Nilinusurika kufa kwenye kilimo cha umwagiliaji

Nilinusurika kufa kwenye kilimo cha umwagiliaji

Njemba Soro.

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2013
Posts
4,281
Reaction score
7,476
Habari....

Ilikuwa mwaka fulani msimu wa kilimo mvua ikaacha kunyesha. Sasa plan B ili mazao yasikauke ni kutumia mifereji inayotoa maji mtoni. Mwenyekiti wa kijiji akaleta utaratibu wa kihuni na kupendelea zamu za kumwagilia. USIKU NIKAWA NAENDA KUJIFUNGULIA MAJI BILA RUHUSA.

Aisee siku moja jamaa wakaniwinda wakanikamata, na walijua ni mimi maana shambani kwetu kulikuwa na maji bila zamu kufika na mahindi yamesitawi tofauti na majirani. Nilipigwa rungu la kichwa ghafla nikajua hapa nikishindana hawa jamaa wapo wengi wananiua.

NIKAJIFANYA NIMEKUFA, NIKAPIGAPIGA MIGUU NIKAJINYOOSHA KAMA NIMEKUFA. Jamaa walikimbia mbio za ajabu nikaamka nikafungulia maji kuelakea kwetu nikamwagilia hadi asubuhi, nilibakiza sehemu ndogo sana ya shamba letu ndipo wakaja kucheki wakakuta sijafa na nimekaribia kumaliza shamba. Wakalalamika sana kwa baba yangu lakini mimi nikasema nilikuta maji shambani nikaanza kumwagilia mahindi....

WALE WAZEE WANNE WAMESHAKUFA NA WENGINE NI WAZEE SANA KWA SASA ILA NI WASHKAJI ZANGU SANA.
 
Mkuu inaonyesha kichwa umekomaa Rungu likutulie kichwani na uamke kuendelea na kazi.
 
HAMNA SIKUNYA... ila lilikuwa rungu la kichwa mwili ukafa ganzi... na ilikuwa ghafla maana sikuwa nimewaona, palepale nikaekti kufa.
Inaitwa Ambush
Yaani Umejikuta Katikati Duniani Haupo, Ahela Unatafutwa
Hakika Bila Shaka Ndogo Ilitoka Ingawa Ukaona Kama Umelowa Maji
 
Habari....
Ilikuwa mwaka fulani msimu wa kilimo mvua ikaacha kunyesha. Sasa plan B ili mazao yasikauke ni kutumia mifereji inayotoa maji mtoni. Mwenyekiti wa kijiji akaleta utaratibu wa kihuni na kupendelea zamu za kumwagilia. USIKU NIKAWA NAENDA KUJIFUNGULIA MAJI BILA RUHUSA. Aisee siku moja jamaa wakaniwinda wakanikamata, na walijua ni mimi maana shambani kwetu kulikuwa na maji bila zamu kufika na mahindi yamesitawi tofauti na majirani. Nilipigwa rungu la kichwa ghafla nikajua hapa nikishindana hawa jamaa wapo wengi wananiua.NIKAJIFANYA NIMEKUFA, NIKAPIGAPIGA MIGUU NIKAJINYOOSHA KAMA NIMEKUFA. Jamaa walikimbia mbio za ajabu nikaamka nikafungulia maji kuelakea kwetu nikamwagilia hadi asubuhi, nilibakiza sehemu ndogo sana ya shamba letu ndipo wakaja kucheki wakakuta sijafa na nimekaribia kumaliza shamba. Wakalalamika sana kwa baba yangu lakini mimi nikasema nilikuta maji shambani nikaanza kumwagilia mahindi.... WALE WAZEE WANNE WAMESHAKUFA NA WENGINE NI WAZEE SANA KWA SASA ILA NI WASHKAJI ZANGU SANA.
Hahahaa, umenikumbusha kitambo.. Tuliwahi piga mwizi usiku wa manane akajifanya amekufa. Kuna wazee wakasema "Tumkate miguu tukalale". Jamaa akasema sijafa, naomba mnipeleke polisi. Alichezea kipigo aisee.
 
Jamaa walikimbia mbio za ajabu nikaamka nikafungulia maji kuelakea kwetu nikamwagilia hadi asubuhi,
Hahahaa, umenikumbusha kitambo.. Tuliwahi piga mwizi usiku wa manane akajifanya amekufa. Kuna wazee wakasema "Tumkate miguu tukalale". Jamaa akasema sijafa, naomba mnipeleke polisi. Alichezea kipigo aisee.
1569259906541.png
 
kichwa chako kitakuwa kina bullet proof kama cha mkemia
 
Umenikumbusha na mimi kipindi hicho Arumeru,ilibidi mashine inunuliwe kisima kichimbwe kuliko mambo yale.
 
Yaani,baada ya kula Rungu la kichwa ukapata nguvu ya kuendelea bila shaka halikua Rungu la mti wa mninga hilo,ungekufa ujue[emoji1] [emoji1] [emoji1] wanaume wa mikoanii, nimecheka hadi nimelia eti nikapigapiga miguu[emoji1]
 
Back
Top Bottom