Huna haja ya kumuumiza maana hutakiwi kulipa baya kwa baya, jifunze kusamehe na haijalishi uliumizwa kwa kiasi gani! Pengine huo ni mtihani uliopewa na kipimo ili baadae uje upate hesabu nzuri mbinguni! Mshinde shetani, akirudi mkaribishe kwa upendo, mwambie nimekusamehe maana ulikuwa hulijui utendalo, nakwambia atakupenda kwa kiasi ambacho hukuwahi kukiwazia, binadamu huwa tunakosea padogo tu kwa kukosa maarifa, yaani huyo akijileta usali kabisa maana wewe pekee ndo umeonekana kuwa wa dhamani kwake! Na akija mwambie nataka ndoa kabla ya yote.