Nimefurahia kwa suala zito la wafanyabiashara wa maduka ya kubadilishia fedha mkoa wa Arusha kuhojiwa kwa mara ya kwanza

Airmanula

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
3,758
5,249
Kati ya mambo ambayo yalitia giza serikali ya awamu iliyopita ya tano ambayo hadi leo ni uchungu mkubwa kwa waliokumbwa na uonevu huo ni hili la wafanyabiashara wa mkoa wa Arusha wa maduka ya kubadilishia fedha za kigeni

Haitosahaulika hii siku ambayo ilileta maumivu makubwa kwa wafanyabiashara hao ambao walinyang'anywa fedha zao zote na maduka kufungwa kwa kile kinachodaiwa kua ETI kufadhili makundi ya kigaidi, kutakatisha fedha na sababu zingine lukuki ambazo hazikua na kichwa wala miguu kwasababu wafanya biashara hao walikua wanafanya biashara hizo kihalali kabisa na kufuata sheria zote.

Tunajiuliza zile pesa zilienda wapi? Zilichukuliwa na kupelekwa wapi au kwa nani na kwa sababu zipi? Suala hili tunashukuru limejadiliwa bungeni na nina imani serikali hii ya furaha ya awamu ya sita italitafutia ufumbuzi suala hili ambalo bado limewaweka wafanyabiashara hawa GIZANI bila kujua hatma yao na hatma za fedha zao zilizochukuliwa KIMABAVU.
 
Dhuluma ni mbaya sana kwa kweli warudishiwe tu pesa zao kama hazikupelekwa kwenye ma sgr..unakuta treni ajali za ajabu ajabu kumbe kuna hela za kuzuru watu ndani yake...
Kurudishiwa ni ngumu,Ila magu hakuwa MTU alooo.
Watu walipigwa mitaji yao na hakuna mahali utaenda kulalamika,kwanza alitumia jeshi kupora.

Kama chizi anaeza logwa tena basi na magu afe tena.
 
Na declear interest
Mm ni mwiongoni mwa wanaopinga biashara hii ya BE kufanyika kiolela holela currency exchange service sio sawa na uchuuzi wa maandazi hata ktk nchi zilizoendelea hii huduma hupatikana ktk ma bank tu sio mitaan.
 
Back
Top Bottom