Niliupenda Muungano...

Niliupenda Muungano...

Siku zote unapo muona mtu analalamjka,basi usimzarau msikilize
anaihitaji nini ?
Wanacho kidai Wazanzibari ni sahihi ,
Hebu jiulize kwa nini walalamike, hakuna mtu ambaye hapendi maslahi ila ukiona lawama jua maslahi hakuna na kama yapo bisi ni yawachache.
Hivi mnajua kama Wazanzibari wamepoteza wasomi wao wengi kutokana na Muungano huu, na sio kama walipotea porini, lahasha bali waliuliwa akiwemo ,
Miongoni mwao ni :
OTHMANI SHARIF & HANGA .hiki ni kilio kikubwa kwa jamii ya Wazanzibari .Sijui kuna siri gani hapa
Ilio sababisha Watu kutupwa nungwa,
Hali yakuwa hai .
Na isitoshe hebu tujiuljze ni Muungano gani huu ulio fanyika bila ya kuwepo wanasheria wanchi zote mbili ( Tanganyika na Zanzibar ) hebu tufikirie .Jamani tuamkeni hapa panakitandawili kizito Tusithpiane lawama kuna haja ya kuwepo Tanganyika na Zanzibar kisha ndio tuitafute Tanzania .
 
Kwa hiyo tulianza na Nchi 1, Serikali 2 baadaye Nchi 2, Serikali 2 na sasa tunaelekea kwenye Nchi 1, Serikali 1, lakini kwa kuvunja Muungano! Kweli Waafrika tumelaaniwa maana wakati mataifa makubwa yanaungana, (hata Crimea ilivyojitenga na Ukraine imeungana na Russia), vinchi vidogo vidogo vya kiafrika vinatengana!

Kwenye Crimea, kwanini na sisi tusiige kwa kupiga kura ya maoni?
 
Mimi sasa nimekuwa muumini wa Serikali Moja; Moja ya kwao na Moja ya kwetu, tukutane Umoja wa Mataifa kama ndugu wamoja! Undugu haung'ang'aniwi na ndugu akishalalamika kuwa unamzibia ni wakati wa kumtakia kila la kheri... Niliupenda Muungano lakini Mungu ameupenda zaidi..
bwana alitoa na bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe
 
Na je mtagawana vipi udugu na upendo mlioujenga kwa muda mrefu?

Hivi kwani hizo ndoa za miaka 50 hazivunjiki? Athari za ndoa ziko palepale iwe miaka 5, 10, 20, 30 au 50. Hoja ni kuwa mpk ndoa inavunjika maana yake hiyo ndio tiba ya mifarakano na mitifuano iliyoko ndani ya ndoa hiyo.
Juu ya kugawana upendo na udugu- ukweli ni kwamba hakuna cha kugawana. Mkikaa nje ya ndoa na kugundua unauhitaji upendo na udugu wa mwenzio basi mnaanza mazungumzo ya namna ya kurudianna
 
Back
Top Bottom