Jimmie Gatsby
JF-Expert Member
- Mar 7, 2013
- 3,588
- 7,288
Pole sana mkuu; kwa uliyopitia kwanza
Waswahili wanadai yatima hadeki na kweli hadeki. Tuache kuwapa hawa mama mimba na kuwa acha ili kupunguza tatizo hili, natumai hutakuja mkimbia mwanamke utakayempatia mimba maana kama ni shule tiyari umeipitia vizuri
Hatuzungumzii single maza,tunazungumzia mama wa kambo asa kuwapa mimba hao na mada hewani vinahusiana nini
kwani mtoto huwa anabaki na mama au baba?wengi wanalelewa na mama za kambo kwa sababu mama zao ni single mother then mshua kaowa mwanamke mwingine
kwahyo mdau hapo yupo sahihi tu
ww ni mtu mzima alafu unauliza maswali ya kitoto....kwani mtoto huwa anabaki na mama au baba?
Mungu akusamehee bure, umeandika utumbo Tena ulioozaaaa,
Hivi unasikia Visa vingap watoto kuumizwa na mama zao wakambo? Kuchomwa Moto,kuchomwa bisibisi, kunyimwa kula, kupigwa Hadi kupoteza fahamu...are you a foolish?
Hakuna mama mzuri ka mama wa kambo. Jichunguze utakuta kuwa weye ndo ulikuwa mkorofi. Kulialia hovyo. Kujinyea na kujikojolea hivyo hovyo. Mama wa kambo huku akilea mimba zake weye unataka akupakate ka mamako alivyokufanyia.
Acheni kuwatukana bali muwashukuru. Mama wa kambo angekuwazia mabaya weye ungelifikia ulipo leo?? Shilingi ina pande mbili
Mashemeji wa kike nao balaaaKuna wale ambao wanalelewa na ndugu(kaka) sasa kwenye picture anaingia shemeji ndio anaanza tabia za umama wa kambo.
hujajibu swaliww ni mtu mzima alafu unauliza maswali ya kitoto....
Huyo mama wa kambo bado yupo hai kama ndio una mawasiliano nae, au unamsaidia lolote?. Umeshawahi kumuuliza kwanini alikuwa akikupa azabu?Nimekumbuka enzi hizo naishi na mama wa kambo nilipitia shida sana kupigwa bila kosa ilikua kawaida sana kupitisha siku nzima dry bila kula ilikua normally sana
Nakumbuka ilikua nikifaulu napigwa naambiwa nimeigilizia na nikifeli naambiwa sina akili napigwa pia yaani nilikua naishi kisungura sungura sana
Manyanyaso gani ushawai kukutana nayo share experience
Nina dada yangu binamu aliwahi kulelewa na mama wa kambo miaka ya 90 mwanzoni, mama yao alifariki, mimi chozi lilinitoka kwa aliyokuwa akinisimulia. Kubwa aliloniambia ni hatowahi kuja kumsamehe kaka yake kwa mama huyo na hilo pengine ndio linaloweza msababisha asiingie Mbinguni.Zamani hakukua na mitandao ndo maana walikua hawasikiki tena walikua wakatili wa kutisha mnoooo