Nimekiwasha NHIF

NHIF mkoa wa Kagera kuna nini??? Mtu kaomba Cadi mwaka wapili huu hazitoki na hakuna majibu ya kueleweka kuna nini??
 
Duuh, umenikumbusha one day nimeenda ofisi ya mkuu wa mkoa Mara.

Before nilikuwa nikifanya mawasiliano na dada mmoja alienipigia baada ya kukabidhiwa barua yangu, akasema niende ofisin nikajitambulishe, so kwa vile barua nireaddress kwa RAS, moja kwa moja nikaenda ofisi ya Ras.

Aisee kidada kilimaind mbaya mno, alinipeleka secretary wa Ras baada ya kujua skuwa na appointment na Ras, secreatry akawa anakisihi, “mama hawa ni wageni wasikileze tu, hakuna kilichoharibika.”

Kikawa kinakaza kwann sikumpigia simu kumjulisha kuwa nimefika, naenda kwa Ras kufanya nn, Ras anaweza kunisikiliza mimi.

Hadi secretary akaondoka akaniacha na msala,

Hizi ofisi za utumishi wa umma kuna baadhi ya staff hawapaswi kuzihudumia, basi tu ni vile hakuna kujibishana serikalini.
 
Kwakweli bro...huu ndio ukweli Mtupu wanazingua
 
Wale jamaa na hii system yao ya kusema fanyia kazi online ni ya hovyooo sanaa.
 
Watu wa Mapokezi wakuwaga na majibu ya hovyo, nyodo na kujiona sana.
 
Hakuna kazi ngumu kama huduma kwa wateja, Bongo bado sana kwenye hii kazi. Sijui wanategemewa wasifiwe tu kwa huduma!
 
Pole ndugu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…