Mmmmh!! Sikubaliani na wewe huu ni mwaka sasa unakatika tokea nimeachana na aliyekuwa girlfriend wangu kutokana na tabia zake ambazo hazivumiliki/kurekebika(sipendi kuziweka wazi hapa)ila unaweza ukaziita ugonjwa wa Ukoo wao(wanawake wote kuanzia bibi mpaka mama yakle mzazi na dada zake wanaumwa hizo TABIA CHAFU)
Basi nikaambiwa piga kimya Rural Swagga mpenzi atakuja nimesubiri nimejiandikisha mpaka kanisani(mm ni mlutheri) nikaanza kuhudhuria ibada+sadaka na fungu la kumi lakini bado bilabila, watoto wa mjini wanasema bado JAU..Na kwa kweli sina tabia yeyote chafu na mbaya au madhaifu yeyote zaidi ya U-Workahollic wangu due to the nature of the Work(iam a programmer)Pombe dini yangu inaruhusu na huwa natumia kwa kiasi,Nimepanga chumba,nalipa umeme,maji,kingamuzi(sikitaji jina),Usafiri wa kawaida,Na kiwanja pia nimebahatika kuwa nacho japo ni nje ya jiji lakini najua ndani ya miaka 5 ijayo patakua pamepiga hatua kimaendeleo.WAPENDWA MPAKA LEO HII SIJAONA HATA DALILI YA HUYO MTARAJIWA AU NIMELOGWA?
cc/
Heaven on Earth