Nimemuomba aje tuishi, tufunge ndoa hataki

Nimemuomba aje tuishi, tufunge ndoa hataki

Tafuta utakaependana nae,..ndo ya wanaopendana itadumu,..ila hyo ya ku'utilize loop hole' n matatzo unatafta..
 
wanaume jamani, akijua una shida atayiiweza huo udhaifu atautumia vibaya hadi ujute kumfahamu
 
Aisee uko na wazo la kimbuzi sana.. Alafu hauna uhalisia na maisha uliyo yaandika.... Labda hayo ya complicated relationship unaweza ukawa kweli uko ndo maana una story za kiivyo tu.
 
Wadau nawasalim,

Kuna mshikaji wangu tulikua tunakaa gheto moja 2005_2007 tuliishi kama ndugu kwa kweli, bahati mbaya 2008 akatangulia mbele za haki.

2010 kuna mdogo wake wa kike aliewahi kututembelea siku za nyuma wakati kaka yake yupo hai akanipigia simu kuwa anaomba kuja mjini afikie kwangu aje kujaribu maisha town, kwa kuwa kuna mdogo wangu wa kike niliekua naishi nae hapo nikaona haina shida aje tu wawe kampani moja.

Akaja, akajiunga na kozi ya hotel mgmt, wakawa hawaishi kugombana na mdogo wangu, yule binti akatoka kwangu na kwenda kuishi kwa ndugu mmoja wa ukoo, lakini ikawa kila mara anafika kazini kwangu kuomba hela za kujikimu, baadae akajiunga kwa certificate of business administration, alinisumbua sana wakati wa kozi hii, maana ada hana ikawa ni kuunga unga tu, nilimsaidia sana, hadi akamaliza

Sasa amejiunga tena chuo kwa ajili ya diploma in business admin academic year iliyoanza November nadhan, akalipa pesa kidogo tu akawaambia December atapeleka zingine, sasa amekuja kwangu juzi, huwa ananiita kaka, akasema ""kaka nisaidie fedha kiasi nikatatue shida za shule, sina hela ya hostel, fees, transport, na nimezuiwa kuingia class.

Nikamwambia, ""mama"" nimeshakusaidia sana huko nyuma, sijanufaika na chochote, sasa basi huna haja ya kuhangaika kiasi hicho, fanya hivi beba mizigo yako yote uje tuishi, tufunge ndoa tuishi kama mke na mme, nitagharamia elimu yako hata hadi degree ukitaka, Chuo unaweza kusoma huku ukiwa umeolewa, na bahati nzuri nimeshamaliza nyumba nimehamia tayari, njoo ujinafasi.

Cha kusikitisha akaanza kujiuma uma, ooh nina mtu wangu, yakaenda yakarudi, na ushenzi mwingine mwingi unaofanana na huo,
Miaka yote niliyokua nakusaidia maisha kama mdogo wangu huyo mpenzi alikua wapi, ingawa nilikua namsaidia kama mdogo wa marehemu rafiki yangu lakini sasa gharama zimeshakua kubwa, pia nami kama mwanadam niliekamilika nimeona nimsaidie kwa muoa hata roho ya ndugu.yake itapumzika kwa amani, anaanza ngonjera.

Mm hadi sasa nimekua na complications nyingi kwenye mapenzi sasa nikaona bora nimchukue huyu binti, siwezi kumlipia hizo gharama kabla ya kumuoa maana nawajua wasichana vizuri atakuja kunigeuka akamaliza chuo, ila nikimuweka ndani, nikapiga na mimba moja mbili hatakua na ujanja tena wa kunigeuka.

Achague moja asome kwa mateso hivyo hivyo kwa kuomba omba, au aje watu wale mpunga asome kwa starehe huku akipunga upepo wa ununio beach nilikohamia.
H
Au wadau mlikua mnasemaje?

Misingi ya ndoa ni mapenzi kati ya watu wawili na siyo huo uroho ulionao
 
Watu kila siku wanalalamika wamepigwa chini baada ya kusomesha we bado unataka kwenda huko, au unataka uje uombe tena ushaurii...

Achana nae akafie mbele
 
Watu kila siku wanalalamika wamepigwa chini baada ya kusomesha we bado unataka kwenda huko, au unataka uje uombe tena ushaurii...

Achana nae akafie mbele

Acha kumbania mwenzio khaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom