Nilizalishwa na kudhalilishwa

Nilizalishwa na kudhalilishwa

Ukitaka kuishi kwa furaha msamehe mtu bila kuwa na condition. Tunafundishwa upendo wa kweli (agape) hauna masharti wala haujivuni na unastahimili jiulize ukimtukana na kumdhalilisha itakusaidia nini??
Jibu ni hakuna. Hivo mwambie nimekusamehe kwa yote uliyofanya japo hatuwezi kurudiana.
Utaishi kwa furaha sana .
Usimchukie yeg chukia uovu wake kwahiyo Mwombee ile roho chafu imuondoke asifanye madhambi yale kwa mtu mwingine
 
M nahis ungemblock kila sehem ingekuwa vzuri tena usifikirie kabsa kuwa ni mzazi mwenzio maana hata yeye hakukufikiria pindi anakuaibisha
 
Labda kama ningelikuwa siwajui wanawake ningelikupa ushauri nini cha kufanya, lakini wanawake akili zake sijui huwa mnazipeleka wapi mnajifanya mna huruma kuliko mama huruma mwenyewe. Wazazi huwa hawatengani, hizo hasira ulikuja nazo hapa sijui unakuja kuomba ushauri jamaa yupo humu humu anakusoma tena atakuja kwa kwa nguvu zote, utamsamehe na maisha yataendelea kama kawaida... wanawake ni viumbe dhaifu.
 
Huna haja ya kumuumiza maana hutakiwi kulipa baya kwa baya, jifunze kusamehe na haijalishi uliumizwa kwa kiasi gani! Pengine huo ni mtihani uliopewa na kipimo ili baadae uje upate hesabu nzuri mbinguni! Mshinde shetani, akirudi mkaribishe kwa upendo, mwambie nimekusamehe maana ulikuwa hulijui utendalo, nakwambia atakupenda kwa kiasi ambacho hukuwahi kukiwazia, binadamu huwa tunakosea padogo tu kwa kukosa maarifa, yaani huyo akijileta usali kabisa maana wewe pekee ndo umeonekana kuwa wa dhamani kwake! Na akija mwambie nataka ndoa kabla ya yote.
 
Ukitaka kuishi kwa furaha msamehe mtu bila kuwa na condition. Tunafundishwa upendo wa kweli (agape) hauna masharti wala haujivuni na unastahimili jiulize ukimtukana na kumdhalilisha itakusaidia nini??
Jibu ni hakuna. Hivo mwambie nimekusamehe kwa yote uliyofanya japo hatuwezi kurudiana.
Utaishi kwa furaha sana .
Usimchukie yeg chukia uovu wake kwahiyo Mwombee ile roho chafu imuondoke asifanye madhambi yale kwa mtu mwingine
Haleluya.. Mtumishi.
Andaa sadaka...sasa.
 
Siri za ndani huwa zinakera sana kuziweka hadharani, ulimkubali mwenyewe hadi mkazaa hivyo huo ni msalaba wako uubebe hadi kalvario. ..
 
Daaaaaaah nmesoma hii post had choz lmenidondoka,umenifanya nikumbuke kitu pole sanaa,cha kufanya we mpotezee tu huyo bwana na usithubutu kumpa hata 1sec ajieleze yaan kaa mbal nae kabsaaa usijarbu kumsogelea hata na hata mawasiliano kata mpe blok kila mahala pia hata akienda kwa nduguzo kataa kabsa vkao vya kusuhisha yaan usikubali acha nae aisome namba usimhurumie hata kdgo,but kua makin sana usijiingize kwenye mahusiano mpk utapopata mtu ambae dhahir ana lengo na wewe otherwise Bora ukawa sngle tu uenjoy life na mwanao,wanaume washenzi my dear take care yalokutokea yasije jirudia
Wee acha tu, nashukuru kwa ushauri
 
Back
Top Bottom