Nimejifunza kuheshimu wanawake

Nimejifunza kuheshimu wanawake

Nilikuwa nawadharau sana wanawake niliwaona kama viumbe dhaifu wasio na akili na hii ilitokana na mazingira niliyokulia ambapo mwanamke anadharaulika na kubezwa.
Wiki iliyopita nilimpeleka mke wa kujifungua kwenye hospitali ya private ambapo hospitali hiyo ina utaratibu wa kumzalisha mwanamke mmewe wake akiwa pembeni anaangalia aisee kuzaa ni shughuli asikwambie mtu nilitoka labour nduki mpaka sasa nikifikria kitendo kile nimeanza kuwaheshimu wanawake kama hospitali zote zingelikuwa na utaratibu ule hakika wanaume tungewaheshimu wake zetu, mama zetu na wanawake wote kwa ujumla acha mama aitwe mama.

Kaka utaratibu upo ila wanaume wengi ni waoga wengine had wanazimia, ushaur wa bure dada zetu mkibeba mimba waambien jamaa waume zenu muiingie nao labor wauone mzik mnaopitia hak ya nan atakueshim
 
Heshima kwa mama miezi mitisa tumboni kwako pole sana mama.
 
Mungu alisema Mwanamke atazaa kwa uchungu na Mwanaume atakula kwa jasho, hivyo hiyo ni nature Mungu aliyoiweka. Lazima iwe hivyo.



ila sahivi wanaume mnata wanawake watafute mle na bado wazae ila mungu atawalipa
 
Sasa Kama Mungu ulisema ndo mlete dharau eti kwa kuwa ni wajibu? Na mbona wanaume siku hizi mnataka kusaidiwa majukumu mkidai maisha siku hizi ni magumu?

Mungu alisema Mwanamke atazaa kwa uchungu na Mwanaume atakula kwa jasho, hivyo hiyo ni nature Mungu aliyoiweka. Lazima iwe hivyo.
 
Umejifunza kuheshimu wanawake baada ya kushuhudia wako akizaa au ulimuhurumia sababu ule uchungu? Wanawake nadhani unawasikia. Tupa mbali kabisa
 
Dini zote zinafundisha mwanaume ampende mkewe na Mwanamke amshimu napata shida kumuelewa mleta mafa
 
Nilikuwa nawadharau sana wanawake niliwaona kama viumbe dhaifu wasio na akili na hii ilitokana na mazingira niliyokulia ambapo mwanamke anadharaulika na kubezwa.
Wiki iliyopita nilimpeleka mke wa kujifungua kwenye hospitali ya private ambapo hospitali hiyo ina utaratibu wa kumzalisha mwanamke mmewe wake akiwa pembeni anaangalia aisee kuzaa ni shughuli asikwambie mtu nilitoka labour nduki mpaka sasa nikifikria kitendo kile nimeanza kuwaheshimu wanawake kama hospitali zote zingelikuwa na utaratibu ule hakika wanaume tungewaheshimu wake zetu, mama zetu na wanawake wote kwa ujumla acha mama aitwe mama.
KWELI KUNA MME NA WA KIUME, HUO MUDA WA KUJIFUNZA HILO UNAUTOA WAPI? Mi nadhani mfumo dume umenikomboa kama sio kuniathiri.
 
Molembe kwahyo heshima inakuja baada ya kuona akijifungua tu baas?

Nafkri huo ndio mwanzo wa kuona mengi na huo ndio mwanzo wa kujifunza mengi juu ya wanawake.

Je, siku ukija kuambiwa huyo mtoto uliyemwona akijifungua kwa taabu sio damu yako itakuwapo heshima tena?

Umeshaoa unatakiwa ufungue moyo kwelikweli, usiseme neno huu ni mwanzo tu. Kiumbe anayeitwa mwanamke acha kabisa kuna mengi sana utakutana nayo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom