Nimeipenda CCM Bure yaani Kama Kambale Vile

Nimeipenda CCM Bure yaani Kama Kambale Vile

Siku za hivi karibuni nimekuwa na furaha tu.... yaani kila nikiangalia hekaheka za CCM. Nilichokipenda zaidi ni ile hali ya familia moja kwa na wasemaji kibao yaani wote wana ndevu kuanzia Baba hadi watoto.

Kila mtu ana la kusema kwenye vyombo vya habari, kila mtu ana uwezo wa kuchagua mgombea, kla mtu ana uwezo wa kumhukumu mwenzie, mara huyu ni mzigo, mara huyu ni kiroba mara huyu ametumwa....bassssi raha tupu.

Honegereni CCM. mlijisahau kidogo mkaelekeza nguvu zenu kwenye mgogoro usiowahusu!

Hiyo ndiyo tofauti kati CCM na CHADEMA, makonda angekuwa CHADEMA angetimuliwa. CCM full Demokrasia.
 
Na bado hakijanuka vizuri. Hii ni rasharasha tu, 2015 ndio mtashuhudia masika halisi ndani ya CCM. Kutakuwa na mafuriko ambayo yatakisomba chama chote na hakitajulikana kimeishia wapi.
 
Waite !waite! Waite! Mjomba chutamaa.

'jei kei ni dhaifu na c.c.yem ni uozo.

Hakuna mwenyekiti pale, aliyepo ni zuzu tu!

Ndani CCM hakuna dictatorship, freedom of expression. Hongereni sana CCM, kila mwenye lake na litoke lakini mwisho wa siku one effort
 
Na bado hakijanuka vizuri. Hii ni rasharasha tu, 2015 ndio mtashuhudia masika halisi ndani ya CCM. Kutakuwa na mafuriko ambayo yatakisomba chama chote na hakitajulikana kimeishia wapi.

Hiyo ni demokrasia ndani ya CHAMA , siyo kama CHADEMA.
 
Kinachonifurahisha nikutumia tingatinga liloisha OIL no LUBRICANT HOW IT CAN WORK WITHOUT??ALTHOUGH THEY ARE NO HYDRAULIC ,THE horse pipe are broken how can work IT??CCM kwishinei

Kama CCM kwshnei, uoga wa nini? tumieni hiyo nafasi, otherwise mtajikojolea pale mtakapowaona wamerudi pamoja , CCM wana demokrasia bwna ,pale hakuna mtu kubanwa kama alivyofanyiwa ZITTO kule Uchaggani.
 
Wazee wa zamani walisema hivi...."Ndugu wakigombana chukua jembe ukalime wakipatana chukua kapu ukavune"So sasa ni wakati wa wapinzani kulima wakija patana waaende wakavune.!!!!!!!!!:dance:

safi sana , SIJUI KAMA cdm mmeipata hii. CCM siyo CHADEMA , akiguswa mtu na kuambiwa ukweli anatimuliwa.
 
CCM haina mwenyewe ,Mwenyekiti wao wa chama kazidiwa nguvu na Mamvi.

Siku zote chama makini hakina mwenyewe, bali kina wenyewe. CCM siyo CHADEMA ya MTEI chini ya mwamvuli wa MBOWE.
 
Mpwa nyumba nzima kila mtu ana ndevu?
Najua hii inawauma sana CHADEMA. mlitaka kuwepo na udikteta kama ule wa MBOWE na SLAA wa kupiga watu kwenye vikao kisa eti wanamuunga mkono ZITTO.
 
thatha maana yake ni kuwa Ugomvi wa Zitto na CDM mngewaachie wenyewe,muende mkalime wakija patana mrudi mkavune.Sasa tatizo la wanaccm mmeingilia ugomvi wao wakija patana sarakasi kwenu.Ni sawa na ugomvi wa NDOA.
 
mbona chadema mpaka akina yericko wanakisemea chama? mbona akina mida8 wanatukana viingozi wakubwa wa chama wanavumiliwa? slaa anaropoka hovyo vitu ambavyo si msimamo wa chama kama kupika gongo?
Nyani haoni kundule mkuu, CHADEMA hata mwenye uwezo tu wa kumlisha ZITTO sumu naye anakuwa na sauti ndani ya CHAMA. kichekesho kweli
 
Jifurahisheni tu hamjui chochote kuhusu siasa za CCM wanatifuana sasa hivi ikikaribia uchaguzi CCM one team na ushindi kama kawa kikwete kidume cha mbegu dhaifu mbowe anaezidiwa akili na mtt mdg ZZK
 
thatha maana yake ni kuwa Ugomvi wa Zitto na CDM mngewaachie wenyewe,muende mkalime wakija patana mrudi mkavune.Sasa tatizo la wanaccm mmeingilia ugomvi wao wakija patana sarakasi kwenu.Ni sawa na ugomvi wa NDOA.

Unaota ndoto ya MCHANA. LISSU,BEN SAA NANE wasikusikie na maneno mbofu mbofu kama hayo.
 
Jifurahisheni tu hamjui chochote kuhusu siasa za CCM wanatifuana sasa hivi ikikaribia uchaguzi CCM one team na ushindi kama kawa kikwete kidume cha mbegu dhaifu mbowe anaezidiwa akili na mtt mdg ZZK

kama kweli wanaume hawa CHADEMA na wawe kitu kimoja na ZITTO kabla ya uchaguzi wa 2015. ZITTO na kundi lake hivi sasa wako makini sana wanasubiri 2015 walipue bomu ambalo litakwenda kuanguka HAI na KARATU na hapo itakuwa mwisho wa uhafidhina wa CDM.
 
Hawana mwelekeo hawa,

laana ya baba wa taifa yawatafuna hawa.
 
Mjomba Elli ulijificha wapi ukawachungulia hao jamaa? Siku zao zimekwisha kabisa. Hakuna aliyetegemea kuwa wangejifia hivyo bila hata kurusha teke. Ndo maana wameamua kila mtu kuchukua anachokiona mbele yake.
Walizoea kwenda kujichotea tu kwenye vyombo vya fedha kama za kwao, walizoea kutamalaki viwanja na mashamba mpaka vijijini. Watanzania M4C OPD imewaamsha. Sasa lile li chama likuubwa liko hoi; hata ya kununulia chumvi hakuna. Kila mwenye mwanya kaiba kaenda kuficha ili atoke nazo 2015.
Mzee EL anawasumbua na zile za Richmond, yaani wamechanganyikiwa hadi baasi. Wamesahau hata vikao vya kujisemea kwani hata vikao vyao m/kiti wao kavidharau. Hakuna faida yeyote ya matamko yao ya vikaoni. Tangu kuvuana magamba mpaka mizigo na sasa EL.
Saa ya ukombozi ni sasa. OPD juu zaidi, washa moto uwachome hadi hayo magamba yawachunuke kama kwato za mbuzi.
 
Hivi huyu thatha hayupo internet cafe kweli? Maana anajibu kila comment haraka haraka anaogopa muda wake usi ishe halafu haja kitetea chama.
 
kama kweli wanaume hawa CHADEMA na wawe kitu kimoja na ZITTO kabla ya uchaguzi wa 2015. ZITTO na kundi lake hivi sasa wako makini sana wanasubiri 2015 walipue bomu ambalo litakwenda kuanguka HAI na KARATU na hapo itakuwa mwisho wa uhafidhina wa CDM.

Du ulivyoivamia hii thread..........., kila post umeijibu.
haya basi jibu na hii.

View attachment 136166
 
Back
Top Bottom