Nilicho-experience katika safari za treni za SGR hadi sasa

Nilicho-experience katika safari za treni za SGR hadi sasa

Twin Tower

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2023
Posts
4,903
Reaction score
7,193
Nimesafiri na aina zote za train tokea ile ya enzi za mkoloni aka gari moshi hadi hii SGR ile express na Ordinary.

Wastani wa safar zangu kwa sasa ni kama mara 24 nikipanda madaraja ya uchumi (economy) na biashara (Business). Royal class ipo njian pia.

Naipongeza serikali kwa huu mradi, hakika umefanya safari kuwa rahisi kiasi kikubwa sio kwa wakazi wa mikoa ya Dodoma, Moro na Dar. Hata wale wa mikoa kama Iringa, singida,Tabora, Mwanza. Hapa unaanzia safar yako Dodoma.

Upatikanaji wa tiketi.
Mfumo wa tiketi umekuwa bora sana, mara moja tu nilipata changamoto za malipo kwa kutumia benk na simu, lakini kupitia huduma kwa wateja nilihudumiwa vizuri.

Ushauri kwenye hili eneo, nikuangalia uwezekano wa mtu

1. Kukata open ticket/tikit ya wazi aweze kuitumia ama ndani ya mwezi lkn afanye confirmation 48/24hrs kabla ya safari.

2. Kukata tiketi ambayo unaweza kubadili taarifa za msafiri. Hii iwe muda wowote, ilimradi wakati kuchek in kuwe na taarifa sahihi.

Huduma ndani ya treni na vituo.
Hili ni moja ya eneo ambalo Kadogosa na timu yake wanapaswa kulisisitiza. Sio mbaya sana, lkn bado hairidhishi.

1. Sehemu za kulumzikia kukosa viti vya kutosha huku msisitizo watu wafike 2hrs kabla ya muda wa kuondoka. Mnawakawalisha wapi?

2. Ukaguzi wa tiketi kufanywa na maafisa wachache.

3.vizuizi kwa abiria wanaoshuka,rahisheni kuwe na maeneo yasiyo na vizuizi kwa wanaoshuka.

4. Usimamizi na huduma ndani ya mabehewa. Watqnzania bado wanajitafuta sana, wanahitaji usimamizi na uongozaji wa matumizi ya vifaa. Msiwe wavivu nyinyi wahudumu ndani ya train.

5. Wekeni wazi mtu akikata business/royal anapata faida zipi.

Miundombinu.
Mpaka sasa hongereni chuma bado mpya, ingawa mfanye maboresho kidogo kuna vitu vimeharibika.

Ile barabara ya kwenda stesheni ya morogoro ni uchafu na inaharibu hadhi. Ni aibu hadi sasa haipo kwenye viwango.

Nitaendelea.
 
Nimesafir na aina zote za train tokea ile ya enzi za mkoloni aka gari moshi hadi hii SGR ile express na Ordinary.

Wastani wa safar zangu kwa sasa ni kama mara 24 nikipanda madaraja ya uchumi (economy) na biashara (Business). Royal class ipo njian pia.

Naipongeza serikali kwa huu mradi, hakika umefanya safari kuwa rahisi kiasi kikubwa sio kwa wakazi wa mikoa ya Dodoma, Moro na Dar. Hata wale wa mikoa kama Iringa, singida,Tabora, Mwanza. Hapa unaanzia safar yako Dodoma.

Upatikanaji wa tiketi.
Mfumo wa tiketi umekuwa bora sana, mara moja tu nilipata changamoto za malipo kwa kutumia benk na simu, lakini kupitia huduma kwa wateja nilihudumiwa vizuri.

Ushauri kwenye hili eneo, nikuangalia uwezekano wa mtu
1. Kukata open ticket/tikit ya wazi aweze kuitumia ama ndani ya mwezi lkn afanye confirmation 48/24hrs kabla ya safari.
2. Kukata tiketi ambayo unaweza kubadili taarifa za msafiri. Hii iwe muda wowote, ilimradi wakati kuchek in kuwe na taarifa sahihi.

Huduma ndani ya treni na vituo.
Hili ni moja ya eneo ambalo Kadogosa na timu yake wanapaswa kulisisitiza. Sio mbaya sana, lkn bado hairidhishi.
1. Sehemu za kulumzikia kukosa viti vya kutosha huku msisitizo watu wafike 2hrs kabla ya muda wa kuondoka. Mnawakawalisha wapi?
2. Ukaguzi wa tiketi kufanywa na maafisa wachache.
3.vizuizi kwa abiria wanaoshuka,rahisheni kuwe na maeneo yasiyo na vizuizi kwa wanaoshuka.
4. Usimamizi na huduma ndani ya mabehewa. Watqnzania bado wanajitafuta sana, wanahitaji usimamizi na uongozaji wa matumizi ya vifaa. Msiwe wavivu nyinyi wahudumu ndani ya train.
5. Wekeni wazi mtu akikata business/royal anapata faida zipi.

Miundombinu.
Mpaka sasa hongereni chuma bado mpya, ingawa mfanye maboresho kidogo kuna vitu vimeharibika.

Ile barabara ya kwenda stesheni ya morogoro ni uchafu na inaharibu hadhi. Ni aibu hadi sasa haipo kwenye viwango.

Nitaendelea.
Sawa
 
Ni uwekezaji wa hali juu sana ndo maana akina kikwete na mkapa hawakuweza

Bila Magufuri tusingepata hii kitu

Abalikiwe Magufuri
 
Eneo lingine katika tiketi ambalo ni wizi kwa wananchi, kimsingi ni kama tunakopi tu baadhi ya mambo.

Ukitaka kubadilisha tiketi gharama unayotozwa zaidi ni kama 30% ama 15k. (Kama sijakosea, ni muda kidogo wa hili tukio)

Nakumbuka nilikuwa na tiketi la daraja la biashara express, dom kwenda moro. Ratiba zikanibana nikaomba nibadilishiwe muda wa kusafiri niondoke na ordinary. Wakanitaka nilipe hela ya zaidi.
Hoja ikawa ninatiket ambayo ni ghali kuliko nayoomba kutaka kuitumia. Iweje tena nilipie gharama zaidi? Nikajaribu kuwapa changamoto watoa huduma wakaishia kusema ni utaratibu upo hivyo.

Muda wa safari ulikuwa bado kwa zaidi ya saa 12, na ordinary ilikuwa na nafasi.

Hili eneo wanapaswa kulitazama kibiashara kuliko kukomoa wasafiri.


Kwani kuna ubaya gani mtu alikuwa na tiket ya juu akarushusiwa kwenda na train rahis, na kuiacha wazi nafasi ya awali?
Ama akalazimika kuongeza fedha kama atatumia train ama daraja la juu kutoka tiketi yake ya awali.

Maana vyote hutokea kutegemea nafasi.
 
Back
Top Bottom