JFK wabongo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2015
- 3,887
- 3,201
Ni bora umetambua wajibu wako kwake.Kwanza nataka nikwambie kitu, Leo ukiwa na ukimwi unaweza kuishi maisha marefu sana kuna magonjwa mengine unaambiwa una miezi minne tu unakuta, japo hatuombi mtu apate hata malaria lakini kwa nn basi usichukue taadhali?
Sijawahi kuwa na uadui mkubwa kiasi hicho hata km kesho sitakuwa nae, tumezaa, tumeishi, ni ndugu sasa hivyo bado hata tushindwe kuelewana kwa kiasi gani lakini binafsi hata wanangu watapenda kumuona baba yao anaendelea vizuri namshukuru maisha yake.
Mwanamke anapolalamika ana sababu kubwa tayali ameshaona mbele, japo ss tunaonekana tunachonga sana lakini tuna sababu
Ila kama mtu ameacha msosi ndani kaamua kwenda kula makombo kwa jirani pia ana sababu. Kama hiyo sababu haijatoka, usitegemee kama atakusikiliza.
Kuhusu kupima itafaa uonane na washauri nasaha ili wakupe approach nzuri ambayo haitavunja uhusiano wenu.