RRONDO
Platinum Member
- Jan 3, 2010
- 57,806
- 129,656
Ndugu zangu mimi sio muumini wa haya mambo, sijui majini wanga siamini kama yapo. Ila leo kuna kitu kimenitokea kinaweza kubadili maoni yangu juu ya hivi viumbe.
Kama mjuavyo mwisho wa wiki huu unapilika nyingi za usiku na mimi leo nilikuwa kwenye misele ya usiku. Sasa wakati narudi mida ya saa kumi na robo hivi alfajiri hii nimeona vitu naona si vya kawaida.
Wakati narudi nyumbani niko peke yangu kwenye gari na barabarani ghafla akatokea paka mweupe anakatiza barabara . Kwa kawaida usiku huwa nakimbiza gari kidogo na ninaendesha katikati ya barabara, basi yule paka katokea upande wa kushoto anakatiza kueleke kulia.
Kwa instict za udereva nikanyunyiza breki kidooogo, nikahamia kushoto alipotoka nikamkwepa bila kashkashi. Kuangalia nyuma kwa kutumia vioo sikumuona yule paka! Kwenda mbele kama mita kumi nikamuona mwanamke wa kizungu 'blonde' kavaa gauni jeusi refu limefunika hadi viatu kasimama upande wa kulia wa barabara!
Nikamwangalia na yeye akaniangalia wakati napta macho yalipogongana mwili wote ukanisisimka! Kwa mazingira yale niliomkuta na muda huu si kawaida kukuta mwanamke kasimama peke yake awe wa kizungu au mswahili, ndugu zanguni huyu ni jini? Nimeandika hii habari kabla sijalala mkiona nipo kimya sana mjue ni athari za huyo 'jini'.
cc: mshana jr
Kama mjuavyo mwisho wa wiki huu unapilika nyingi za usiku na mimi leo nilikuwa kwenye misele ya usiku. Sasa wakati narudi mida ya saa kumi na robo hivi alfajiri hii nimeona vitu naona si vya kawaida.
Wakati narudi nyumbani niko peke yangu kwenye gari na barabarani ghafla akatokea paka mweupe anakatiza barabara . Kwa kawaida usiku huwa nakimbiza gari kidogo na ninaendesha katikati ya barabara, basi yule paka katokea upande wa kushoto anakatiza kueleke kulia.
Kwa instict za udereva nikanyunyiza breki kidooogo, nikahamia kushoto alipotoka nikamkwepa bila kashkashi. Kuangalia nyuma kwa kutumia vioo sikumuona yule paka! Kwenda mbele kama mita kumi nikamuona mwanamke wa kizungu 'blonde' kavaa gauni jeusi refu limefunika hadi viatu kasimama upande wa kulia wa barabara!
Nikamwangalia na yeye akaniangalia wakati napta macho yalipogongana mwili wote ukanisisimka! Kwa mazingira yale niliomkuta na muda huu si kawaida kukuta mwanamke kasimama peke yake awe wa kizungu au mswahili, ndugu zanguni huyu ni jini? Nimeandika hii habari kabla sijalala mkiona nipo kimya sana mjue ni athari za huyo 'jini'.
cc: mshana jr
