Nimekata shauri, naandika wosia

Nimekata shauri, naandika wosia

Ishu sio kutishwa na mauti bali ni kuiachia familia yako mazingira bora . Mara nyingi mashemeji ,wazee hukimbilia kupora kila kitu pale ndugu yao anapofariki bila kujali haki za watoto na mke wa marehemu. Rejea kisa cha mke wa marehemu deo filikunjombe ambae pamoja na umaarufu wake anapambana mahakamani kupata haki ya mali alizoacha mumewe.
Mjane unamsaidia vipi wakati capital yake (mbunye)unamuacha nayo?
Sisi tunaoamini katika uzima wa milele hatutishwi tishwi na mauti maana tujapokufa tutaishi na kama hivyo vijimali si kitu, hakika twauendea mji ambao mali zake haziliwi na kutu wa nondo TAMANI FAMILIA YAKO WAWE SEHEMU YA MALI HIZO.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mjane unamsaidia vipi wakati capital yake (mbunye)unamuacha nayo?
Sisi tunaoamini katika uzima wa milele hatutishwi tishwi na mauti maana tujapokufa tutaishi na kama hivyo vijimali si kitu, hakika twauendea mji ambao mali zake haziliwi na kutu wa nondo TAMANI FAMILIA YAKO WAWE SEHEMU YA MALI HIZO.
Inaonekana we mbinafsi Sana, halafu katika katika vitu vinakuumiza kichwa ni Hilo la mke kubaki anatanua

Hapo unazungumzia mke tu, ambaye OK yeye atategemea mbunye kama unavo Sema , vipi kuhusu watoto uluowatengeneza?, ambao kimantiki ni jukumu lako kuwapa security na Amani kama una nafasi hiyo, mana wamekuja hapa Duniani kwa hisani yako!

Mimi ninayo fahamu ni kuwa ukizaliwa mwanaume unapata mengi mazuri na upendeleo mwingi wa kidunia. ila nimeprove bila wasi wasi kuwa hatudumu kimaisha, yaan tunakufa mapema Sana
Kwa hiyo mkuu wakati unasherekea uanaume wako fahamu pia wenzetu wamepewa maisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
OK unaweza kuwa na template ya wosia from Rita?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haha template Sina ila ni maneno Machache Sana wala usicomplicate,

MI kwa mfano ni mjasiliamali mambo ya kusema nyumba hii a sijui achukue Nani hiki achukue Nani niliona itakuwa ngumu , sababu ni naweza amua kuuza baadhi ya asset katika Kuongeza mtaji wangu nikiwa bado hai
So ilikuwa kama hivi " chochote kitakacho kuwa Mali yangu, ikiwemo akaunti za benki na fedha taslim, ikithibitishwa nimefariki , apewe mke wangu na watoto wake"

Halafu ni kaweka phrases kadhaa za kupiga lock kwa viben ten and the likes kujimilikisha nilichotafuta, "Mke ataruhusiwa kuwa na mahusiano mapya baada ya kifo changu, ila kwa mashati kuwa asizae na wala kuleta mume Mpya katika maeneo wanayoishi, ikithibitika kuwa amekiuka hayo usimamizi wake utakoma mara Moja na badala yake upekelekwe kwa watoto wenyewe "


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haha template Sina ila ni maneno Machache Sana wala usicomplicate,

MI kwa mfano ni mjasiliamali mambo ya kusema nyumba hii a sijui achukue Nani hiki achukue Nani niliona itakuwa ngumu , sababu ni naweza amua kuuza baadhi ya asset katika Kuongeza mtaji wangu nikiwa bado hai
So ilikuwa kama hivi " chochote kitakacho kuwa Mali yangu, ikiwemo akaunti za benki na fedha taslim, ikithibitishwa nimefariki , apewe mke wangu na watoto wake"

