chongchung
JF-Expert Member
- Jun 23, 2013
- 14,297
- 45,087
Hatuwezi kuzungumzia plan za 2013 mwaka huu hivi unachukuaje statistics za sensa ya 2002 na kuacha ya 2012 em kuwa msomi kidogo aise.Hivi wewe umeingia kwenye hiyo web au unaongea tu...?! Kwenye hiyo web kuna Halmashauri zote Tanzania na kiasi kilichokukusanywa katika Vyanzo vya Halmashauri yaani Own Source Revenue zipo data mwisho mpaka mwakaa 2012/2013
kuna sehemu unaingiza mwaka unachagua na Halmashauri unachagua unataka halmashauri ipi, katika orodha kuna Arusha City Council, kuna Mwanza City Council pia kuna Ilemela Municipal Council...
Sasa wewe unabisha hata hujaingia, yaani unapinga vitu visivyokuwepo... labda nikuulize yaani unaweza ukakadiria kiaje kwamba tumepata kitu fulani ilhali mnakusanya...?! Labda nikuulize zile kodi za majengo halmashauri wanazokusanya kodi za huduma ambapo huwa ni 0.3% ya sales turnover wanakadiriaje...?! Kodi ya hotel ambayo huwa ni 10% ya mauzo halmashauri wanakadiriaje kama wamekusanya...?! Ushuru wa mabango huwa wanakadiaria kiaje kama imekusanywa...?! Ushuru wa masoko na minada, ushuru wa maua, ushuru wa mazao, ada za leseni za biashara vyanzo vipo vingi halmashauri wanaweza wakakadiariaje kama wamekusanya...?!
sasa huwa kuna kitu kimoja huwa wanapewa target wakusanye kiasi fulani kulingana na halmsahauri husika na vyanzo vyake vya ndani katika mwaka sasa wanaweza wakavuka malengo au wakakusanya kwa asilimia fulani kubwa...
Kama unasema makusanyo yanakadiriwa basi na TRA wanakadiria pia, sidhani kama hata kama unajua miundo ya halmashauri unaweza ukawa unaongea lakini hujui unachoongea...
Unajua kwamba kuna maeneo ya halmashauri ya wilaya ya Arusha yalichukuliwa na halmashauri ya manispaa ya Arusha ili kuweza kuwezesha manispaa ya Arusha kuwa jiji na walipata hadhi kuna kata kama tatu zilichukuliwa mfano ni kata ya Moshono...
Mwanza
Madiwani wapitisha bajeti
Baraza la madiwani la Halmashauri ya jiji la
MWANZA limepitisha makadirio ya mapato
na matumizi ya shilingi Bilioni 87 katika
mwaka wa fedha wa 2016/2017
Madiwani wapitisha bajeti - TBC.go.tz
Arusha
bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka
wa fedha 2016/2017 ya Halimasahauri ya
jiji la Arusha hatimaye jambo hilo
limewekwa hadharani ambapo kiasi cha
shilingi bilioni 109 zimepitishwa na baraza
la madiwani kwa ajili ya kuanza kutekeleza
mipango ya kimaendeleo.
CHAGUO LA MSOMI | UNLIMITED NEWS
Hizi ndio current situations.