Nilizama katika mapenzi mazito,,,,,,

Nilizama katika mapenzi mazito,,,,,,

Ma boy emb cool down kwanz,kuna uwezekan mkubwa ukawa umewekwa kwenye mtego, huyo unaeona anakupoza kwa upand wangu naon n kama mtu hatar xana. Ckwambi uanza mchukia bt be care, Halaf kuhusu huyo wa nyodo kaa zako punguza kmtumia sms,kumpigia taratibu bdae utaacha kabsa. Bt ucmchukie kuwa 2 wa kawaida ila uliyepoteza matumain kwake
Sawa, ila mi nadhani huyu anayenipoza ameona jins gan navoumia na ndo mana ameamua kufanya hivyo. Na pale nyumbani kwa huyu aliyekua wangu hayupo na hana mpango wa kurudi tena ndo mana nikaomba ushauri
 
tulia kaka yangu subira yavuta heri me yalinikuta nikatulia kumbe mpenzi kabadilika cz ya maneno ya watu wa karibu alivyogundua wanamdanganya hadi leo karudi kwangu na kaganda
Sawa lady nashukuru
 
Habari zenu wana jf, nimefurahi kupata sehemu ambayo naweza kusema imenisaidia kujua mawazo ya watu na jinsi gani tunaweza kusaidiana katika masuala mazima tunayokabiliana nayo katika maisha yetu ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kupost humu na ntafurah kama mtanisaidia ktk hili suala linalontatiza...
Nilizama ktk mapenzi mazito ya msichana ambaye jina lake naomba nilihifadhi, yeye ndie alikua wa kwanza kunitamkia kuwa ananipenda, na kwakua hakua mgeni machoni mwangu, na tulishazoeana hapo mwanzo kama mtu na rafiki yake, ilibidi nikubali kuwa naye, nilimpatia mapenzi mazito na tulikua watu wenye furaha sana katka mapenzi yetu, hakuchoka kutabasamu kila alipokutana na mimi. Nilimsimulia story nzuri pamoja na kumpatia zawadi kama inavotakiwa kwa wapenzi. Naye pia hakusita kunipatia zawadi mbalimbali ambazo zilinifanya nijione ni mimi tu katika dunia ya mapenzi. Katika mwezi wa 1 mwaka 2013, aliweza kuchukuliwa na kwenda kwa Baba mkubwa wake mkoani Shinyanga, alipokua huko tuliweza kuwasiliana kupitia simu kila mara. Na aliporudi mapenzi yetu yaliendelea kama kawaida___. Huku nyumbani alikua anaish na wazazi wake mdogo wake pamoja na kaka yake, sikuzoeana kivile na kaka yake. Pia kulikua na dada mmoja hivi ambae yeye (Mpenzi wangu) aliweza kunitambulisha kuwa ni dada yake, nami niliamini. Na haikuchukua muda kumzoea kwani alikua mchangamfu, mkarimu na mpenda kusali, na aliweza kunishauri mara kwa mara kwenda kusali naye ila sikuwah kufanya hivyo,,, Lakini wakati anarudi kutoka Shinyanga, dada huyo aliyeniambia ni dada yake aliondoka pale kwao na kwenda kwa wazazi wake. Hivyo basi kumbe hakua dada yake na wala hawana mahusiano yoyote.
Sasa alipokuwa hapa nyumbani huyo Mpenzi wangu mimi, hakua na muda wa kutosha wa kukutana na mimi kama alivyokua akisema mwenyewe. Nikiwa naongea naye anaondoka, kifupi ni kuwa alionesha kunichoka, mimi sikukata tamaa, nikijaribu kumpatia zawadi kama zamani, hapo alikua anaonesha tabasamu. Kitu kingine anadai kuwa kuna watu walimfuata na kumwambia aachane na mimi, na hicho ndicho kitu ambacho kinanisumbua na sijawahi fanya kitu kama hicho. Na yeye anajua jins gani nampenda, siku hizi amebadilika na akiniona anatafuta njia nyingine ya kwenda, zile romantic moments tulizokuanazo zamani sasa hazipo.
Sijui amepatwa na jinamizi gani, nikiongea naye anaonesha kama amechoka flan mi hata simuelewi, lakn mimi bado nampenda.
Na sasa yule dada, ambaye aliniambia ni dada yake kumbe hawana udugu wowote anatumia muda mwingingi kunifariji na kunipa moyo na kuniambia huenda labda mungu hajanipangia bado mtu wa kuwa naye. Ananifariji na kunipa moyo kiasi kwamba najikuta namsahau mpenzi wangu.
***
Ambacho naomba mnisaidie ni kuwa ni muache mpenzi wangu wa zamani, niende kwa huyu dada, ambaye ananifanya nasahau matatizo nilo nayo? Au nimvumilie kwa kuamini kua ipo siku atabadilika na kuwa kama zamani? Manake nilimfanya kweli ajione mwanamke, na sikumfosi kufanya kitu alichowahi kuniambia hakimpendezi au kitu ambacho hakujiskia kufanya kwa wakati niliokuanaye.
Ningependa kumaliza kwa kusema nakushukuru wewe ambae umetumia muda wako kwa kusoma post hii, naomba ushauri wako tafadhali. Nifanyeje?
We kaka usipoteze muda wako na mtu ambae hataki kuwa na ww!Hao wanawake wote hawakufai wewe hujui kilichotokea kati yao na isitoshe huyo mpenzi wako hakuwa mkweli kuhusu huyo shoga yake kwahio hapo kuna ulakini...Mimi nakushauri usonge mbele na maisha yako...Utapata mtu mwenye mapenzi ya dhati nawe inshallah...Utaumia lakini U WILL HEAL WITH TIME...
 
We kaka usipoteze muda wako na mtu ambae hataki kuwa na ww!Hao wanawake wote hawakufai wewe hujui kilichotokea kati yao na isitoshe huyo mpenzi wako hakuwa mkweli kuhusu huyo shoga yake kwahio hapo kuna ulakini...Mimi nakushauri usonge mbele na maisha yako...Utapata mtu mwenye mapenzi ya dhati nawe inshallah...Utaumia lakini U WILL HEAL WITH TIME...

thank you, nashukuru sana kwa ushauri wako,,,
 
Kaka angu unataka kusema wanaume hamkosei nimekujibu swali ambalo hujaniuliza sababu nimeshuhudia mwanaume akikosea

ok, tunakosea lakn, si wote na makosa yetu kwa asilimia kubwa yanatokana na reaction zenu
 
Ndg yangu kusoma hujui hata picha nayo inakushinda....we chapa lapa faster atakuzingua sana huyo kama vp jitulize kwa mfariji wako.
 
Mapenz ndivyo yalivyo ndugu,ktu cha muhimu ni kukaa na mwenza wako na kutomuogopa na mweleze yale yako yanakusibu,kwa njia moja au nyingine utakuwa unauwezo fulani wa kudai haki yako na kulinda wenu upendo,uckate tamaa mapema ivyo kwa 7bu hata huyo mdada anayekupa ushauri mpaka unamsahau wako mwenza anaweza kuwa ndo chanzo cha yako matatizo,kwa mtazamo wangu wewe ni mwanaume unajua jema lp na baya lipi,ko jembe unabidi kuwa care na maamuzi unayofanya.
 
.......Somo linajirudia,

NINI/NANI chaguo lako katika mapenzi? Au unatumika tu kama 'hankerchief?'

Jiulize, kwanini yule alikupenda nawe ukampenda, kiasi ya huyu kukuchanganya na upendo 'mwingine!'

It is a learning process, you have to go through this phase ili -ugangamale!- Ushauri wangu, endelea na hii swde B ya 'Egoli'.... "Stelingi" hauwawi!
 
^^
Mwanaume akimpenda mwanamke amekosa yote.
Mwanamke akimpenda mwanaume amepata yote.
^^


..oo big Noo...
.. the opposite is true... u wrote this to go hand in hand with thread, but sio kweli...
...MWANAUME ndio akimpenda mwanamke hapo maisha yataenda...not otherwise... mwanaume can tune a woman the way he wants... mwanamke kumfuata au kumtongoza mwanaume HIYO HAIPO.....
...U GET IT...
 
Mkuu Himidini , kesho naomba unifafanulie hizi sentensi zako mbili hata kwa kupitia PM. Am very serious to understand them in deep
^^
Mwanaume akimpenda mwanamke amekosa yote.
Mwanamke akimpenda mwanaume amepata yote.
^^
 
..oo big Noo...
.. the opposite is true... u wrote this to go hand in hand with thread, but sio kweli...
...MWANAUME ndio akimpenda mwanamke hapo maisha yataenda...not otherwise... mwanaume can tune a woman the way he wants... mwanamke kumfuata au kumtongoza mwanaume HIYO HAIPO.....
...U GET IT...

^^
Kuna tarehe utawajua wanawake vizuri,,na utakumbuka huo usemi.
^^
 
Back
Top Bottom