Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,863
- 7,724
Mara nyingi, ukipoteza kitu ndio unajua thamani yake! Huwezi kujua sana thamani ya macho yako mpaka uwe kipofu kwanza.
Ukipoteza uono, yaani macho yako yasipoweza kuona kwa muda mrefu, kisha ghafla ukaanza kuona tena, ni kama dunia inasherehekea nawe! Nuru inakuingia kwa nguvu, rangi zinacheza mbele ya macho yako kama siku ya tamasha kubwa. Kila kitu kinakuwa kipya kana kwamba kimeumbwa kwa ajili yako tu.
Ni hisia inayoweza kukufanya ulie na kucheka kwa wakati mmoja, kwa sababu safari ya kutoka gizani hadi kwenye mwanga ni tukio la kushangaza. Huo ndio uzuri wa kuona baada ya kutokuona kwa muda mrefu. Ni furaha isiyoelezeka kwa urahisi, na shukrani isiyo na kikomo.
Mimi sio wa kwanza kupitia mabadiliko haya makubwa. Katika Biblia kuna habari ya mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa. Mtu huyo aliponywa na Yesu kwa muujiza. Kwa furaha na mshangao, akasema: “Nilikuwa kipofu, sasa ninaona” (Yohana 9:25). Tofauti yake na mimi ni kwamba, yeye alikuwa kipofu wa kimwili, lakini mimi nilikuwa kipofu wa rohoni, fikra zangu zilikuwa zimepofushwa na ibilisi.
Kwa sababu ya upofu wa rohoni, matusi, chuki, kusema uongo, vyote hivyo sikuona ubaya wake. Maisha ya uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo sikuona hatari yake, hadi Yesu aliponiondolea upofu wa rohoni. Hiyo ilitokea miaka kadhaa iliyopita, katika mkutano wa Injili. Siku hiyo Yesu alinigusa, akanipa macho mapya ya rohoni. Sasa ninaona nuru yake ang’avu. Natambua waziwazi dhambi ni nini na mshahara wa dhambi naujua. Hiyo ndiyo hali anayokutana nayo kila mtu aliyekuwa dhambini kisha akaokoka.
Yesu alipoingia ndani ya moyo wangu alileta badiliko halisi la maisha. Ukinikasirisha, mimi nacheka tu. Ukinichukia, mimi nakupenda tu. Ukinidharau, mimi nakuhurumia. Ukinitupia mawe, mimi namshukuru Yesu. Haya ndiyo maisha ya kila mtu aliyeokolewa kwelikweli na Yesu.
Asante Yesu kwa kuniokoa. Asante Yesu kwa kuwa sasa ninao uhakika wa kuingia mbinguni.
Ukipoteza uono, yaani macho yako yasipoweza kuona kwa muda mrefu, kisha ghafla ukaanza kuona tena, ni kama dunia inasherehekea nawe! Nuru inakuingia kwa nguvu, rangi zinacheza mbele ya macho yako kama siku ya tamasha kubwa. Kila kitu kinakuwa kipya kana kwamba kimeumbwa kwa ajili yako tu.
Ni hisia inayoweza kukufanya ulie na kucheka kwa wakati mmoja, kwa sababu safari ya kutoka gizani hadi kwenye mwanga ni tukio la kushangaza. Huo ndio uzuri wa kuona baada ya kutokuona kwa muda mrefu. Ni furaha isiyoelezeka kwa urahisi, na shukrani isiyo na kikomo.
Mimi sio wa kwanza kupitia mabadiliko haya makubwa. Katika Biblia kuna habari ya mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa. Mtu huyo aliponywa na Yesu kwa muujiza. Kwa furaha na mshangao, akasema: “Nilikuwa kipofu, sasa ninaona” (Yohana 9:25). Tofauti yake na mimi ni kwamba, yeye alikuwa kipofu wa kimwili, lakini mimi nilikuwa kipofu wa rohoni, fikra zangu zilikuwa zimepofushwa na ibilisi.
Kwa sababu ya upofu wa rohoni, matusi, chuki, kusema uongo, vyote hivyo sikuona ubaya wake. Maisha ya uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo sikuona hatari yake, hadi Yesu aliponiondolea upofu wa rohoni. Hiyo ilitokea miaka kadhaa iliyopita, katika mkutano wa Injili. Siku hiyo Yesu alinigusa, akanipa macho mapya ya rohoni. Sasa ninaona nuru yake ang’avu. Natambua waziwazi dhambi ni nini na mshahara wa dhambi naujua. Hiyo ndiyo hali anayokutana nayo kila mtu aliyekuwa dhambini kisha akaokoka.
Yesu alipoingia ndani ya moyo wangu alileta badiliko halisi la maisha. Ukinikasirisha, mimi nacheka tu. Ukinichukia, mimi nakupenda tu. Ukinidharau, mimi nakuhurumia. Ukinitupia mawe, mimi namshukuru Yesu. Haya ndiyo maisha ya kila mtu aliyeokolewa kwelikweli na Yesu.
Asante Yesu kwa kuniokoa. Asante Yesu kwa kuwa sasa ninao uhakika wa kuingia mbinguni.