Je, Unamwona Yesu Kama Nani Kwako?

Je, Unamwona Yesu Kama Nani Kwako?

Samson Ernest

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
1,217
Reaction score
1,705
Mk 8:27 SUV
[27] Akatoka Yesu na wanafunzi wake, wakaenda kwenye vijiji vya Kaisaria-Filipi; na njiani akawauliza wanafunzi wake, akasema, Watu huninena mimi kuwa ni nani?

Swali hili waliloulizwa wanafunzi linatuhusu mimi na wewe leo, kwa sababu tunaweza tukawa tunasema tumeokoka ila tukawa na mtazamo tofauti juu ya Yesu.

Kila mwamini akiulizwa swali hili anaweza akawa na majibu yake tofauti, tena majibu mengine yanaweza kukushangaza kabisa.

Utashangaa kile kitajibiwa na mtu ambaye unamwamini ni muumini wa siku, alafu akitoa majibu ambayo hukutegemea.

Sijui unamwonaje Yesu au unaufahamu kiasi gani juu ya Yesu, vile unamwona Yesu ndivyo mambo yatakavyotokea kwako.

Ukiwa unaufahamu kwa kiasi kidogo juu ya Yesu, atakuwa kwa kiwango kile kile katika maisha yako.

Ukimwona Yesu hawezi kukusaidia jambo fulani, ndivyo itakavyokuwa kwako, hawezi kufanya nje na imani yako.

Ikiwa umwona Yesu kwa viwango vya juu, ndivyo itakavyokuwa kwako, vipo vitu vitakuwa kwako vya viwango vya juu.

Eneo tunalomweka Yesu ndivyo itakavyokuwa katika maisha yetu, jambo ambalo linaweza likawa jema au lenye upungufu fulani.

Unaweza kuona ni jinsi gani ilivyo muhimu kukazana kuongeza kiwango chako cha imani yako, ili uanze kumwona Yesu katika ukubwa.

Soma biblia kwa mtazamo mpana, usisome kwa ajili ya kuhubiri au kufundisha au kumshinda shetani tu, soma kwa malengo mapema ya ufalme wa Mungu.

Maisha yako yanaweza kubadilishwa moja kwa moja na Yesu, watu wanaokufahamu wakaachwa midomo wazi kwa yale wanayoyaona yakiendelea kwenye maisha yako.

Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana
 
Namwona kama nabii na mitume wengine wa kabla na baada yake, si mwana wa Mungu na wala si Mungu kama yeye mwenyewe asemavyo.
 
Ilikuwa vigumu kwa mitume kumjua Yesu ni nani kwa sababu wakati huo walipoulizwa, walikuwa hawajaambiwa, na ilitakiwa wajibu kwa kutegemea yale matendo waliyokuwa wakiyashuhudia, au kwa kuangaziwa na Roho Mtakatifu. Lakini baada ya pale, Mara kadhaa Yesu alieleza kwa uwazi kuwa Yeye ni nani. Yafuatayo ni majibu halisia yenye chanzo cha matamko yake mwenyewe:
1. Yesu ni ufufuo na uzima (ref. ndimi ndiye huo ufufuo na uzima)

2. Yesu ni njia ya kufika kwa Baba (ref. mtu hafiki kwa Baba ila kwa kupitia mimi)

3. Yesu ni ushirika wa Mungu (ref. Mimi ni ndani ya Baba na Baba yu ndani yangu, ukiniona mimi umemwona Baba)

4. Yesu ni mkombozi wa wanadamu wote (ref. sikuja kuuhukumu Ulimwengu bali kuukomboa)

5. Yesu ni chanzo cha uzima wa milele (ref. Nimepewa mamlaka yote Duniani na mbinguni, aniaminiye mimi ana uzima wa milele).

6. Yesu ni Agano la milele kati ya wanadamu na Mungu (ref. Huu ndio mwili wangu, mwili wa Agano jipya la milele)

7. Yesu ni nafsi kamili ya Mungu (ref. Unitukuze mimi pamoja nawe katika utukufu ule niliokuwa nao kabla Ulimwengu haujakuwako; nendeni Ulimwenguni kote mkawabatize kwa jina la BABA, MWANA na ROHO MTAKATIFU).

8. Yesu ni nafsi pekee kwaajili ya wokovu wa mwanadamu (ref. hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo, ila Yesu Kristo).

JUMUISHO:
Yesu Kristo, ni nafsi ya Mungu kwaajili ya wokovu wa mwanadamu. Ndiyo nafsi pekee ambayo katika mwili iliishi na wanadamu, ikafundisha kwa mamlaka ya kimungu (nimepewa mamlaka yote Duniani na mbinguni), ikatufunulia siri za ufalme wa mbingu (ref. Hakuna amjuaye Baba isipokuwa Mwana).
 
Back
Top Bottom