Halafu ni kaweka phrases kadhaa za kupiga lock kwa viben ten and the likes kujimilikisha nilichotafuta, "Mke ataruhusiwa kuwa na mahusiano mapya baada ya kifo changu, ila kwa mashati kuwa asizae na wala kuleta mume Mpya katika maeneo wanayoishi, ikithibitika kuwa amekiuka hayo usimamizi wake utakoma mara Moja na badala yake upekelekwe kwa watoto wenyewe "


Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa una wivu mpaka Akhera!?, Swali: wengi humu naamini mnaabudu ktk Dini, kwani hamna muongozo wa kidini mali igawanywe vipi baada ya Mungu kumpenda zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haha template Sina ila ni maneno Machache Sana wala usicomplicate,

MI kwa mfano ni mjasiliamali mambo ya kusema nyumba hii a sijui achukue Nani hiki achukue Nani niliona itakuwa ngumu , sababu ni naweza amua kuuza baadhi ya asset katika Kuongeza mtaji wangu nikiwa bado hai
So ilikuwa kama hivi " chochote kitakacho kuwa Mali yangu, ikiwemo akaunti za benki na fedha taslim, ikithibitishwa nimefariki , apewe mke wangu na watoto wake"

Halafu ni kaweka phrases kadhaa za kupiga lock kwa viben ten and the likes kujimilikisha nilichotafuta, "Mke ataruhusiwa kuwa na mahusiano mapya baada ya kifo changu, ila kwa mashati kuwa asizae na wala kuleta mume Mpya katika maeneo wanayoishi, ikithibitika kuwa amekiuka hayo usimamizi wake utakoma mara Moja na badala yake upekelekwe kwa watoto wenyewe "


Sent using Jamii Forums mobile app
Wazazi vipi mkuu,hukuwaweka?si nasikia nao wanakuwa na fungu lao?
 
Wazazi vipi mkuu,hukuwaweka?si nasikia nao wanakuwa na fungu lao?
Bahati mbaya nilipoteza wazazi, na hata kama wangekuwa hai pengine nisingewapa kipaumbele Sana
Kimsingi tunawajibika Sana kwenye hizi Familia tulizoanzisha yaan mke na watoto,

Dhana nzima ya wosia Ina apply Sana katika familia zetu hizi zilizofunikwa na umasikini, Niwshuhudia sehemu pikipiki tu ya marehemu ilisababisha Wanafamilia kukatana mapanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana we mbinafsi Sana, halafu katika katika vitu vinakuumiza kichwa ni Hilo la mke kubaki anatanua

Hapo unazungumzia mke tu, ambaye OK yeye atategemea mbunye kama unavo Sema , vipi kuhusu watoto uluowatengeneza?, ambao kimantiki ni jukumu lako kuwapa security na Amani kama una nafasi hiyo, mana wamekuja hapa Duniani kwa hisani yako!

Mimi ninayo fahamu ni kuwa ukizaliwa mwanaume unapata mengi mazuri na upendeleo mwingi wa kidunia. ila nimeprove bila wasi wasi kuwa hatudumu kimaisha, yaan tunakufa mapema Sana
Kwa hiyo mkuu wakati unasherekea uanaume wako fahamu pia wenzetu wamepewa maisha

Sent using Jamii Forums mobile app
Ili uonekane angalau reasoning yako ina mantiki jaribu kutanua wigo wa majukumu i.e aliyekuleta wewe duniani hajui majukumu aliyokupa ya kulea wana wa viuno vyako?

Sipendi kuona bin adamu akifikiri chini ya kiwango tena hadharani.

Miaka dahari iliyopita hakukuwa na watoto wa mitaani mpaka pale mlipoanza kuwatenga watoto na jamii yao mizoga nyie (mmedhamiria kufa) mkidhani mnawasaidia saaana wanenu.

Wanangu wanajua kuwa kuishi kwao kunategemea uhai na mazingira yao kwa maana watakula ili waishi.

Kuhusu watoto tambua kuwa :-

MLANGO MMOJA UKIFUNGWA, MINGINE MINGI YAFUNGULIWA KWAO.
 
