nimechafukwa
JF-Expert Member
- Oct 2, 2013
- 290
- 237
Mwaka 2015 nilimpoteza baba yangu ambaye alikuwa tegemezi kubwa sana katika familia, enzi za uhai wa baba financially alikuwa vizuri sana. Nilikuwa nimeajiriwa, pesa zangu ziliishia kwenye pombe na wanawake. Imagine at the age of 30 I was staying at home with my parents na nilikuwa na kazi nzuri tu.
Nilikuwa ninaamini nina back-up ya baba yangu milele (tumeambiwa na vitabu vya dini tusiwategemee binadamu). Nakumbuka wakati natoka makaburini nilikuwa na mawazo mengi sana, maisha yatakuaje bila Baba? Mama yetu nani atamtunza ingali tulikuwa tukitegemea mshahara mnono wa Baba?
Niliamua kuishi nyumbani kwa miezi mitatu tu nikaenda kupanga, wakati huo pesa zangu zote nilizielekeza kwenye investment, pombe niliacha, siku-date na mwanamke yoyote for 2 yrs, baada ya miaka mitatu niliona mabadiliko makubwa sanaa, ngoja niwatajie hapa kwa ufupi:
1. Nimeoa nina mtoto mmoja
2. Situmii pombe
3. Naishi kwangu
4. Nina miradi mitatu.
Ni wengi sana wanaonaga maisha yao yamefika mwisho pale wanapopoteza watu wao wa karibu lakini nakuambia ndugu yangu, be positive!
Nilikuwa ninaamini nina back-up ya baba yangu milele (tumeambiwa na vitabu vya dini tusiwategemee binadamu). Nakumbuka wakati natoka makaburini nilikuwa na mawazo mengi sana, maisha yatakuaje bila Baba? Mama yetu nani atamtunza ingali tulikuwa tukitegemea mshahara mnono wa Baba?
Niliamua kuishi nyumbani kwa miezi mitatu tu nikaenda kupanga, wakati huo pesa zangu zote nilizielekeza kwenye investment, pombe niliacha, siku-date na mwanamke yoyote for 2 yrs, baada ya miaka mitatu niliona mabadiliko makubwa sanaa, ngoja niwatajie hapa kwa ufupi:
1. Nimeoa nina mtoto mmoja
2. Situmii pombe
3. Naishi kwangu
4. Nina miradi mitatu.
Ni wengi sana wanaonaga maisha yao yamefika mwisho pale wanapopoteza watu wao wa karibu lakini nakuambia ndugu yangu, be positive!