kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,293
- 12,593
Moto wa kumbi ni moto mkali sana unaweza kuyeyusha chuma au kutoboa sufuria likiwa na maji yake ndani lakini hauna miale, moshi wingi wala kelele kama mioto ya mabiwi, nyika, kuni au petroli. Unapoota moto wa kumbi inakubidi ukae mbali kidogo vinginevyo utapata mbalanga.
Kwa muda mrefu wananchi na watumishi tumezoea viongozi wanaotoa sauti kubwa kama radi wanapokerwa na jambo fulani na kukemea. Na mara nyingi wanaweza kufoka sana mdomoni na hadharani kuhusu rushwa lakini matendo yao hayaendani na maneno yao. Wanaweza kuonekana wakimtaja Mungu sana lakini matendo yao yako kinyume na Mungu, wanaweza kuonekana wanawapenda viongozi wa dini lakini kuna viongozi wa dini wako jela kwa maagizo yao.
Rais Samia ni utamaduni mpya sana nchini ambao unaweza kuondoka na watu wengi sana na hasa wavaa suruali. Anaetaka apewe maji ya kunywa kwa ukali na kufoka na anaeomba maji kwa upole na unyenyekevu wote watapata maji yaleyale, matokeo yatakuwa yaleyele ya kupata glasi ya maji safi ya kunywa, lakini yule aliyeomba kwa upole atakuwa na faida ya ziada ya kupendwa zaidi na aliyemletea maji kuliko yule aliyefoka kwa ukali.
Ndugu zangu urais ni taasisi, jukumu na mamlaka, na sio jinsia, personality, dini, kabila wala kanda ya mtu alikotoka, lazima mindset zetu zibadilike haraka kutoka kusia sauti zinazokwaruza kwenda kwenye sauti nyororo lakini zenye maana ileile na zaidi.
Tuzoee utamaduni mpya wa kuongozwa, tii mamlaka bila shuruti
Kwa muda mrefu wananchi na watumishi tumezoea viongozi wanaotoa sauti kubwa kama radi wanapokerwa na jambo fulani na kukemea. Na mara nyingi wanaweza kufoka sana mdomoni na hadharani kuhusu rushwa lakini matendo yao hayaendani na maneno yao. Wanaweza kuonekana wakimtaja Mungu sana lakini matendo yao yako kinyume na Mungu, wanaweza kuonekana wanawapenda viongozi wa dini lakini kuna viongozi wa dini wako jela kwa maagizo yao.
Rais Samia ni utamaduni mpya sana nchini ambao unaweza kuondoka na watu wengi sana na hasa wavaa suruali. Anaetaka apewe maji ya kunywa kwa ukali na kufoka na anaeomba maji kwa upole na unyenyekevu wote watapata maji yaleyale, matokeo yatakuwa yaleyele ya kupata glasi ya maji safi ya kunywa, lakini yule aliyeomba kwa upole atakuwa na faida ya ziada ya kupendwa zaidi na aliyemletea maji kuliko yule aliyefoka kwa ukali.
Ndugu zangu urais ni taasisi, jukumu na mamlaka, na sio jinsia, personality, dini, kabila wala kanda ya mtu alikotoka, lazima mindset zetu zibadilike haraka kutoka kusia sauti zinazokwaruza kwenda kwenye sauti nyororo lakini zenye maana ileile na zaidi.
Tuzoee utamaduni mpya wa kuongozwa, tii mamlaka bila shuruti