Bahati mbaya nilipoteza wazazi, na hata kama wangekuwa hai pengine nisingewapa kipaumbele Sana
Kimsingi tunawajibika Sana kwenye hizi Familia tulizoanzisha yaan mke na watoto,

Dhana nzima ya wosia Ina apply Sana katika familia zetu hizi zilizofunikwa na umasikini, Niwshuhudia sehemu pikipiki tu ya marehemu ilisababisha Wanafamilia kukatana mapanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna binti ndugu yangu nimetoka kumfaitia mirathi juzi kati. Ni mambo ya kusikitisha kabisa, watu mpaka wamerogana kwa ajili ya ugomvi wa usimamizi tu wa mirathi. Eti mpaka wajomba wa marehemu wanataka mgawo. Tulipofanikiwa kuwapangua,tukakuta hakimu alishaahidiwa 3m na baba mzazi akisimama upande wake.

Nilishangazwa sana
 
Jamaa una wivu mpaka Akhera!?, Swali: wengi humu naamini mnaabudu ktk Dini, kwani hamna muongozo wa kidini mali igawanywe vipi baada ya Mungu kumpenda zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haa mkuu Sina wivu, ila mjini kuna masomo mengi Sana,
katika watu wanaharibu mchakato mzima wa mirathi ni mwanaume anayekujua kuishi na mkeo baada ya ww kufariki, anaweza akamzalisha mkeo na akatake advantage ya wosia wako kwamba Mali ni za mke na watoto, nahatimaye wanao wakataabika, ndo maana ya kuweka Ile pini

Dini Ina bandwidth kwenye hili la mirathi, ili lifanikiwe swala hili, inabidi wote muwe mmeishika na kunielewa hiyo Dini la sivyo atatokea mtu hana mpango na kanisa wala msikiti na atasumbua tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna binti ndugu yangu nimetoka kumfaitia mirathi juzi kati. Ni mambo ya kusikitisha kabisa, watu mpaka wamerogana kwa ajili ya ugomvi wa usimamizi tu wa mirathi. Eti mpaka wajomba wa marehemu wanataka mgawo. Tulipofanikiwa kuwapangua,tukakuta hakimu alishaahidiwa 3m na baba mzazi akisimama upande wake.

Nilishangazwa sana
Yap! ndo maana halisi ya wosia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna binti ndugu yangu nimetoka kumfaitia mirathi juzi kati. Ni mambo ya kusikitisha kabisa, watu mpaka wamerogana kwa ajili ya ugomvi wa usimamizi tu wa mirathi. Eti mpaka wajomba wa marehemu wanataka mgawo. Tulipofanikiwa kuwapangua,tukakuta hakimu alishaahidiwa 3m na baba mzazi akisimama upande wake.

Nilishangazwa sana
Atapata hizo ulizom fight-ia zikiisha uendelee kumsuport (kutoka kwenye fungu la wanao)
 
Ili uonekane angalau reasoning yako ina mantiki jaribu kutanua wigo wa majukumu i.e aliyekuleta wewe duniani hajui majukumu aliyokupa ya kulea wana wa viuno vyako?

Sipendi kuona bin adamu akifikiri chini ya kiwango tena hadharani.

Miaka dahari iliyopita hakukuwa na watoto wa mitaani mpaka pale mlipoanza kuwatenga watoto na jamii yao mizoga nyie (mmedhamiria kufa) mkidhani mnawasaidia saaana wanenu.

Wanangu wanajua kuwa kuishi kwao kunategemea uhai na mazingira yao kwa maana watakula ili waishi.

Kuhusu watoto tambua kuwa :-

MLANGO MMOJA UKIFUNGWA, MINGINE MINGI YAFUNGULIWA KWAO.
Mkuu kuna jambo unakwepa kuliweka wazi.
Umekuwa unasema watoto watakosa wa kuwalea,kivipi?unamaanisha ndugu warithi hizo mali badala ya watoto ili wawe na moyo wa kulea watoto wa marehemu? Kama ni hivyo basi hao watakuwa ndugu wa ajabu sana.

