lady Jay
JF-Expert Member
- May 29, 2016
- 529
- 655
Habari zenu wapendwa,
Mimi ni msichana niliyemaliza chuo lakini natafuta kazi. Naishi na wazazi wangu na wadogo zangu wa kike ambao nawapenda sana. Nimekulia na kulelewa na bibi sana na mama mdgo ambao wote walikua wapole na wakarimu ila mama mdogo alitangulia mbele ya haki.
Nilimpenda sana mamdogo kuliko mama yangu mzazi kwasababu alinipenda na kuchukua nafasi ya mzazi wangu na ndiye aliyeniambia mume wake mama siyo baba yangu mzazi ( ila ni baba yao wadogo zangu ) nikiwa darasa la sita.
Niliumia sana kwasababu mama yangu alikuwa hana time kabisa kunieleza hayo. Hapo form one ndo nikaanza kuishi na mama yangu ila jamani ni mkali kwangu adi naliaga. Kuna siku nilimuuliza mama mdgo kama huyu kweli ni mama yangu mzazi au la akasema ndo mamako.
My mum hana ukaribu na mimi, ananifokea kila wakati bila hata sababu. Hanaga shukrani in anything i do. Uzuri darasani nilikua nafanya vzuri sana nikishuka position kidgo atafoka likizo nzima. Nilikua nashika nafasi ya nne nikiwa naongoza wasichana ila nikiwa tu wa tano ataongea likizo nzima.
Anavyokuwa ananiangalia, utafikiri yeye ndo mama yangu wa kambo hata akipiga honi ya gari getini nikiwa tu nje nilikua nakimbilia chooni. Anyway namshukuru kwasababu yeye ndo aliyenisomesha. (japo ni wajibu wake).
Tatizo ni pale mama anavyokuwa hana mother to daughter love au affection. Hajali what I do. Naweza kumuomba hela anakuwa mkali mpaka namwambia basi mama natafuta njia napata na haulizi ila wadogo zangu wanapewa hata extra. Mimi sijawahi kununuliwa simu na mama ila wao wananunuliwa tena mimi ndo namsindikizaga mama kununua na haniulizi mimi napata wapi simu.
Nikitaka tuongee labda angalau nimwambie kitu kinachonisumbua au just kupata faraja ya mama anaongea kwa ukali kwamba kachoka au bwanae ondoka ila roho inaniumaga. Marafiki zangu wanavyoongelea mama zao huwa nawatazama na kuwatamani.
Nyumbani kuna mfanyakazi lakini kazi zote nafanya mimi na mama humtetea dada na kusema mimi sina umuhimu ndani wakati kutwa nzima mimi ndo najishughulisha ila nakaaga kimya hadi nikiwa chuo nikija kusalimia huwa hataki niondoke ili nifanye kazi. Nikimwambia mama nina test atasema bwanae kwani wewe wa kwanza kusoma mpaka nakosa raha nikiwa chuo nakuwaga very lonely na mawazo. Sikufanikiwa kupata mkopo wala hela ya matumizi hvyo nilikua nahudumiwa na mama. Aisee sitokuja kusahau mateso niliyopata chuo.
Nimelala hungry nights mpaka ilibidi nizoee. Hapo ndo nikaona nitakufa nikaanza mahusiano na wanaume kisa nipate hela. Hapo mama uwezo anao wakunisaidia lakini anasema hana hela nitafute wanaume tena kwa ukali.
Anyway nilipunguza ukaribu na mama hata upendo kwasababu nilijaribu kuwa karibu nae nipate mapenzi ya mama lakini nikashindwa. Afu yeye ndo anasema nina roho mbaya, sina upendo kama wadogo zangu. Ninamwangalia tu kwasababu najua yeye ndo hanipendi. Na anasema hivyo kwasababu anawasikiliza sana yuko karibu nao but she pushes me away yaani utafikiri niliokotwa.
Kuna wakati huwa natamani niolewe ila ndoa ina majanga yake pia na sina hata mtu. Na hali ya mama imenifanya nikose upendo kwa watu wengne niponipo tu all alone. Kuna wakati nakaa tu na kulia na kinachoniuma nikiwa 7 yrs nilishawahi kubakwa kijijini kwa bibi na mfanyakazi ila sijawahi kumwambia mama wala mtu yeyote.
Watu watakua wanajiuliza mbona sitaji baba. Baba yangu ana familia yake mkoani na alishasahau kama ana mtoto. Baba yangu wa kambo yupoyupo tu but sana sana anawajali wanae ila hainiumizi roho. Ninachomuomba Mungu niondoke nipate kazi hata mkoani mbali na mama yangu.
NB. Wazazi wa hivi especially wamama jaribu kuweni karibu na watoto wenu kuweni na upendo. Mimi siwezi elezea kila kitu hapa ila umuhimu wa mamangu ni kunisomesha tu tena kwa maneno namshukuru sana kwa hilo.
Wapendwa sjui mtanisaidiaje but nimevumilia sana ni mama yangu huyo ndo maana wengne hukimbia kwao au kutaka ndoa haraka ili waondoke makwao.
Wazazi badilikeni tafadhali.
Mimi ni msichana niliyemaliza chuo lakini natafuta kazi. Naishi na wazazi wangu na wadogo zangu wa kike ambao nawapenda sana. Nimekulia na kulelewa na bibi sana na mama mdgo ambao wote walikua wapole na wakarimu ila mama mdogo alitangulia mbele ya haki.
Nilimpenda sana mamdogo kuliko mama yangu mzazi kwasababu alinipenda na kuchukua nafasi ya mzazi wangu na ndiye aliyeniambia mume wake mama siyo baba yangu mzazi ( ila ni baba yao wadogo zangu ) nikiwa darasa la sita.
Niliumia sana kwasababu mama yangu alikuwa hana time kabisa kunieleza hayo. Hapo form one ndo nikaanza kuishi na mama yangu ila jamani ni mkali kwangu adi naliaga. Kuna siku nilimuuliza mama mdgo kama huyu kweli ni mama yangu mzazi au la akasema ndo mamako.
My mum hana ukaribu na mimi, ananifokea kila wakati bila hata sababu. Hanaga shukrani in anything i do. Uzuri darasani nilikua nafanya vzuri sana nikishuka position kidgo atafoka likizo nzima. Nilikua nashika nafasi ya nne nikiwa naongoza wasichana ila nikiwa tu wa tano ataongea likizo nzima.
Anavyokuwa ananiangalia, utafikiri yeye ndo mama yangu wa kambo hata akipiga honi ya gari getini nikiwa tu nje nilikua nakimbilia chooni. Anyway namshukuru kwasababu yeye ndo aliyenisomesha. (japo ni wajibu wake).
Tatizo ni pale mama anavyokuwa hana mother to daughter love au affection. Hajali what I do. Naweza kumuomba hela anakuwa mkali mpaka namwambia basi mama natafuta njia napata na haulizi ila wadogo zangu wanapewa hata extra. Mimi sijawahi kununuliwa simu na mama ila wao wananunuliwa tena mimi ndo namsindikizaga mama kununua na haniulizi mimi napata wapi simu.
Nikitaka tuongee labda angalau nimwambie kitu kinachonisumbua au just kupata faraja ya mama anaongea kwa ukali kwamba kachoka au bwanae ondoka ila roho inaniumaga. Marafiki zangu wanavyoongelea mama zao huwa nawatazama na kuwatamani.
Nyumbani kuna mfanyakazi lakini kazi zote nafanya mimi na mama humtetea dada na kusema mimi sina umuhimu ndani wakati kutwa nzima mimi ndo najishughulisha ila nakaaga kimya hadi nikiwa chuo nikija kusalimia huwa hataki niondoke ili nifanye kazi. Nikimwambia mama nina test atasema bwanae kwani wewe wa kwanza kusoma mpaka nakosa raha nikiwa chuo nakuwaga very lonely na mawazo. Sikufanikiwa kupata mkopo wala hela ya matumizi hvyo nilikua nahudumiwa na mama. Aisee sitokuja kusahau mateso niliyopata chuo.
Nimelala hungry nights mpaka ilibidi nizoee. Hapo ndo nikaona nitakufa nikaanza mahusiano na wanaume kisa nipate hela. Hapo mama uwezo anao wakunisaidia lakini anasema hana hela nitafute wanaume tena kwa ukali.
Anyway nilipunguza ukaribu na mama hata upendo kwasababu nilijaribu kuwa karibu nae nipate mapenzi ya mama lakini nikashindwa. Afu yeye ndo anasema nina roho mbaya, sina upendo kama wadogo zangu. Ninamwangalia tu kwasababu najua yeye ndo hanipendi. Na anasema hivyo kwasababu anawasikiliza sana yuko karibu nao but she pushes me away yaani utafikiri niliokotwa.
Kuna wakati huwa natamani niolewe ila ndoa ina majanga yake pia na sina hata mtu. Na hali ya mama imenifanya nikose upendo kwa watu wengne niponipo tu all alone. Kuna wakati nakaa tu na kulia na kinachoniuma nikiwa 7 yrs nilishawahi kubakwa kijijini kwa bibi na mfanyakazi ila sijawahi kumwambia mama wala mtu yeyote.
Watu watakua wanajiuliza mbona sitaji baba. Baba yangu ana familia yake mkoani na alishasahau kama ana mtoto. Baba yangu wa kambo yupoyupo tu but sana sana anawajali wanae ila hainiumizi roho. Ninachomuomba Mungu niondoke nipate kazi hata mkoani mbali na mama yangu.
NB. Wazazi wa hivi especially wamama jaribu kuweni karibu na watoto wenu kuweni na upendo. Mimi siwezi elezea kila kitu hapa ila umuhimu wa mamangu ni kunisomesha tu tena kwa maneno namshukuru sana kwa hilo.
Wapendwa sjui mtanisaidiaje but nimevumilia sana ni mama yangu huyo ndo maana wengne hukimbia kwao au kutaka ndoa haraka ili waondoke makwao.
Wazazi badilikeni tafadhali.