Nimemchoka sana mama yangu

Nimemchoka sana mama yangu

hii story ni kama vile unaelezea maisha yangu kwa upande mwingine...
my late mama mdogo loved me so much kuliko mama,hadi leo hii hua najiuliza kama huyu mama kanizaa mimi....
nimeamini it takes both parents to have a one happy family...
my parents hawalali one room kitambo and that explains a lot why mum takes all her anger on me,kila nachofanya anaona kibaya...
i understand why she is being like that ndomana now nataka nisepe maybe in time she will realise that something is wrong with her and not me...
Njoo nikuhifadhi mtoto mzuri

Nikupe maisha unayo yaona kwa kina Kardashian
 
Jamani mimi uvumilivu wa kufanyiwa mambo ya kipuuzi sina na siangalii umri wala mtu,mungu ndio anahukumu kwa haki mimi mama yangu ananijua namuheshimu lakini akiniletea habari za ajabu ajabu namchana laivu kinoma noma na kwakua anafanyaga kweli makosa au kunikosea hua anaelewa na baadae tunaanza kuongea vizuri.Ila sasa hivi ameacha maana ameona hazinitoshi,na angeleta habari za kunimwagia radhi ningemrekodi na kushare kwenye wasap ili dunia nzima imchungulie

NB;mzazi akikosea harafu ukamwambia ukweli akakasirika na kukuvulia nguo usipate tabu wala usiwe na wasi wasi we mrekodi harafu share kwenye wasap ili achunguliwe dunia nzima maana atakua anataka kuchunguliwa
umenifanya nistop kulia kwa muda...nimcheka lol
 
Jamani mimi uvumilivu wa kufanyiwa mambo ya kipuuzi sina na siangalii umri wala mtu,mungu ndio anahukumu kwa haki mimi mama yangu ananijua namuheshimu lakini akiniletea habari za ajabu ajabu namchana laivu kinoma noma na kwakua anafanyaga kweli makosa au kunikosea hua anaelewa na baadae tunaanza kuongea vizuri.Ila sasa hivi ameacha maana ameona hazinitoshi,na angeleta habari za kunimwagia radhi ningemrekodi na kushare kwenye wasap ili dunia nzima imchungulie

NB;mzazi akikosea harafu ukamwambia ukweli akakasirika na kukuvulia nguo usipate tabu wala usiwe na wasi wasi we mrekodi harafu share kwenye wasap ili achunguliwe dunia nzima maana atakua anataka kuchunguliwa
Hahaha balaa lako ni kama sheikh aliyelishwa nguruwe
 
Pole sana inaonekana baba na mama ako hawakumaliza mahusiano yao vizuri so mama anahamishia hasira kwako
 
Habari zenu wapendwa,

Mimi ni msichana niliyemaliza chuo lakini natafuta kazi. Naishi na wazazi wangu na wadogo zangu wa kike ambao nawapenda sana. Nimekulia na kulelewa na bibi sana na mama mdgo ambao wote walikua wapole na wakarimu ila mama mdogo alitangulia mbele ya haki.

Nilimpenda sana mamdogo kuliko mama yangu mzazi kwasababu alinipenda na kuchukua nafasi ya mzazi wangu na ndiye aliyeniambia mume wake mama siyo baba yangu mzazi ( ila ni baba yao wadogo zangu ) nikiwa darasa la sita.
Niliumia sana kwasababu mama yangu alikuwa hana time kabisa kunieleza hayo. Hapo form one ndo nikaanza kuishi na mama yangu ila jamani ni mkali kwangu adi naliaga. Kuna siku nilimuuliza mama mdgo kama huyu kweli ni mama yangu mzazi au la akasema ndo mamako.

My mum hana ukaribu na mimi, ananifokea kila wakati bila hata sababu. Hanaga shukrani in anything i do. Uzuri darasani nilikua nafanya vzuri sana nikishuka position kidgo atafoka likizo nzima. Nilikua nashika nafasi ya nne nikiwa naongoza wasichana ila nikiwa tu wa tano ataongea likizo nzima.

Anavyokuwa ananiangalia, utafikiri yeye ndo mama yangu wa kambo hata akipiga honi ya gari getini nikiwa tu nje nilikua nakimbilia chooni. Anyway namshukuru kwasababu yeye ndo aliyenisomesha. (japo ni wajibu wake).

Tatizo ni pale mama anavyokuwa hana mother to daughter love au affection. Hajali what I do. Naweza kumuomba hela anakuwa mkali mpaka namwambia basi mama natafuta njia napata na haulizi ila wadogo zangu wanapewa hata extra. Mimi sijawahi kununuliwa simu na mama ila wao wananunuliwa tena mimi ndo namsindikizaga mama kununua na haniulizi mimi napata wapi simu.

Nikitaka tuongee labda angalau nimwambie kitu kinachonisumbua au just kupata faraja ya mama anaongea kwa ukali kwamba kachoka au bwanae ondoka ila roho inaniumaga. Marafiki zangu wanavyoongelea mama zao huwa nawatazama na kuwatamani.

Nyumbani kuna mfanyakazi lakini kazi zote nafanya mimi na mama humtetea dada na kusema mimi sina umuhimu ndani wakati kutwa nzima mimi ndo najishughulisha ila nakaaga kimya hadi nikiwa chuo nikija kusalimia huwa hataki niondoke ili nifanye kazi. Nikimwambia mama nina test atasema bwanae kwani wewe wa kwanza kusoma mpaka nakosa raha nikiwa chuo nakuwaga very lonely na mawazo. Sikufanikiwa kupata mkopo wala hela ya matumizi hvyo nilikua nahudumiwa na mama. Aisee sitokuja kusahau mateso niliyopata chuo.

Nimelala hungry nights mpaka ilibidi nizoee. Hapo ndo nikaona nitakufa nikaanza mahusiano na wanaume kisa nipate hela. Hapo mama uwezo anao wakunisaidia lakini anasema hana hela nitafute wanaume tena kwa ukali.

Anyway nilipunguza ukaribu na mama hata upendo kwasababu nilijaribu kuwa karibu nae nipate mapenzi ya mama lakini nikashindwa. Afu yeye ndo anasema nina roho mbaya, sina upendo kama wadogo zangu. Ninamwangalia tu kwasababu najua yeye ndo hanipendi. Na anasema hivyo kwasababu anawasikiliza sana yuko karibu nao but she pushes me away yaani utafikiri niliokotwa.

Kuna wakati huwa natamani niolewe ila ndoa ina majanga yake pia na sina hata mtu. Na hali ya mama imenifanya nikose upendo kwa watu wengne niponipo tu all alone. Kuna wakati nakaa tu na kulia na kinachoniuma nikiwa 7 yrs nilishawahi kubakwa kijijini kwa bibi na mfanyakazi ila sijawahi kumwambia mama wala mtu yeyote.

Watu watakua wanajiuliza mbona sitaji baba. Baba yangu ana familia yake mkoani na alishasahau kama ana mtoto. Baba yangu wa kambo yupoyupo tu but sana sana anawajali wanae ila hainiumizi roho. Ninachomuomba Mungu niondoke nipate kazi hata mkoani mbali na mama yangu.

NB. Wazazi wa hivi especially wamama jaribu kuweni karibu na watoto wenu kuweni na upendo. Mimi siwezi elezea kila kitu hapa ila umuhimu wa mamangu ni kunisomesha tu tena kwa maneno namshukuru sana kwa hilo.

Wapendwa sjui mtanisaidiaje but nimevumilia sana ni mama yangu huyo ndo maana wengne hukimbia kwao au kutaka ndoa haraka ili waondoke makwao.

Wazazi badilikeni tafadhali.
Lady Jay pole sana ujumbe wako umenitoa machozi maana naisi Mimi nawewe hii historia inafanana kuna wakati nasema bola walio yatima wana jua hawana wazazi wana amani Mimi naelewa inatesa sana hii imepelekea kuzaa Na kuwa single mother maana unajikuta unajiingiza katika mahusiano bila kutalajia pole mamy Mungu yupo mapito hayo bado nayapitia Mimi pia sina mapenzi Na mama yangu hata kidogo katika maisha sikuwahi kuipata upendo,furaha, najikuta napenda mama Wa wenzangu najisahau kama sio Wa kwangu Kiukweli sina upendo Na mama wala baba mama Na baba wanachukiana sana nimejikuta nampenda babu yangu bila babu nisingesoma Leo ata la kwanza Mimi nilitupwa kwenye kapu nje Na mwezi mmoja my dear mengine hatuwez kuyasema ndomana naangaika nisake kazi niondoke Mimi ata line nitabadili
 
Pole sana!
Kutakua na story nyuma ya kuzaliwa kwako... Wazazi wengine wanahamishia chuki na hasira kwa watoto.
Tafuta kazi ukipata hama hapo kajitegemee... Ipo siku mama yako atajirudi tu. Jaribu kumpenda hivyohivyo alivyo.
Mungu ndo amekukea kukufikisha hapo! Mtumaini yeye!
Ningumu sana mgesa wote niyametukuta ngumu Mimi kiukweli mama ,baba sina mapenzi nao
 
Kiukweli inauma sana na kama kunakidonda kinacholeta maumivu moyoni basis ni hiki....kupoteza au kutokupata penzi la wazazi...daima tunaamini mama au Baba ndio wenye mpnz ya dhati... Wao mapnz yao ni kama titi lilojaa utamu ambao huupati kwenye maziwa asali wala choculate au sehemu nyingine yoyote ileee....ni pnz hili linalofanya hata kama umezaliwa kwenye familia maskini kama Mimi uridhie hali ilee au ulale na njaaa utaona kawaida kabisa....kwasababu pnz LA dhati, adhimu na adimu umelikumbatia na kuliishi moyoni mwako!!!... Nakushauri njia pekeee ya kuondonakana na hali ya upweke ni kutafuta marafiki kama sio mitaani basi rudi kwenye dinii yako. Angalau utapata MTU ambaye utashare Naye maumivu haya yootee kwasababu kunaathari kubwa mno ya kuwa na mawazo mfululizo. Kwako na kwa kizazi chako. Kuwa makini sana juu ya hilo sii jambo LA kawaida kabisa. Mungu akusaidie upite salama kwenye bonde hili ngumu na lenye mtihani... Ubarikiwe.
Yeah inauma sana maumivu yake hayaelezeki
 
Japo na weza tofautiana na mawazo yako nna uhakika umemissunderstand mama yako,..
Kila kitu ni jinsi unavokichukulia, ukikichulia kwa ubaya unaweza ukawa chizi, ila ukichukilia kwa uzuri kitakupa baraka na kukupeleka mbali sana katika maisha,... Mama yako atakua anapitia insecurities zake kweny ndoa na moja wapo ya kitu icho ni wewe, anajaribu kukufundisha kitu,... Be independent kwa mfano, baba yako hakujali na unaishi na baba wa kambo, na yeye anapenda iyo ndoa yake isivunjike,... Jaribu kuchukua changamoto izo anazokupa kujiimarisha uwe strong kupitia maisha yako bila kutegemea watu, utafanikiwa
 
Pole sana mwombe mungu atakusaidia kwanza msamehe maana hajui atendalo ataona thamani yako baadae ukipata ajira kaa mbali nao atakutafuta
 
Duuh ebanee watu wanateseka hii dunia jaman.
Halafu unajkuta unaingia katika mahusiano bila kupenda huko nako unaumizwa arooooo hii mioyo ingekuwa inatoboka
Tungeshaoza wengi sanaaa zamani mnooo

Pole mkuu jikaze maana kuna wengine wamepitia zaidi ya hayo lakin wamejipa moyo now wameshasahau mapito
Jikaze.
 
Kwa maelezo yako inaonekana kuna kitu kimuathiri mama yako ambapo kila akikuona wewe kumbukumbu ya hicho kitu humjia...
Jaribu kudadisi alipo baba yako, pia tafuta historia ya mahusiano kati ya baba yako (mzazi) na mama yako yalikuaje. Uliza mama alipataje mimba yako.
Yawezekana mimba yako ilimkatisha masomo au ndoto zake kadhaa...
Yawezekana baba yako alimkataa baada ya kupata mimba...
Yawezekana alibakwa ndio akapata mimba...
Kuna baadhi ya watu huwa wanaweza kuzimudu hizo hali lkn baadhi hawawezi na chuki zao huishi miaka yote. Hii inawezekana pia imemtokea mama na hivyo chuki za tukio zinahamia kwako kwa sbb wewe pekee ndio humkumbusha tukio lenyewe.
Nakushari uwashirikishe watu wakubwa ili waweze kukusaidia kuongea na mama.
Pole sana.
 
Hiyo ni psychological problem, huenda baba yako alimlazimisha au kumbaka mama yako ndo akapata mimba yako, kumchukia baba yako Mzazi kinamfanya hata mama yako akuone kama unaroho kama ya baba yako Mzazi.

Muulize vizuri bibi kama anajua atakueleza ilikuwaje na utapata mwanga zaidi.

Na baada ya kujua hilo tatizo la mama hutomlaumu tena bali utamhurumia na utampenda zaidi. Huu ndo mchango Wangu kwako.
 
Pole sweetheart, Mimi mama yangu Nilikuwa nikimuudhi anasema lione n kufanana marehemu baba yako siufe km baba yako Hata kuzaa hutokuja kuzaa Wakati huo ndo Nilikuwa nimeolewa na sababu ya kuwahi kuolewa ni hayo matatizo ya kifamilia chuki yake kwa baba akaihamishia kwangu matokeo yake nimemchukia Mara mia zaidi yake.
 
Pole sanaa inauma lakini ndivyo ulipangiwa upitie ila ukivumilia utakuwa MTU wa kukimbiliwa na wengi me hata mama yangu sijui majina yake yote sijui umri wake sijui tareh ya kuzaliwa kwangu kwan nilipo muuliza aliniambia kwa kuisi I was disappointment ila nimemwamini Mungu ananivusha hadi kesho nimeishi na familia kumi na moja hatuna udugu kabisa nilianza kuishi na watu nikiwa na miaka 6 ivyo I was not experienced mother's love any more nilijipa moyo kwamba maisha nuliyo kuwa naishi ndo yakwangu kwan sikujua mjomba bandogo wala Shangaz nilimjua mama wadogo zangu tyu nilisoma kwa msaada wa Mungu ada ikikosa nakaa nikipata nasoma nimekaa home three years yaan secondary nimeisa 7 years baada 4 year nikirudisha nimefauli matokea nimeenda home kwa mama alikuwa hataki kusikia Babar hizo nimefany kaz zandani zote nazijua kwan kila nilipoishi nilijua kuwa sikustahil kupata upendo wowote ivyo Mimi nilikuwa najitenga Mara kwa Mara maana nikaa nafaliy wananicheka na kunisema so baada ya kula naosha vyomb au napenda shamban au kutfuta kumi au kuchunga mbuz aukuchota maji lakini Mungu amenivusha taratibu Leo Niko chuo kikuu China nasoma lakini namjengea mummy Nyumba namalizia kuezeka nimemsamehe na nimewasemehe wote ila closeness kwao zero ndo ivyoo tunaisongesha safar
 
Kwaiyo nakutia moyo usikate tamaa Mpende Mungu wasaidie wasiojiweza ndo namalizia master's
 
Pole sana unaonekana umelelewa na Mama tu bila Baba !! Uoni aibu kueleza kua unamchana live !!hivi ni Mama au ni mdogo wako !! Ulifikiri ni sifa huna adabu na wewe ndiyo type za kuharibu watoto wenye maadili kwa wazazi wao ! Ulipata malezi machafu toka mwanzo .
 
Pole sana dada!Mtafute babaako mzazi wa kiume hakatai mtoto wake hasa akiwa ameshakua mkubwa!
 
Lady Jay pole sana ujumbe wako umenitoa machozi maana naisi Mimi nawewe hii historia inafanana kuna wakati nasema bola walio yatima wana jua hawana wazazi wana amani Mimi naelewa inatesa sana hii imepelekea kuzaa Na kuwa single mother maana unajikuta unajiingiza katika mahusiano bila kutalajia pole mamy Mungu yupo mapito hayo bado nayapitia Mimi pia sina mapenzi Na mama yangu hata kidogo katika maisha sikuwahi kuipata upendo,furaha, najikuta napenda mama Wa wenzangu najisahau kama sio Wa kwangu Kiukweli sina upendo Na mama wala baba mama Na baba wanachukiana sana nimejikuta nampenda babu yangu bila babu nisingesoma Leo ata la kwanza Mimi nilitupwa kwenye kapu nje Na mwezi mmoja my dear mengine hatuwez kuyasema ndomana naangaika nisake kazi niondoke Mimi ata line nitabadili
mmmh makubwa!
 
Back
Top Bottom