Nimewaza tuu process ya kifo..Nyie kufa kuna maumivu acheni..yani kuna ile hali unapitia kwny mwili hakuna mtu anaejua unayoyapitia..juzi bana nimeenda kwny kuvunja kikoba sijui kile chakula ilikua ni ajee...yani usiku maumivu yalivyoanza ni kama naota...ila nikaamka laivu nakuta tumbo hapa juu maumivu yake si mchezo ni kama nimekula asidi imejaa pomoni..yani jasho lilinitoka moyo unaenda mbio..nikaamka uzuri huwa nalala na chupa ya maji nikanywa nikaona kama ile sehemu ya juu ya tumbo inaachia lakini mwili unakosa balance nahisi kuanguka...nyiee nikasema ndo nakufa hivi jamani...nikasema nitembee tembee humo room huku nakunywa maji kidogo kidogo..baabdae nikakumbuka kuna ant acids huwa ninazo ndani nikazitafuna chapuu ndo kupata ahueni...
Nimewaza tuu mtoa mada jinsi atakavyopitia mateso pale atakapojinywea zake hiyo pombe..