Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
TAKRIBANI wiki tatu nilikuwa nafuatilia mkasa wa dada Easter Deo. Hakika mkasa huo ulinigusa sana nami nikashawishika kusimulia yaliyonikuta katika maisha yangu.
Naamini kuwa kuna baadhi ya watu hawakuamini mkasa wa dada Easter kama ni wa kweli ama ulikuwa ni wa kutunga.
Ninachoamini ni hiki, uchungu wa maumivu ya ugonjwa ama majeraha yoyote huwa anayasikia mhusika lakini si mtu mwingine. Kwa jina naitwa Steven Frances Soso, ni mwenyeji wa Morogoro Wilaya ya Ifakara.
Nimezaliwa katika familia ya wacha Mungu. Baba yangu mzee Frances Kasela Soso ni Mchungaji wa Kanisa la Living Word Pentecost lililopo Ifakara.
Nilikuwa na hali ya kuwa naumwa mara kwa mara. Pamoja na kwamba baba yangu ni mchungaji, binafsi sikukubaliana na masuala ya ulokole kwani niliona kama ni shida kwangu.
Baba yangu alikuwa anafanya taratibu za kuniandaa kuwa mchungaji hapo baadaye. Alikuwa karibu na mimi na alikuwa ananielekeza mambo mbalimbali yanayohusiana na uchungaji.
Kitendo hicho nilikiona kama mzigo kwangu nikaamua kuondoka na kwenda kupanga chumba Ifakara mjini.
Nikiwa hapo, nilimpata rafiki yangu ambaye sitapenda kutaja jina lake. Rafiki huyo alikuwa msaada mkubwa kwangu.
Tatizo la kuugua mara kwa mara lilionekana kuwa la kawaida. Nilikuwa naumwa kichwa, hali iliyokuwa inanifanya niwe nalia kila kukicha kutokana na maumivu makali niliyokuwa nayapata.
Kila nikienda kupima madaktari hawakuona kitu chochote.
Hali hiyo ilinitesa kwa muda mrefu. Rafiki yangu alinishawishi kwenda kwa waganga wa jadi kwa ajili ya kupata tiba zaidi.
Nilipofika kwa mganga huyo sehemu inayoitwa Ipangalala, alitukaribisha kwa furaha.
Alipoanza matibabu aliniambia kuwa, sisumbuliwi na kitu chochote bali nina mapepo ya kiganga hivyo nalitakiwa nifuate masharti yote ili niwe salama.
Nilianza kupata matibabu kwa ajili ya kuondoa mapepo hayo.
Niliambiwa nikanunue ubani ili niweke ndani ya chumba nilichofikia kwa mganga huyo. Hali yangu niliona kuwa na mabadiliko makubwa.
Itaendelea
Naamini kuwa kuna baadhi ya watu hawakuamini mkasa wa dada Easter kama ni wa kweli ama ulikuwa ni wa kutunga.
Ninachoamini ni hiki, uchungu wa maumivu ya ugonjwa ama majeraha yoyote huwa anayasikia mhusika lakini si mtu mwingine. Kwa jina naitwa Steven Frances Soso, ni mwenyeji wa Morogoro Wilaya ya Ifakara.
Nimezaliwa katika familia ya wacha Mungu. Baba yangu mzee Frances Kasela Soso ni Mchungaji wa Kanisa la Living Word Pentecost lililopo Ifakara.
Nilikuwa na hali ya kuwa naumwa mara kwa mara. Pamoja na kwamba baba yangu ni mchungaji, binafsi sikukubaliana na masuala ya ulokole kwani niliona kama ni shida kwangu.
Baba yangu alikuwa anafanya taratibu za kuniandaa kuwa mchungaji hapo baadaye. Alikuwa karibu na mimi na alikuwa ananielekeza mambo mbalimbali yanayohusiana na uchungaji.
Kitendo hicho nilikiona kama mzigo kwangu nikaamua kuondoka na kwenda kupanga chumba Ifakara mjini.
Nikiwa hapo, nilimpata rafiki yangu ambaye sitapenda kutaja jina lake. Rafiki huyo alikuwa msaada mkubwa kwangu.
Tatizo la kuugua mara kwa mara lilionekana kuwa la kawaida. Nilikuwa naumwa kichwa, hali iliyokuwa inanifanya niwe nalia kila kukicha kutokana na maumivu makali niliyokuwa nayapata.
Kila nikienda kupima madaktari hawakuona kitu chochote.
Hali hiyo ilinitesa kwa muda mrefu. Rafiki yangu alinishawishi kwenda kwa waganga wa jadi kwa ajili ya kupata tiba zaidi.
Nilipofika kwa mganga huyo sehemu inayoitwa Ipangalala, alitukaribisha kwa furaha.
Alipoanza matibabu aliniambia kuwa, sisumbuliwi na kitu chochote bali nina mapepo ya kiganga hivyo nalitakiwa nifuate masharti yote ili niwe salama.
Nilianza kupata matibabu kwa ajili ya kuondoa mapepo hayo.
Niliambiwa nikanunue ubani ili niweke ndani ya chumba nilichofikia kwa mganga huyo. Hali yangu niliona kuwa na mabadiliko makubwa.
Itaendelea