Nimemwaga mboga...lakini nafsi inanisuta.

Mkuu ni kweli umekosea na jambo moja zuri na wewe umelitambua hilo. Ujue umeumiza feelings za hao wana ndoa - nina uhakika kwa sasa hakuna maelewano, chakufanya hapa waite mbele ya mke wako ujaribu kuwaelewesha na uwaombe msamaha. Fikiria hii ingetokea kwako je?
 
Mzee mengine nimeona niyaache kwanza ila hili nitalijibu hapa ingawa si mahala pake, kwa bahati mbaya hapa hatujuani kwa majina ila niamini ninapokuambia nimepata bahati ya kuishi sehemu nyingi duniani kwa vipindi tofauti tofauti, nimeishi karibu mabara yote ya dunia tena nikiwa na bahati ya kushuhudia mabadiliko makubwa makubwa makubwa.

Nimeishi wakati sheria za ubaguzi zinaishia ishia Marekani, nimeishi wakati Russia ikiwa ni taifa kubwa, nimeishi ujerumani wakati ukuta wa Berlin ukianguka na pia nilikuwa Rwanda wakati Genocide inalipuka, nime save Bosnia kama askari wa kulinda amani na nilikuwa volunteer wa uchaguzi juzi wakati Bingu wa Mutharika wa Malawi aningia madarakani kwa matumaini makubwa.

Niamini ninapokuambia hakuna system iliyokamilika duniani na hakuna mwenye suluhisho la matatizo yoote ya mwanadamu in one package, so misimamo yangu ya kisiasa haina uhusiano kabisa na suluhu ya maisha bora kwa kila mtu. Siamini na sitegemei kuona jamii inayoishi kama peponi, kwa bahati mbaya sana pia mimi ni mjamaa hivyo naamini katika misuguano katika jamii na matabaka yanayo sababishwa na ukomo wa resources.

Nitampinga na kumdharau kila mwanasiasa anayewahadaa watu kuwa yeye ni mtume mwenye suluhu ya matatizo ya watu. Hii ni falsa yangu na ndio inayoniongoza katika misimamo yangu yangu.

Kwa hiyo pamoja na exposure kama hiyo bado unafanya maamuzi au kuongea vile kama vile? Kama wewe ni askari wa kulinda amani kwa maamuzi kama hayo utakuwa unakiuza kikosi chako kwa adui. Seruously. Sheria za ubaguzi ziliisha lini Marekani??? Tuyaache hayo. Jibu lile swali lingine. Kwa nini ulidhani atakuhaibisha au kukudhalilisha?
 
...........wakati mwingine huwa siamini kama kuna haja ya kuendelea na mawasiliano na x's zetu na wewe unazidi kunithibitishia hilo,ona ulivyoharibu familia ya mwenzio hata kama mlikuwa na nia nzuri na huyo mke wa mtu!umefanya kitu kibaya na malipo ni hapa hapa duniani
 
Namuonea huruma huyo mwanamke
anaonesha hajui to pick the right guys for her..

Mumewe ni mshamba kwa kuita watu kuja kuongea hiyo ishu..

Na wewe nae umemfanya ajute kwa kukusaidia.....

kwa namna moja jamaa alifanya poa alivomjibu kipuuzi//... kama alijaribu kuelimisha mlalamikaji kwa ustaarabu hakuelewa.. wanakutanishwa mezani jamaa anakuja na kundi ka mchiriku unatarajia mtuhumiwa afaneje.. ?!mbwai tu maadamu masapu keshafaulishwa!!
 
Yaani umejipunguzia point chache za kuitwa Mwanaume.....................nina mashaa na urijali wako!
 
KOSA SIO KOSA .......
Ikiwa uliweza kuulizia habari za hao watu ukaambiwa mdada hakwenda job na mjamaa hajaonekana.... chagua mmoja wa hao unaofanya nao kazi ambaye ana busara mueleze jinsi ilivyokuwa ili akiweza akuitie huyo jamaa muongee kiume (men to men),akifanikiwa kuja mueleze ukweli bila kuficha kitu pia mweleze kuilikua na haja gani mambo yenu ya watu wanne (2couples) yajadiliwe na grupu kubwa hivyo?kama alikuwa hajiamini basi angewakalisha meza tofauti na ya mazungumzo yenu,huyo jamaa amejifunza kitu na pia wewe umejifunza kitu
 
Kwa hiyo pamoja na exposure kama hiyo bado unafanya maamuzi au kuongea vile kama vile? Kama wewe ni askari wa kulinda amani kwa maamuzi kama hayo utakuwa unakiuza kikosi chako kwa adui. Seruously. Sheria za ubaguzi ziliisha lini Marekani??? Tuyaache hayo. Jibu lile swali lingine. Kwa nini ulidhani atakuhaibisha au kukudhalilisha?

Mkuu nimezaliwa mwaka 1969, na siku sema sheria za ubaguzi zimeisha, ila zinaishia ishia, hapa nilikuwa namaanisha ule ubaguzi wa Jim Crow laws ulipokuwa unaishia. Kama unakumbuka historia sheria ya civil act ya 1964 na voting right ya mwaka 1965 ndizo hasa zina mark kuishia ishia kwa ubaguzi, kwa maana hiyo wamerakani wengi weusi walianza kupiga kura baada ya mimi kuzaliwa. Hayo ya kuuza wenzangu hapo ninakiri sikuwa rational sana nilipo tamaka maneno hayo.

Nimeeleza kulikuwa na mawasiliano kabla kati yake na familia yangu na ile shutuma kama ninatembea na mke wake alikwisha itoa, kwangu mimi niliona ingekuwa ni jambo la busara yeye kuzumza na mimi na mke wangu lakini kutoa hizi shutuma mbele ya watu wengine tena ninaofanya nao kazi ni kutaka kunidhalilisha.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Nenda kaonane na huyu mume wa huyo dada wa RITA (ana kwa ana), na umueleze kwamba hiyo ilikuwa ni defensive mechanism baada ya kuona kundi kubwa la watu linakujia kwa ajili ya hicho kikao, ila mkuu usithubutu kurudia tena kitu cha namna hiyo.:gossip:
 
Shantel wanaume tumeumbwa na kitu inaitwa PRIDE nadhani hii ndio chanzo.
<br />
<br />
mme wangu hayumo kwenye hilo kundi,kwanza asingeenda kwenye meeting place.Agezuga anasafari.ukweli si hakuna mahusiano batili?ss akameet ili iweje
 
Km kweli we mwanajesh km nlivoelewa ktk coment yako then jamaa aliogopa akijua unaweza kumpiga thats why akaja na wenzake. Pia maaskari hamuaminiki ktk suala zima la mahusiano ndo mana akakazia muonane na mambo yawe sawia. Above all with that pride thng unachojifyagilia nacho sidhan kn una PRIDE ya kiume cuz ungekuwa nayo ungemwacha mkeo hapo ili nae asikie upuuz wako. Ulijua ulichotaka kusema ni cha kuumiza thats why ukamtoa mkeo ili asiumie, then ukaropoka ulichoropoka ukaiumiza famijy ya m2. I THNK INGEKUWA WEWE NDIE ULIEAMBIWA HAYO ULIYOMWAMBIA MWENZIO NAJUA TUNGEKUWA TUNASOMA KTK MAGAZETI TUKIO ila huyo mkaka ni mwerevu na ako na busara thats why aliondoka....! Unatakiwa umweleze mkeo ulichomwambia then mkeo aarange meeting nyingne mkutane 4 muyamalize. Ukiacha kumuinvolve mkeo ktk suluhu,eti u2me watu wenye busara then hakitaeleweka kamwe na zaid utafanya kidonda kikue! Mkeo ndie kombora lako la mwisho ktk kuijenga ndoa hyo tena....! Itakupa heshma na utaonekana m2 hata mbele ya hao co workers as watajua haukutembea na mke wa m2, ni hasira tu zilikuponza ukasema uliyosema. Ur wife is ur on duster brush and antstains u can use to erase ur mess. Mwisho...jifunze kucontrol hasira as most of pipo like u ending killed or kiling
 
mme wangu hayumo kwenye hilo kundi,kwanza asingeenda kwenye meeting place.Agezuga anasafari.ukweli si hakuna mahusiano batili?ss akameet ili iweje

Kulikuwa na mkanganyiko wa taarifa, tulikutana ili tujaribu ku clear hilo wingu, nadhani mume wako anafanya kazi yake vizuri sana ya kukufanya uamini yeye ni mtu msafasi kuliko watu wote huku duniani, mwambie Nduka anampa hongera sana
 
I wish ungejua complexity ya hiyo kitu unayoita 'kucontrol hasira'
<br />
<br />
i knw how complex it is...nilikuwa nakasirika hata m2 akipiga honi barabarani, nimevunja vunja vi2 vya thaman na mara kadhaa nilipona kupelekwa police kwa kuwashambulia watu kwa kunitania kidogo tu bt thanx to God now unaweza hata kunizaba vibao na nisikasirike! U can do it ukiamua...
 
Ukikasirika utadhani umekuwa posesd na demons, unakuwa so powerful ila ukipoa unakuwa mpole, muoga na mwenye mawazo sana....ukizembea unaweza hata kujiua as unaweza dhani unaonewa ktk kila jambo.
 
i knw how complex it is...nilikuwa nakasirika hata m2 akipiga honi barabarani, nimevunja vunja vi2 vya thaman na mara kadhaa nilipona kupelekwa police kwa kuwashambulia watu kwa kunitania kidogo tu bt thanx to God now unaweza hata kunizaba vibao na nisikasirike! U can do it ukiamua...

Najitahidi sana, kwa wanao nifahamu toka nilipokuwa mdogo hadi leo wanaweza kuliongelea hili vizuri, ila siwezi kuchukua point kuwa mwenyewe nimeweza kwa kuwa kiwango kikubwa nilikuwa kwenye program nyingi za anger mangement chini ya madaktari bingwa kabisa. Ila nakuambia it even harder than kuamua tu.
 
Mkuu nimezaliwa mwaka 1969, na siku sema sheria za ubaguzi zimeisha, ila zinaishia ishia, hapa nilikuwa namaanisha ule ubaguzi wa Jim Crow laws ulipokuwa unaishia. Kama unakumbuka historia sheria ya civil act ya 1964 na voting right ya mwaka 1965 ndizo hasa zina mark kuishia ishia kwa ubaguzi, kwa maana hiyo wamerakani wengi weusi walianza kupiga kura baada ya mimi kuzaliwa. Hayo ya kuuza wenzangu hapo ninakiri sikuwa rational sana nilipo tamaka maneno hayo.

Nimeeleza kulikuwa na mawasiliano kabla kati yake na familia yangu na ile shutuma kama ninatembea na mke wake alikwisha itoa, kwangu mimi niliona ingekuwa ni jambo la busara yeye kuzumza na mimi na mke wangu lakini kutoa hizi shutuma mbele ya watu wengine tena ninaofanya nao kazi ni kutaka kunidhalilisha.

Nimekupata. Labda uwatumie hao hao unaofanya nao kazi wakamweleze jamaa ukweli wenyewe? Maana ukienda wewe mwenyewe si anaweza akakututoa nduki? Ila hii imekaa vibaya. It could go either way. Au mtafute mtu toka dini yako (shehe au mchungaji) akamweleze ukweli na kuwa ulisema uliyosema kwa kuwa una matatizo ya anger tokea ukiwa mdogo na bado upo kwenye anger management program? Then kama akipooza ukamwombe radhi personally.
 
Nimekupata. Labda uwatumie hao hao unaofanya nao kazi wakamweleze jamaa ukweli wenyewe? Maana ukienda wewe mwenyewe si anaweza akakututoa nduki? Ila hii imekaa vibaya. It could go either way. Au mtafute mtu toka dini yako (shehe au mchungaji).

Naogopa kurudia kosa la kuwashikirisha watu wengi na mimi nisije kumkera na yeye, hapo kwenye bold wasiwasi wangu hawa mabwana ukiwapa hata issue ndogo mtamaliza mwezi mnasuluhishwa, jamaa tunasali naye msikiti mmoja na pia hata viongozi wa msikiti wanatufahamu toka zamani ila option hii naiogopa nikiwaza jinsi litakavyogeuzwa jambo kubwa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom