Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

Wanabodi,

Naomba kukiri kumfahamu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kitambo kidogo na kuwahi kukutana naye na kutambulishwa kwangu, kiukweli nilimuona ni mtu anayejisikia sana!, anajiona sana na anainga sana, ukijumlisha na zile kauli zake za utumbo utumbo enzi zile, kiukweli kabisa nilimuona ni mtu wa hovyo hovyo tuu hata apewe madaraka gani!. Hivyo alipoteuliwa kuwa DC wa Kinondoni, mengi aliyoyafanya niliyahesabu ni muendelezo wa kutafuta masifa tuu!.

Kwa maoni yangu, niliona nafasi za UDC ni wastage of time, money and resources, na ma DC zaidi ya kuwa wakuu wa kamati za ulinzi na usalama za wilaya, ni watu wasio na lolote la maana la kufanya, lakini DC Makonda, ameupa u DC hadhi, Ma DC sasa wanaonekana ni watu wa maana, na DC wa Kinondoni anaimpact kuliko hata RC, hivyo position inayomstahiki ni kuwa RC wa DSM!.

Leo nimemsikia akizungumza katika tukio la Malkia wa Nguvu lililoushwa live na Clouds TV, kiukweli nimeguswa sana na aliyoyasema kuhusu bughudha kwa wafanyabiashaa ndogo ndogo kuzungushwa kuhusu vibali!.

Akamuagiza ofisa biashara wake kokote aliko, kama hakutazama TV, au kusikiliza redio kuhusu agizo hilo, then mke wake au watoto wake watakuwa wamesikia hivyo wampe ujumbe baba yao kuwa kuanzia Jumatatu, hakuna kukaa ofisini kubugudhi vafanyabishara, bali atoke nje kukagua biashara na kutoa leseni papo kwa papo, na yeye DC kwa upande wake, kuanzia Jumatatu, ataweka dawati maalum la wafanyabiashara watakao bughudhiwa au kuzungushwa zungushwa, waripoti kwake direct, halafu huyo ofisa anayewazungusha, ataipata habari yake!.

Kiukweli, watu wa aina ya DC Makonda, ndio wanaohitajika kukabidhiwa jiji kama la Darisalama, kiukweli jiji litanyooka!.

Natoa wito kwa Mhe. Rais Magufuli, kufuatia RC wa DSM, Said Meck Sadick kufikisha umi wa kustaafu kwa mujibu wa sheria, (just by look), tunakuomba ututeulie DC Makonda awe RC wa DSM, atakusaidia sanna wewe na serikali yako, kayika utekelezaji wa falsafa yako ya "HAPA KAZI TUU!".

Katika sherehe hiyo ya Malkia wa Nguvu, DC Makonda amedhihirisha wazi yeye ni Balkia wa Nguvu!.

Hongea Sana DC Makonda, sasa unastahili U RC-DSM!.

Naomba kuwasilisha.

Pasco
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
Done!.

P.
 
Mkuu Pasco nadhani sasa wanakuelewa, Ilikuwa wazi Makonda atapewa Dar, tatizo waTz hatupendi mtu anayejituma tunataka wote tuwe wavivu ili tuwe walalamikaji. Hongera Makonda
 
Mkuu Paskali hapo mwisho sijakuelewa umeandika,Wewe ni balkia wa nguvu''naomba maana ya neno balkia.
Nimsaidie kama Ntaweza. Nikishindwa Pasco ingilia kati kusaidia: Malkia ni wa kike (Mama) na Balkia ni wa kiume(Baba) ! Si ndio Pasco?
 
Wanabodi,

Naomba kukiri kumfahamu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kitambo kidogo na kuwahi kukutana naye na kutambulishwa kwangu, kiukweli nilimuona ni mtu anayejisikia sana!, anajiona sana na anainga sana, ukijumlisha na zile kauli zake za utumbo utumbo enzi zile, kiukweli kabisa nilimuona ni mtu wa hovyo hovyo tuu hata apewe madaraka gani!. Hivyo alipoteuliwa kuwa DC wa Kinondoni, mengi aliyoyafanya niliyahesabu ni muendelezo wa kutafuta masifa tuu!.

