimi ni kijana wa miaka 27, kwa Sasa nipo kusini mwa nchi lakini siku za usoni natarajia kuhamia Dodoma ili nipambane mbali na nyumbani.
Nimefanya maamuzi haya kwa kuzingatia Mambo mengi:
Kwanza, Dodoma Kuna fursa nyingi za kiuchumi ambazo zimechagizwa na uwepo wa watu wengi (wanafunzi wa vyuo, wabunge, mawaziri na wafanyakazi wengi wa umma). Huku kusini hasa Lindi, kusema ukweli kumesahaulika kabisa, idadi ya watu ni ndogo na mzunguko wa pesa ni mdogo sana.
Pili, Dodoma ni makao makuu ya serikali na ofisi nyingi za umma ziko Dom. Nikiwa hapo sitawaza tena kuhusu interview za utumishi ambapo awali nilikuwa siwezi kuzifanya kutokana na umbali, yaani kutoka huku kwetu hadi Dom kuja kufanya interview ingenighalimu Sana ukizingatia pia interview zinakuwa nyingi kwa post moja (oral na written)
Tatu, ninapafahamu Dodoma kwa uchache, kwasababu nimemaliza degree yangu UDOM, kwaiyo Dodoma ni jiji nalolijua.
Nne, natamani kukaa mbali na home.
Tano, nimepapenda Dodoma.
Changamoto nayoipata (swali nalojiuliza) kwa Sasa ni nini nitafanya nikiwa Dodoma? Na hapa ndio nahitaji mawazo ya wadau na wenyeji wa Dom mnipe faida na hasara, raha na shida za kukaa Dom.
Mwenyewe niliwaza kufanya shughuli hizi,
Kwanza, Bodaboda (kwakua nina kamtaji kidogo naweza nunua pikipiki yangu hata used na Kuanza nayo biashara)
Pili, kuuza nguo na bidhaa nyengine ndogondogo
Tatu, shughuli yeyote ya mtaani Kama kubeba zege, kufyatua matofari n.k.
Kwasasa najipanga ili nisije mikono mitupu katika miji ya watu, nasubiri kidogo nijichange change ili nije vizuri.
Najua huu ni mpango tu na unaweza usiwe sahihi Sana, hivyo nahitaji ushauri wenu wadau, hali ikoje hapo makao makuu? Bei za vyumba vya kupanga ikoje?
Ushauri wenu ni wamuhimu sana, karibuni wanajamiiforums
Bila kupoteza muda, Mimi ni kijana wa miaka 27, kwa Sasa nipo kusini mwa nchi lakini siku za usoni natarajia kuhamia Dodoma ili nipambane mbali na nyumbani.
Nimefanya maamuzi haya kwa kuzingatia Mambo mengi:
Kwanza, Dodoma Kuna fursa nyingi za kiuchumi ambazo zimechagizwa na uwepo wa watu wengi (wanafunzi wa vyuo, wabunge, mawaziri na wafanyakazi wengi wa umma). Huku kusini hasa Lindi, kusema ukweli kumesahaulika kabisa, idadi ya watu ni ndogo na mzunguko wa pesa ni mdogo sana.
Pili, Dodoma ni makao makuu ya serikali na ofisi nyingi za umma ziko Dom. Nikiwa hapo sitawaza tena kuhusu interview za utumishi ambapo awali nilikuwa siwezi kuzifanya kutokana na umbali, yaani kutoka huku kwetu hadi Dom kuja kufanya interview ingenighalimu Sana ukizingatia pia interview zinakuwa nyingi kwa post moja (oral na written)
Tatu, ninapafahamu Dodoma kwa uchache, kwasababu nimemaliza degree yangu UDOM, kwaiyo Dodoma ni jiji nalolijua.
Nne, natamani kukaa mbali na home.
Tano, nimepapenda Dodoma.
Changamoto nayoipata (swali nalojiuliza) kwa Sasa ni nini nitafanya nikiwa Dodoma? Na hapa ndio nahitaji mawazo ya wadau na wenyeji wa Dom mnipe faida na hasara, raha na shida za kukaa Dom.
Mwenyewe niliwaza kufanya shughuli hizi,
Kwanza, Bodaboda (kwakua nina kamtaji kidogo naweza nunua pikipiki yangu hata used na Kuanza nayo biashara)
Pili, kuuza nguo na bidhaa nyengine ndogondogo
Tatu, shughuli yeyote ya mtaani Kama kubeba zege, kufyatua matofari n.k.
Kwasasa najipanga ili nisije mikono mitupu katika miji ya watu, nasubiri kidogo nijichange change ili nije vizuri.
Najua huu ni mpango tu na unaweza usiwe sahihi Sana, hivyo nahitaji ushauri wenu wadau, hali ikoje hapo makao makuu? Bei za vyumba vya kupanga ikoje?
Ushauri wenu ni wamuhimu sana, karibuni wanajamiiforums