Mkuu Mwanakijiji, hivi umekaa ukatafakari kujua madhara yatakayojitokeza ikiwa Muungano utavunjika? Hivi uliwahi kuwafikiria wale wafanyabiaahara wenye asili ya Pekba ambao wamejazana pale Tandika, Ilala, Kariakoo na Buguruni? Vipi wataishi ikiwa Muungano utavunjika? Mkuu Mwanakijiji, hivi uliwahi kufikiria juu ya hawa watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wametoka pande zote za muungano na wapo kila upande? Mkuu, hivi uliwahi kutafakari mathalan juu ya kuvunjika kwa ndoa yako ambayo imesumu zaidi ya miaka 50 mkiwa mmezaa watoto na wajukuu, mmechuma mali nyingi na kikubwa zaidi mmejenga udugu wa kifamilia?