Nadhani ndugu wasio na tamaa watafurahi ukiacha mirathi kwa sababu utakuwa umewarahisishia michakato.

Hivi mali za familia si ni kwa ajili yako,mkeo na watoto,sambamba na kusaidia wazazi?Kama ndivyo,kivipi iwe nongwa unapokuwa umewazingatia mke,watoto na wazazi katika mirathi?Kuna zaidi ya hao?

Nadhani kuwawekea watoto urithi wa kudumu ni kuwajengea mahusiano mazuri na nduguzo wa damu,familia pande zote,uwasaidie kadri ya uwezo wake na uwe karibu nao kipindi cha uhai. Mioyo itawasuta kuona wanao wakitekea na watajitoa kwa ajili ya wanao.

Kama uliishi na nduguzo vuzuri,sidhani kama mdogo wako asuse kumlea mwanao kwa sababu hukumpa chochote kwenye mirathi. Huyo anakuwa na roho ya kinyama.

Mimi mke wangu huwa nampa somo kwamba acha tujitoe kuwasomesha shemeji zako ili siku nikifa watakutunzia wanao na hawatakuwa na roho ya tamaa ya kukupokonya mali kwa sababu wewe ni sehemu ya mafanikio yao.

Sasa sidhani kama kuna wengine zaidi ya mke,watoto na wazazi kwa kumzingatia uwezo wao. Undugu unaunganishwa na mahusiano ya sasa na sio mgao wa mali za marehemu.

Fafanua hoja yako,unashauri tuache mali zizagae kwa sababu ndugu watachukia kuona umewagawia familia mali? Au unadhani utakuwa umewanyanganya ndugu mamlaka ya kugawa? Kama ni hivyo,nani mwenye mamlaka na mali zaidi yangu na mke
 
Haa mkuu Sina wivu, ila mjini kuna masomo mengi Sana,
katika watu wanaharibu mchakato mzima wa mirathi ni mwanaume anayekujua kuishi na mkeo baada ya ww kufariki, anaweza akamzalisha mkeo na akatake advantage ya wosia wako kwamba Mali ni za mke na watoto, nahatimaye wanao wakataabika, ndo maana ya kuweka Ile pini

Dini Ina bandwidth kwenye hili la mirathi, ili lifanikiwe swala hili, inabidi wote muwe mmeishika na kunielewa hiyo Dini la sivyo atatokea mtu hana mpango na kanisa wala msikiti na atasumbua tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mimi nimekupata vizuri sana,na umeniongezea kitu.
 
Duu hata nimeshindwa kuelewa kwamba kuna mtu atakuja kuwakomoa wanangu kwa kuwa nilikuwa na nyodo au ukwasi?

Unaishi maisha gani mkuu. Ya chuki, vinyongo au visasi? maana point unazotoa sio relevant kabisa kwa matukio ya Dunia ya Leo.

Tambua kuwa' vijimali' unavosemea ni kwa vile wewe una ukwasi, lkn kuna mtu atakuwa yupo tayari kufanya unyama kwa vitu vya Thamani ndogo sana


Sent using Jamii Forums mobile app
Yesu kristo hakueleweka na wengi kwa kuwa hakuyatamka wayatarajiayo.

Jifunze kuelewa kwa kusababu vya kutosha kupitia swali hili

Kwa nini siku hizi kuna watoto wengi wa mitaani?

Watu wazima mmekaa kudhani vijimali vyenu vitawalea wanenu mkishakufa! Mnajitutumua na kunyanyua mabega kwa dharau mbele ya familia!

Ukidanja hakuna mtu wa kukupelekea mwanao mlimani city kula ice cream! Sasa ikibidi akakae kwa bamdogo wanakochunga daily lazima aone ananyanyasika kwa mtazamo wako.
 
Back
Top Bottom