Niliyoyaona Jijini Mwanza

Kusini bado wamelala na ukipenda kule unalima unasafirisha maana tena kusini sio mikoa ya biashara ni ya kilimo TU ila biashara unatafta mikoa Kanda tofaut utapiga Hela mno japo Kuna ushirikina wanaloga wale wakiona unapiga kazi
 
ushirikina wanaloga wale wakiona unapiga kazi
Mbona wazungu wao wakija wanapiga kazi ama itafute ngoizi bandia uvae ili wasijue wewe Ni mbongo. Ama una act Kama umetoka nchi nyingine so imekuja kuwekeza unatafuta wenyeji unawatumia. Pia ukiwa na capital ya maana nadhani hata mchawi hakugusi am sure.

Hivi Hakuna mchawi akaniwezesha nikapata betting hata ya 800M ivi jamani. Hawa waganga wangekuwepo kweli vijana tungekuwa tunahangaika Ajira kweli.
Kuna mwekezaji mmoja akakimbia Nigeria sijui Ni Nani huyo
 
Itakua Mwanza umefika peke yako, binafsi nishafika Mwanza zaidi ya mara 3 kuna baadhi ya sehemu wanaongea kilugha mfano stand ya mabasi
Acha uongo stand gani hiyo ,stand siku zote kuna mwingiliano wa watu wageni labda kama ni sokoni na sokoni haipo hiyo,

Kikawaida kila mkoa una wakazi wake n a lugha ya wakazi hutawala kwa kiasi fulani hilo sikatai ila si kwa miaka hii sasa,mwingiliano umekuwa mkubwa sana ni nadra sana kukuta mtu anaongea kilugha mjini kati ila pia si ajabu kukuta mtu anaongea mana ni lugha kama lugha zingine,arusha kwa kuongea kilugha mjini wanaongoza hasa wakazi wa kilimanjaro huwa hawajivungi na lugha yoa,
Na mtu kuongea ki lugha si zambi wala ushamba ila inategemea na mtu na mazingira yake,
 
Waganga walikuwag zamani hasa BARIADI huko walikuwa wanatoa dawa za ndagu lakin now wapo waganga njaa TU ukikaa kizembe wanakuibia 😂😂
 
Ila wasukuma kwa kweli mkisoma wote na mlivyo wengi hii nchi mkawa wamoja mnaweza kuipindua pia itakuwa vigumu sana kuwaepuka kila nyanja za serikalini .

Kila mkoa ninaoenda lazima nikutane na wasukumu ila ni wastaarabu sana pia wavumilivu jinsi mnavyotaniwa ila mko poa sana.

Tulisoma na jamaa yaani mpole sana anataniwa sana hata kurusha ngumi yaani anacheka ila darasani ni hatar kweny paper anajua sana.

Bwana sisi wa Pwani tulikuwa tunavurugu na kuongea mpaka kero😂😂wakorofi sana sana hatukubali kushindwa
 
Ukweli sisi hatuna mambo mengi sana japo Kuna Kanda znalazimisha bifu huku zikijua haziwezi ni sawa na kujenga bifu na mvua huku waishi majarubani
 
Niko huku asee kisukuma nilugha yataifa hapa
Hebu niambie ni wapi Arusha mjini ukikutana na wamasai wanaongea kiswahili? Hata hao mnaowaita sijui waarusha ni jamii za wamasai tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…