Nimekumisi sana Baba mwenye nyumba wangu

Nimekumisi sana Baba mwenye nyumba wangu

Mr Mhando

Member
Joined
Nov 2, 2018
Posts
21
Reaction score
34
Leo nimekaa nimemkumbuka baba mwenye nyumba yangu, kipindi nipo chuo huko mkoa Xy nilikuwa mlevi sana na baba mwenye nyumba yangu alikuwa ni mlevi sana, lakini walevi wastaarabu, tuliivana sana,

Sasa ilikuwa kila ikifika muda wa kodi lazima pesa nimpe siku ya ijumaa, nitamtegea muda yupo nyumbani nitaenda kununua bia 4 mbili zangu mbili zake basi namuita nje tunakunywa, then najifanya nina stress sana kisha nampa hela yake ya kodi, wakati huo nimeshampa kiu ya pombe,

Utasikia anasema john hebu twende hapo tukanywe moja moja, aisee tukitoka sasa nilikuwa nahakikisha kodi yangu naitumia vizuri kuna muda tunarudi hadi asubuhi yaani, ikawa ndio utaratibu wangu huo alikujaga akanistukia bana, 😂
Nimemis sana moment za kutumia kodi yangu
 
Mwanaume anam-miss baba wake mwenye nyumba....kumbe wote walevi!

Nilifikiria mengine kabisa!

IMG_20201227_091146.jpg
 
Aisee umenikumbusha nyakati za chuo na baba mwenye nyumba off campus, alikuwa mshirika wangu ktk ulevi..akigombana na mke wake wakiwa wamelewa mimi ndie nilikuwa mwamuzi! Basi nilijizolea ujiko na kupewa kipaumbele kama kijana wa familia...ilipekea mm na baba mwenye nyumba tukafirisi biashara ndogo ya familia ambayo ni grocery.
 
Kuna operation kabambe imeanzishwa ya kula kiapo cha utii kwa Kipenzi chetu cha dhati mwamba mkombozi wa waislamu Imam Hussain ibn Ali AS.

Ikilazimika kila mtu atalishwa hiki kiapo kwa nguvu na lazima.

Maovu yamezidi kwenye jamii dhulma ukandamizaji unyanyasaji na uonevu ambayo haya yote kipenzi chetu cha dhati Imam Hussain aliuwawa kikatili akiutetea na kupigania.

Labaika ya Hussain.

The road to Karbala join the movement NOW!

Screenshot_2025-07-30-19-19-40-01_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12~2.jpg
 
Kuna operation kabambe imeanzishwa ya kula kiapo cha utii kwa Kipenzi chetu cha dhati mwamba mkombozi wa waislamu Imam Hussain ibn Ali AS.

Ikilazimika kila mtu atalishwa hiki kiapo kwa nguvu na lazima.

Maovu yamezidi kwenye jamii dhulma ukandamizaji unyanyasaji na uonevu ambayo haya yote kipenzi chetu cha dhati Imam Hussain aliuwawa kikatili akiutetea na kupigania.

Labaika ya Hussain.

The road to Karbala join the movement NOW!

View attachment 3436333
Takataka gani tena hizi
 
Mwanaume rijali huwezi kumtamkia mwanaume mwenzako umem miss, hiyo sio sawa
 
Back
Top Bottom