Kwa maoni yangu, niliona nafasi za UDC ni wastage of time, money and resources, na ma DC zaidi ya kuwa wakuu wa kamati za ulinzi na usalama za wilaya, ni watu wasio na lolote la maana la kufanya, lakini DC Makonda, ameupa u DC hadhi, Ma DC sasa wanaonekana ni watu wa maana, na DC wa Kinondoni anaimpact kuliko hata RC, hivyo position inayomstahiki ni kuwa RC wa DSM!.

Leo nimemsikia akizungumza katika tukio la Malkia wa Nguvu lililoushwa live na Clouds TV, kiukweli nimeguswa sana na aliyoyasema kuhusu bughudha kwa wafanyabiashaa ndogo ndogo kuzungushwa kuhusu vibali!.

Akamuagiza ofisa biashara wake kokote aliko, kama hakutazama TV, au kusikiliza redio kuhusu agizo hilo, then mke wake au watoto wake watakuwa wamesikia hivyo wampe ujumbe baba yao kuwa kuanzia Jumatatu, hakuna kukaa ofisini kubugudhi vafanyabishara, bali atoke nje kukagua biashara na kutoa leseni papo kwa papo, na yeye DC kwa upande wake, kuanzia Jumatatu, ataweka dawati maalum la wafanyabiashara watakao bughudhiwa au kuzungushwa zungushwa, waripoti kwake direct, halafu huyo ofisa anayewazungusha, ataipata habari yake!.

Kiukweli, watu wa aina ya DC Makonda, ndio wanaohitajika kukabidhiwa jiji kama la Darisalama, kiukweli jiji litanyooka!.

Natoa wito kwa Mhe. Rais Magufuli, kufuatia RC wa DSM, Said Meck Sadick kufikisha umi wa kustaafu kwa mujibu wa sheria, (just by look), tunakuomba ututeulie DC Makonda awe RC wa DSM, atakusaidia sanna wewe na serikali yako, kayika utekelezaji wa falsafa yako ya "HAPA KAZI TUU!".

Katika sherehe hiyo ya Malkia wa Nguvu, DC Makonda amedhihirisha wazi yeye ni Balkia wa Nguvu!.

Hongea Sana DC Makonda, sasa unastahili U RC-DSM!.

Naomba kuwasilisha.

Pasco
Wewe jamaa hukusomea uandishi wa habari bali ulisomea usanii wa kuishi
 
Mwambie kwanza afute mpango wake wa kutupandisha bure cc walimu yani tupande bila kulipa kwani haya madaladala ya babayake? Hatutaki vya ubwete amwambie magu atuongeze posho zetu
Hapo ataonekana akili zake zimekaa sawa. vinginevo ataendelea kuwa
Mkuu INSPECTOR MWALLA , naona hutaki kushonewa uniform ili nawe usafirishwe bure?
1461101072214.jpg
 
Nimsaidie kama Ntaweza. Nikishindwa Pasco ingilia kati kusaidia: Malkia ni wa kike (Mama) na Balkia ni wa kiume(Baba) ! Si ndio Pasco?
Mkuu Albert, umepatia kabisa, tena hapa kitu walichofanya Clouds ni kuunda neno jipya, lugha sio static, ni dynamic, hence changes with time, yaani ni a living thing, maneno mapya yanazaliwa huku mengine yanakufa!, mfano Masaburi ni jina la mtu, Didas Masaburi, sasa hivi mtu akikuambia masaburi yako ni tusi!. Kihiyo pia ni jina la mtu, lakini sasa neno kihiyo ni sifa fulani mbaya, hivyo Clouds wametuundia neno balikia!.

Pasco
 
Wewe jamaa hukusomea uandishi wa habari bali ulisomea usanii wa kuishi
Mkuu Mmawia, kwenye alimu yetu tuna mikondo miwili tuu mikuu ambayo ni sayansi au arts, sasa ats zozote ni sanaa, hata siasa ni sanaa tuu, bali ili kuipa hadhi siasa isionekane ni usanii, wakaamua kuuita sayansi ya siasa!.

Lakini kwenye hili la usanii wa kuishi, kwa bahati nzuri sana, mimi nafanya uandishi just for the love of it, tena nafanya bure!, siutegemei uandishi kwa kuishi na kuendesha maisha yangu!.

Pasco
 
Mkuu Mmawia, kwenye alimu yetu tuna mikondo miwili tuu mikuu ambayo ni sayansi au arts, sasa ats zozote ni sanaa, hata siasa ni sanaa tuu, bali ili kuipa hadhi siasa isionekane ni usanii, wakaamua kuuita sayansi ya siasa!.

Lakini kwenye hili la usanii wa kuishi, kwa bahati nzuri sana, mimi nafanya uandishi just for the love of it, tena nafanya bure!, siutegemei uandishi kwa kuishi na kuendesha maisha yangu!.

Pasco
Teeeeeeeeh teeeeeeeeh, pasco wacha kutudanganya kama watoto wa chekechea kwa tanzania ya sasa hakuna mtu anafanya kazi kwa mapenzi!
 
Teeeeeeeeh teeeeeeeeh, pasco wacha kutudanganya kama watoto wa chekechea kwa tanzania ya sasa hakuna mtu anafanya kazi kwa mapenzi!
Mkuu Mmawia, wengi humu hatufahamiani kiuhalisia zaidi ya kupitia michango yetu humu jf!, mimi kila siku najitambulisha kama mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, niliachishwa kazi rasmi mwaka 2002 tangu hapo sikuwahi kuajiriwa tena!.

Kazi za uandishi wa kujitegemea mtu unalipwa per story published, lakini kiwango jinacholipwa ni kidogo mno!. Mimi ninashughuli nyingine ninayoifanya inayoniingizia kipato cha kuendeshea maisha yangu na sio huu uandishi wa habari!, hii kazi ya uandishi, ninaifanya kwa kujitolea tuu, just for the love of it!, nasubmit stories zangu newsroom bure, na sihitaji kulipwa hata senti tano na media yoyote!, yaani nafanya kazi ya bure kwa kujitolea tuu just for the love of it!.

Kama miongoni mwa thawabu binadamu anazopata ni pamoja na kufanya kazi bure kwa kujitolea, then mimi Pasco wa JF, nimeishajiwekea akiba kubwa za thawabu za mabilion, hata nikiitwa leo/kesho, ujue Pasco wa jf ni moja kwa moja peponi!.

Pasco
 
Mkuu Mmawia, wengi humu hatifahamiani zaidi ya kupitia michango yetu!, mimi kila siku najitambulisha kama mwandishi wa habari wa kujitegemea, niliachishwa kazi rasmi mwaka 2002 tangu hapo sikuwahi kuajiriwa tena!. Sasa kazi za uandishi wa kujitegemea mtu unalipwa per story published, lakini kiwango ni kidogo mno!. Sasa mimi ninashughuli nyingine ninayoifanya inayoniingizia kipato cha kuendeshea maisha yangu na sio uandishi wa habari!, lakini hii kazi ya uandishi, ninaifanya kwa kujitolea tuu, just for the love of it!, nasubmit stories zangu newsroom na sihitaji kulipwa hata senti tano!, yaani nafanya kazi ya bue for the love of it!.

Kama miongoni mwa thawabu binadamu anazopata ni pamoja na kufanya kazi za kujitolea bure, then nimeishajiwekea thawabu za mabilion, hata nikiitwa leo/kesho, ujue Pasco wa jf ni peponi moja kwa moja!.

Pasco
Wacha masihara pasco kumbe ninavyo kuonaga unatoka jasho kibao kumbe unafanya kazi ya bure?wewe ndiye mtanzania wa kwanza hongera sana,nina imani mh rais atakutupia jicho labda unaweza kupata ka wilaya
 
Teeeeeeeeh teeeeeeeeh, pasco wacha kutudanganya kama watoto wa chekechea kwa tanzania ya sasa hakuna mtu anafanya kazi kwa mapenzi!
Tupooooo.Nami ni mmoja wao. Mwingine, kwa maoni yangu, ni Mheshimiwa JPJM, Raisi wa sasa wa Tanzania. Sema tu TUKO wachache, na kwa sababu WENGI wanafanya kazi bila mapenzi ya dhati, bali WANATAKA fedha, watu wengi wetu katika jamii hudhani kuwa:
"Kwa Tanzania ya sasa hakuna mtu anafanya kazi kwa mapenzi."
 
Back
Top Bottom