Suprise
JF-Expert Member
- Nov 2, 2012
- 2,696
- 1,063
Habari wana MMU,
Nimesikia na kushuhudia mengi na kupokea ushauri juu ya kuyumba kwa ndoa yangu lakini napenda kukiri kua wengi wamekua wakinikatisha tama na kunitaka nijiengue .hivyo naombeni msaada wa mawazo utakaonifanya niirudishe ndoa yangu na si kuivunja,
Nna miaka tisa na mume wangu kipenzi, tumebahatika kupata watoto 2, miaka 6 ilikua ya amani na pendo ndani ya nyumba, mume wangu alinionyesha upendo wote niliokua nautaraji toka kwake.
Hali ilikua mbaya mwanzoni mwa mwaka 2011, ambapo mume wangu alianza kunionyesha vitendo vya tofauti , hakua msikivu tena, anachelewa kurudi home , baada ya muda nilicikia na kuthibitisha haya;
1. Ni kweli kua ana nyumba ndogo kimara
2. Ni kweli kua ana uhusiano usio rasmi na mfanyakazi mwenzie
3. Ni kweli kua safari za kikazi zimeongezeka maradufu
4. Ni kweli kua hana mda na familia yake,
5. Ni kweli kua hata haki ya ndoa inasuasua na mpaka nilazimishe.
Vikao vya familia na wasimamizi wa ndoa vimefanyika viwili akakiri na kusema atavunja mahusiano ya nje , na hii ilionyesha mafanikio kidogo kwa mwaka jana alijirudi na inasemekana ameachana na nyumba ndogo hiyo ya kimara,
Kilichonisukuma kuandika ni kua amebadilika tena na nahisi ameanzisha makoloni mapya ingawa haya cjayahakikisha,amekua ni mtu mkorofi halali ndani, akirudi mda anaotaka,
Kuhusu matumizi ya nyumbani na mengineyo hana matatizo anaprovide inavyotakikana,
Naumia , natamani miaka 6 ya mwanzoni ya upendo irudi tena, hana sababu aliyowahi kuitoa zaidi ya kupitiwa na shetani,
Wengi wamenishauri kuivunja ndoa lakini moyo wangu bado upo kwake na nahitaji kiapo changu kwake kiwe cha milele, Hivyo naombeni ushauri wa kuirudisha ndoa yangu na c kuivunja.
Nimesikia na kushuhudia mengi na kupokea ushauri juu ya kuyumba kwa ndoa yangu lakini napenda kukiri kua wengi wamekua wakinikatisha tama na kunitaka nijiengue .hivyo naombeni msaada wa mawazo utakaonifanya niirudishe ndoa yangu na si kuivunja,
Nna miaka tisa na mume wangu kipenzi, tumebahatika kupata watoto 2, miaka 6 ilikua ya amani na pendo ndani ya nyumba, mume wangu alinionyesha upendo wote niliokua nautaraji toka kwake.
Hali ilikua mbaya mwanzoni mwa mwaka 2011, ambapo mume wangu alianza kunionyesha vitendo vya tofauti , hakua msikivu tena, anachelewa kurudi home , baada ya muda nilicikia na kuthibitisha haya;
1. Ni kweli kua ana nyumba ndogo kimara
2. Ni kweli kua ana uhusiano usio rasmi na mfanyakazi mwenzie
3. Ni kweli kua safari za kikazi zimeongezeka maradufu
4. Ni kweli kua hana mda na familia yake,
5. Ni kweli kua hata haki ya ndoa inasuasua na mpaka nilazimishe.
Vikao vya familia na wasimamizi wa ndoa vimefanyika viwili akakiri na kusema atavunja mahusiano ya nje , na hii ilionyesha mafanikio kidogo kwa mwaka jana alijirudi na inasemekana ameachana na nyumba ndogo hiyo ya kimara,
Kilichonisukuma kuandika ni kua amebadilika tena na nahisi ameanzisha makoloni mapya ingawa haya cjayahakikisha,amekua ni mtu mkorofi halali ndani, akirudi mda anaotaka,
Kuhusu matumizi ya nyumbani na mengineyo hana matatizo anaprovide inavyotakikana,
Naumia , natamani miaka 6 ya mwanzoni ya upendo irudi tena, hana sababu aliyowahi kuitoa zaidi ya kupitiwa na shetani,
Wengi wamenishauri kuivunja ndoa lakini moyo wangu bado upo kwake na nahitaji kiapo changu kwake kiwe cha milele, Hivyo naombeni ushauri wa kuirudisha ndoa yangu na c kuivunja.