HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Nikiwa ni mwingi wa mawazo na kukumbuka miaka 3 nyuma nilivyotendwa na mdada ambaye sintamsahau maishani mwangu,
Naingia ofcn kwa kishindo nikiwa na uchovu wa kimwili na akili. Walinzi ambao pia ni waosha gari langu wananidaka kwa maneno mengi ya furaha na utani na kunipa misifa nisiyostahili kwa ajili ya visenti vichache ninavyowapa kila mara! Sikutamani kuwaangalia mara mbili kwa ule uchovu, na pia nilielewa fika kuwa misifa yote hiyo ni kutaka kuniomba vijisenti vya kunywea chai!
Nikiwa nimepoteza mtazamo; Najaribu kupandisha ngazi bila uangalifu kuingia ofcn kwangu, ghafla nagongana na binti aliyebeba makabrasha huku akiongea na simu. Anayumba sana, na alipojaribu kapata balance kwa kupapasa sehemu ya kujishikiza kwenye ngazi, anajikuta akinipa kibao kikali shavuni! Samahani pole sana! Sauti ilimtoka. Binafsi kwa jinsi alivyo mrembo na ulaini wa mikono yake, sikusikia hata tone la maumivu! Cha kushangaza nilitamani hata aniongeze kofi lingine!
HP jamani hukuniona? Aliuliza lakini ghafla nikajikuta nimemjibu Mawazo dada, nahisi nimekuwa mwehu!, heee kwa nini unasema hivyo? Aliuliza si mwehu tu, nafikiri unaweza kuniita kichaa au mwendawazimu, hata ukiniita taahira nitaridhika. Ebbo? Alingaka kwa mshangao! Uzuri wako ndiyo ulionifanya niwe hivi Niliropoka
HP sikutarajia alisema. Unaonekana mpole na mstaarabu, kwa nini umeanza haya mambo? Sina utani na sijawahi kufanya utani na nafsi yangu, ni kweli tupu ninayokwambia, sijiwezi kwako niamini, moyo wangu umezizima niliropoka. Aliniangalia, hakujibu.
Wakati najibizana naye, ki-ukweli sikujielewa maneno yote niliyoyasema niliyapata wapi, kutendwa miaka 3 iliyopita ilinifanya niwachukie wanawake kupita kiasi, na sikuwahi kufikiria kama ningeweza kutumbukia kwenye haya mambo kirahisi namna hii.
Aliinama kwa haraka na kuokota karatasi zake na kuanza kushuka ngazi kwa kasi. Ghalfa nilijikuta nikianza kuongea Ohh please, naomba . Kabla sijamaliza, aligeuka na kuniangalia kwa upole, unataka nini zaidi? aliuliza, akanikonyeza
Sifa zake za utulivu na tabia njema zilizagaa kwenye shirika letu hili lisilo la kiserikali. Nilishawahi kusikia vijana wenzangu mara kadhaa wakimsimulia binti huyu kwa jinsi alivyo na misimamo thabiti ya kimaisha na kuonyesha tabia njema. Ingawa
****** Itaendelea kesho, ngoja nimalizie kazi za ofisi ***** :A S embarassed:
Naingia ofcn kwa kishindo nikiwa na uchovu wa kimwili na akili. Walinzi ambao pia ni waosha gari langu wananidaka kwa maneno mengi ya furaha na utani na kunipa misifa nisiyostahili kwa ajili ya visenti vichache ninavyowapa kila mara! Sikutamani kuwaangalia mara mbili kwa ule uchovu, na pia nilielewa fika kuwa misifa yote hiyo ni kutaka kuniomba vijisenti vya kunywea chai!
Nikiwa nimepoteza mtazamo; Najaribu kupandisha ngazi bila uangalifu kuingia ofcn kwangu, ghafla nagongana na binti aliyebeba makabrasha huku akiongea na simu. Anayumba sana, na alipojaribu kapata balance kwa kupapasa sehemu ya kujishikiza kwenye ngazi, anajikuta akinipa kibao kikali shavuni! Samahani pole sana! Sauti ilimtoka. Binafsi kwa jinsi alivyo mrembo na ulaini wa mikono yake, sikusikia hata tone la maumivu! Cha kushangaza nilitamani hata aniongeze kofi lingine!
HP jamani hukuniona? Aliuliza lakini ghafla nikajikuta nimemjibu Mawazo dada, nahisi nimekuwa mwehu!, heee kwa nini unasema hivyo? Aliuliza si mwehu tu, nafikiri unaweza kuniita kichaa au mwendawazimu, hata ukiniita taahira nitaridhika. Ebbo? Alingaka kwa mshangao! Uzuri wako ndiyo ulionifanya niwe hivi Niliropoka
HP sikutarajia alisema. Unaonekana mpole na mstaarabu, kwa nini umeanza haya mambo? Sina utani na sijawahi kufanya utani na nafsi yangu, ni kweli tupu ninayokwambia, sijiwezi kwako niamini, moyo wangu umezizima niliropoka. Aliniangalia, hakujibu.
Wakati najibizana naye, ki-ukweli sikujielewa maneno yote niliyoyasema niliyapata wapi, kutendwa miaka 3 iliyopita ilinifanya niwachukie wanawake kupita kiasi, na sikuwahi kufikiria kama ningeweza kutumbukia kwenye haya mambo kirahisi namna hii.
Aliinama kwa haraka na kuokota karatasi zake na kuanza kushuka ngazi kwa kasi. Ghalfa nilijikuta nikianza kuongea Ohh please, naomba . Kabla sijamaliza, aligeuka na kuniangalia kwa upole, unataka nini zaidi? aliuliza, akanikonyeza
Sifa zake za utulivu na tabia njema zilizagaa kwenye shirika letu hili lisilo la kiserikali. Nilishawahi kusikia vijana wenzangu mara kadhaa wakimsimulia binti huyu kwa jinsi alivyo na misimamo thabiti ya kimaisha na kuonyesha tabia njema. Ingawa
****** Itaendelea kesho, ngoja nimalizie kazi za ofisi ***** :A S embarassed: