Nimekataliwa ukweni kisa kabila langu

Nimekataliwa ukweni kisa kabila langu

Zingatia hili. Ukiona unaingia kwenye mahusiano kwakulazimisha, jua mbeleni utaumia kuliko ukikubali ukweli kwasasa.
Kama binti mwenyeweNanaelekea kuwaelewa ndugu, wanawake wapo wengi sana japo mwanzo utaumia ila utazoea. Kubali kuishi bila yeye kisha anza kumove on. Kingine, usiwabembeleze sana maana wanaweza kukupa masharti magumu kukukomoa na ukikubaliwa utakuwa mtumwa wao. Usipige simu kuomba ukubalike wala nn, kaa kimya mwezi mzima. Na wakipiga simu (hata kama ni binti) waambie umewaelewa. Usilazimishe mahusiano hata kama unampenda sana, unless awe amebeba oksijeni unayovuta.
Nimekusoma vyema mkuu wangu, ahsante kwa ushauri wako. Nitazingatia
 
Hi kitu imeniuma sana wakuu, sikutegemea Karne hi bado kuna ubaguzi wa aina hii.

Iko hivi, nimempata binti wa kibena tumependana na tukakubaliana tuoane, kimbembe ni pale alipowapa taarifa nyumbani kwao kuwa kapata mchumba mjita wa Musoma.
Walivyosikia tu Musoma wakaitisha kikao Cha familia na kukataa katakata kuwa binti yao hawezi olewa Musoma. Sababu zao ni
1. Musoma ni mbali na kwao(Njombe). Ikumbukwe mm na binti wore tunaishi Dar es Salaam
2. Watu wa Musoma ni wakatili sana

Wakuu, kusema kweli kutoka moyoni mwangu nampenda sana huyu binti, sijui nitumie njia gani kupindua meza maana kwa Hali ilivyo yeye binafsi ni Kama anaelekea kuwatii ndugu zake(Yuko dilemma)

Naombeni mnishauri, nifanyeje au nitumie njia gani ili kuweza kumuoa huyu binti.

Ahsanteni.
Mjaze upepo mkuu...
 
Unatafuta Vita na wabena naomba nikuambie hao watu sio "warahisi" Kama unavyodhani .
Sijakusoma mkuu, sio warahisi kivipi. Ni vita gani hiyo unayoizungumzia. Fafanua nikuelewe kama hutojali chief
 
Zingatia hili. Ukiona unaingia kwenye mahusiano kwakulazimisha, jua mbeleni utaumia kuliko ukikubali ukweli kwasasa.

Kama binti mwenyewe anaelekea kuwaelewa ndugu, wanawake wapo wengi sana japo mwanzo utaumia ila utazoea. Kubali kuishi bila yeye kisha anza kumove on. Kingine, usiwabembeleze sana maana wanaweza kukupa masharti magumu kukukomoa na ukikubaliwa utakuwa mtumwa wao. Usipige simu kuomba ukubalike wala nn, kaa kimya mwezi mzima. Na wakipiga simu (hata kama ni binti) waambie umewaelewa. Usilazimishe mahusiano hata kama unampenda sana, unless awe amebeba oksijeni unayovuta.

Kijana fata ushauri huu na hasa ukizingatia makabila ya kwenu yanasifa za hovyo fanya uwende tu ukaoe kijijini kwenu au kabila lako
 
Tukushauri halafu baadaye uende kumpiga panga mtoto wa watu.
Ila wajita siyo katili sana kama wakurya eti? Kuna mkurya mmoja alioaga sista angu aisee,kila mara ukienda kwa sista utakuta ana kama kuvimba vimba hiv usoni na vimakovu vya hapa na pale.kwa kuwa wazazi walimkatalia asiolewe huko akawa anawaficha kinachoendelea baadaye akaweka wazi,mbwa alikuwa anamtembezea kipigo hatari
 
Tukushauri halafu baadaye uende kumpiga panga mtoto wa watu.
Ila wajita siyo katili sana kama wakurya eti? Kuna mkurya mmoja alioaga sista angu aisee,kila mara ukienda kwa sista utakuta ana kama kuvimba vimba hiv usoni na vimakovu vya hapa na pale.kwa kuwa wazazi walimkatalia asiolewe huko akawa anawaficha kinachoendelea baadaye akaweka wazi,mbwa alikuwa anamtembezea kipigo hatari
Sio kila mpigaji ni mkurya. Kupiga ni tabia ya mtu.
 
