Mzee Madoshi
Senior Member
- Feb 16, 2011
- 134
- 41
Kutoka Raiamwema kwenye kichwa cha habari " Kikwete anusurika, awang'oa wenzake' kuna sentensi zimenichekesha na kunisikitisha sana kwa hawa wanasiasa wetu. Kuna huyu waziri katumwa na wenzake awakilishe maoni yao katika kikao cha NEC kutetea wabunge waruhusiwe kugombea NEC:
Baada ya Kamati Kuu kumaliza kikao, hawakugundua na walijipanga upya kulikabili suala lao ndani ya NEC kama lingejitokeza. Nako kwenye NEC hawakuliona, walitaraji lingeandikwa wazi wazi. Kule ilikuja tu hoja ya wajumbe wapya wa NEC wafanye kazi zao kama shughuli za muda wote, wakaunga mkono.
Wassira anadaiwa kumuuliza mjumbe mwenzake wa Kamati Kuu na NEC, Abdulrahman Kinana; Hivi hili suala la wabunge kutogombea u-NEC limefia wapi? Naye Kinana baada ya kucheka akamjibu; aaah, mbona limeshapitishwa muda mrefu!
Mawazo yangu
Sasa kama ameshindwa hata kujitetea mwenyewe na wabunge wenzake, je anawezaje kutetea wananchi wake?, lakini la kushangaza wale wabunge wote waliotaka hoja yao ipite walikuwa wanafikiria nini kumtuma huyu Mzee? Na labda kusikitisha zaidi, kama wanashindwa kuelewa mtego mdogo kiasi hiki uliowekwa na kina Nape, je mtu huyu anawezaje kushughulikia masuala makubwa au mikataba mikubwa ya kitaifa yenye mitego ya kibiashara na kisheria?
Wazungu huwa wanatukana weusi kuwa If you want to hide something from a Black person, put it in a book. La huyu bwana limepitiliza huu msemo ..
Baada ya Kamati Kuu kumaliza kikao, hawakugundua na walijipanga upya kulikabili suala lao ndani ya NEC kama lingejitokeza. Nako kwenye NEC hawakuliona, walitaraji lingeandikwa wazi wazi. Kule ilikuja tu hoja ya wajumbe wapya wa NEC wafanye kazi zao kama shughuli za muda wote, wakaunga mkono.
Wassira anadaiwa kumuuliza mjumbe mwenzake wa Kamati Kuu na NEC, Abdulrahman Kinana; Hivi hili suala la wabunge kutogombea u-NEC limefia wapi? Naye Kinana baada ya kucheka akamjibu; aaah, mbona limeshapitishwa muda mrefu!
Mawazo yangu
Sasa kama ameshindwa hata kujitetea mwenyewe na wabunge wenzake, je anawezaje kutetea wananchi wake?, lakini la kushangaza wale wabunge wote waliotaka hoja yao ipite walikuwa wanafikiria nini kumtuma huyu Mzee? Na labda kusikitisha zaidi, kama wanashindwa kuelewa mtego mdogo kiasi hiki uliowekwa na kina Nape, je mtu huyu anawezaje kushughulikia masuala makubwa au mikataba mikubwa ya kitaifa yenye mitego ya kibiashara na kisheria?
Wazungu huwa wanatukana weusi kuwa If you want to hide something from a Black person, put it in a book. La huyu bwana limepitiliza huu msemo ..