Niliyoyaona Jijini Mwanza

Niliyoyaona Jijini Mwanza

Glas

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2016
Posts
1,242
Reaction score
1,188
Wakuu wazima?

Nafikiri kuna kapost kangu niliwah post humu kuuliza sehem nzuri ya kupumzika kwa hapa Mwanza.
Sasa kwa kipindi hiki cha wiki 2 nilizokaa huku hay ndo niliyoyaona na kujifunza

1. Wanawake wanapiga kazi sana huku(wanajishughulisha) mida ya jioni barabarani utakutana nao sana wakiuza either matunda, dagaa, samaki, maharagwe yaliyochemshwa tu, nyanya na vikorombwezo vingine4, pia wanachoma mahindi na kuyauza.

2. Wengi wa wasichana huku ni waoga sana hasa kwa strangers.

3. Draft la huku wengi hucheza French( hawajui kuhusu British).

4. Kila wanapokaa hudhani wote ni wa huku hivyo huongea tu kilugha.

5. Hotels and Lodge za huku no bei rahis sana sana huanzia 30k.

6. Mwanza ni mji mzuri sana, una mandhari nzuri kuliko Arusha( kwa mtazamo wangu)

Asanteni wakuu
 
Namba 6 imenifurahisha
Mwanza hua ni nzuri bana, ndoto za watu wa Arusha ni kuishi na kuwekeza mwanza hauwezi the kusikia msukuma anawaza kwenda arusha afadhali aende ifakara, lindi, chunya, kigoma, mpanda, sumbawanga, madibila, rujewa, ubaruku, ambapo atalima na kufuga au kuchimba dhahabu , kuliko akateseke arusha
 
Mwanza hua ni nzuri bana, ndoto za watu wa Arusha ni kuishi na kuwekeza mwanza hauwezi the kusikia msukuma anawaza kwenda arusha afadhali aende ifakara, lindi, chunya, kigoma, mpanda, sumbawanga, madibila, rujewa, ubaruku, ambapo atalima na kufuga au kuchimba dhahabu , kuliko akateseke arusha

Umeona ee Mwanza Mwanza
 
Mwanza wanawake wanakimbiza baiskeli kinoma, tena wanaendesha zile Phoenix alaf mrembo kuwazidi wenzake baiskeli yake inakua ina swaga flan hivi anaitolea kiti Cha nyuma anaweka na bendera ya Simba au yanga hapo mbele
 
Back
Top Bottom