Hi kitu imeniuma sana wakuu, sikutegemea Karne hi bado kuna ubaguzi wa aina hii.

Iko hivi, nimempata binti wa kibena tumependana na tukakubaliana tuoane, kimbembe ni pale alipowapa taarifa nyumbani kwao kuwa kapata mchumba mjita wa Musoma.
Walivyosikia tu Musoma wakaitisha kikao Cha familia na kukataa katakata kuwa binti yao hawezi olewa Musoma. Sababu zao ni
1. Musoma ni mbali na kwao(Njombe). Ikumbukwe mm na binti wore tunaishi Dar es Salaam
2. Watu wa Musoma ni wakatili sana

Wakuu, kusema kweli kutoka moyoni mwangu nampenda sana huyu binti, sijui nitumie njia gani kupindua meza maana kwa Hali ilivyo yeye binafsi ni Kama anaelekea kuwatii ndugu zake(Yuko dilemma)

Naombeni mnishauri, nifanyeje au nitumie njia gani ili kuweza kumuoa huyu binti.

Ahsanteni.
Mbaya zaidi ni Kabila tu ambalo huwezi badili kamwe....

Dini na Jina waweza badili Kisheria ila Kabila utazaliwa nalo na kufa nalo...

Anyway, ishakula kwako Afsa kwani yaonekana Mkoa wa Mara wengi wanaona jamii ya huko haifai !!
 
Vipigo,ukatili dhidi ya wanawake Hauna kabila,
Hivi mmesahau ya Ufo Saro,Yule mtangazaji wa ITV,ambaye mume wake(mchaga)alivyowashambulia yeye na mama yake kwa risasi akitaka kuua,na yeye kujiua kwa risasi?
Je Yule muhaya Tena aliyewahi kuwa padre,alivyoua mke wake kwa shoka la kichwa,
Mi nakushauri kaa na huyo mbena wako,mpe maneno,tafuta mtu mzima mmoja,wa kutoka huko ubenani,akaongee na wazee,hili jambo dogo sana.
Ubaguzi kwenye jamii upo sana,
Kuwa muhaya haimaniishi ndio utaweza kuoa binti wa kihaya kutoka familia yoyote,wahaya wanaweza kupinga,Kama wewe unaetaka kuoa ni choka mbaya,sio tajiri,yaani wewe uzaliwe buguruni,usome kayumba,harafu utake binti aliyezaliwa,masaki,wahaya hapa watakupa jamba jamba,hata Kama ni muhaya mwenzao,
 
Zingatia hili. Ukiona unaingia kwenye mahusiano kwakulazimisha, jua mbeleni utaumia kuliko ukikubali ukweli kwasasa.

Kama binti mwenyewe anaelekea kuwaelewa ndugu, wanawake wapo wengi sana japo mwanzo utaumia ila utazoea. Kubali kuishi bila yeye kisha anza kumove on. Kingine, usiwabembeleze sana maana wanaweza kukupa masharti magumu kukukomoa na ukikubaliwa utakuwa mtumwa wao. Usipige simu kuomba ukubalike wala nn, kaa kimya mwezi mzima. Na wakipiga simu (hata kama ni binti) waambie umewaelewa. Usilazimishe mahusiano hata kama unampenda sana, unless awe amebeba oksijeni unayovuta.
Para ya mwisho [emoji3]
 
Back
Top Bottom