Ni kweli. Huyu mama tunaweza kuwa tunamuonea kwa sababu amaezungukwa na mapapa hata yeye anayaogopa. Huyu alikuwa anafiti huko huko Zanzibar.Nimewahi kuishi Zanzibar nikiwa mdogo huko na pia kufanya nao kazi sehemu mbalimbali. Hawa watu ni wapole, wasio na makuu, wasio na majivuno!
Shida unakuja ni hawa ndugu zetu wa huku bara! Sio wa kweli kwenye moja wao wanasema ni mbili! kwenye uongo, wanasema ni ukweli, kwenye ukweli wanasema ni uongo!.
Huyu nae ni Binadamu kama tulivyo sisi wengine, mapungufu nae anayo. Chukulia mtu kama Lukas Mwashambwa kwenye mada yake Moja, Anadai Raisi asiwe na ukomo! Maana yake katiba Raisi aivunje, unategemea Nini kwa ushauri wa watu kama Hawa na mwenzake tlaahtlaah?!
Ukweli au jambo la uongo,lisemwe kwa staha bila kificho Wala fitina.
Ahsanteni sana.
Wazanzibar hawana kona kona. Tazama walivyopambana mpaka wakapata bendera yao na mwisho wa siku wakabadilisha katiba na kuruhusu serikali ya umoja wa kitaifa ili tu kuleta amani.
Shida ni huku bara wasaidizi wake wanafiki, wabinafsi wanamshauri kwa kuangalia maslahi yao ilimradi tu waendelee kula keki ya taifa na familia zao.
Tujiulize, mbona CCM ya Zanzibar walikaa chini wakaweka mambo yao sawa na upinzani? Iweje CCM ya bara haitaki maridhiano na wapinzani wakati chama ni kile kile? Hapo ndipo utagundua utofauti wa Wazanzibar na Watanganyika katika misimamo!