Niko njia panda ushaurii wenu tafadhari

Niko njia panda ushaurii wenu tafadhari

Kwa hiyo ukirudi nyumbani unataka kuolewa tena? ni bora ukafanya maamuzi ya busara kwa kuamua kubadili dini na kufunga ndoa, zaidi ya hapo sijui unachotaka, acha kumsumbua mwenzio wakati mmetoka nae mbali mpaka mmefikia kuzaa!
 
Ushauri mzuri utaupata kwa wazazi wako, ipo siku utanikumbuka usipozingatia ushauri wa wazazi


Hivi hao wazazi wake ndio pia walimpa ushauri wa atafute mwanaume wa kufanya majukumu yao ya kumsomesha pia!?
 
ungekuwa unapenda dini usingezini mpaka kuzaa..pili usingewekwa kinyumba. kwahiyo kwanza tubu sana halafu kama jamaa anakupenda muombe abadili dini ili mfunge ndoa ila wewe usibadili dini wala msioane kila mtu na dini yake. plz fuata ushauri huu
 
Hayo uloyaeleza hapa ndo mazingira ya dini? kuishi na mtu mkazini mpaka mkazaa mtoto? ndo kupenda dini yako hivyo? kama umelelewa katika mzingira ya dini ni kwa nn usijue kuwa unaoyafanya nikinyume na misingi ya dini?

Nikuambie tu mtu aliyelelewa katika mazingra ya dini hathubutu hata kufkiria kuyafanya hayo uloyafanya wewe. Huipedi dini yako hata alama na ndo maana umefikia hatua uliyopo sasa. Kama unaipenda kweli dini yako fanya tauba yakweli, ujute na uazimie kutokurejea makosa uliyoyatenda.

Nikiku-quote, ujue umeleta ujumbe sahihi 100%isiyo na shaka. NAZIPENDA SANA FIKRA SAHIHI KAMA HII YAKO.
Endelea kujitokeza humu...nami niendelee kuchangamka. Asent.
 
Aaah, miss chaga! Amini kama unaishi kwa hii dunia, na maisha yako ni mteremko hata hujakutana na kindumbwe ndumbwe, basii bado songombingo lako liko mbele lina kusubiri. Ukichelewa sana kupata vikwazo vya maisha ungali chipukizi.....ndio matokeo ya ufooo-saro, ndo kujinyonga, ndo kunywa sumu, ndo kuuwa mtu...ndio kwenda jela na kusahaulika. KUTOKANA NA VIKWAZO NA VISA vya maisha mchanganyikooo, ndo niko imara hivi sasa. SINA PRESHA.

Basi tu humu kwa sasa nazipekua post za wakuu na kuchangia kama nikivutiwa kufanya ivo. Nikiweka post za visa nilivokutana navyo...vya kimapenz...very interesting, utasema "toba!"...yamenikuta mzee mwenzangu sina changu, cjui nikae chini nilie...kwa visa visa!

Post zangu nikizitoa uzisome....na hakika zitakutafakarisha, na mwisho utasema oouph! Ee Mungu weeeh! HATA IVO NINA IMANI MOYO WAKO NI SUPPER. Xo, hakitaharibika kitu. Stay tuned..next week nitadondosha post moja tutafakari pamoja. Kama vp nitaiweka rasmi hiyo niliyo ichomekea humu...sababu ya kufanana kwake. Asent miss chaga!

Thank you for your comment,,
 
ungekuwa unapenda dini usingezini mpaka kuzaa..pili usingewekwa kinyumba. kwahiyo kwanza tubu sana halafu kama jamaa anakupenda muombe abadili dini ili mfunge ndoa ila wewe usibadili dini wala msioane kila mtu na dini yake. plz fuata ushauri huu

WANAUME HATUBADILI DINI. Ukitaka mwanaume abadili dini basi mshauri huyo mdada auvae uanaume. KUMBE MPO WENGI WA IVVO EEEH!!!
 
kama jamaa anakupenda muombe abadili dini ili mfunge ndoa ila wewe usibadili dini wala msioane kila mtu na dini yake. plz fuata ushauri huu

Hapo ndio palikua pananishangaza na panaendelea kunishangaza.
 
WANAUME HATUBADILI DINI. Ukitaka mwanaume abadili dini basi mshauri huyo mdada auvae uanaume. KUMBE MPO WENGI WA IVVO EEEH!!!

Dini zinatofautiana na mafundisho ni tofauti pia..yeye niliemweleza ameshanielewa kwasababu amesema ni dini gani kwahiyo nimemshauri kutokana na dini yake inavyosema.
 
Kosa Ulilofanya Kuanzia Mwanzo Ni Kukubali Kuishi Naye Na Kuzaa Naye.Hayo Yalimfanya Mwenzio Aamini Umeshakubali Kuwa Mke Wake Na Muda Utakapofika Utakuwa Tayari Madhabahuni Kudhibitisha Hilo.Sasa Leo Anakueleza Unaanza Kuleta Sababu Zisizo Na Mashiko As If Ulikuwa Haujui Kama Ni Mkristo.Kwa Nini Hukukataa Kuanzia Mwanzo? Amekusomesha,kakuhudumia Kafanya Yote Hayo Ulikaa Kimya Leo Mwiba Umekuwa Mchungu? Hujui Kama Mwanamke Anafata Dini Ya Mwenza Wake?
 
Kingine Ambacho Nakiona Hapa Ni Kuwa Hata Tabia Yake Ya Kuwa Na Michepuko Wewe Haikuumizi Unaona Ni Kawaida Sana Kwa Kuwa Unampenda.Sasa Kama Umeweza Kuvumilia Hilo La Michepuko Ambalo Ni Hatari Zaidi Kuliko Hilo La Dini Kwa Nini Unashindwa Kubadilisha Dini Ili Kumtendea Haki Mtoto Wako?
 
Dini zinatofautiana na mafundisho ni tofauti pia..yeye niliemweleza ameshanielewa kwasababu amesema ni dini gani kwahiyo nimemshauri kutokana na dini yake inavyosema.

Huyu yey ni mpagani...je umemshauri kwa usahihi??? Kama umeamini kuwa ni muislam...ni danganya toto...waislam hawaishi maisha ya ivo. Ila kama anapenda uislam sasa, ndo aanze kwenda madrassa. Na kama anapenda ukristo...akaanze mafundisho sasa...kiongozi wake ni baba mtoto.
 
dada angalia pm nimekutumia ushuri mzuri uzingatie kubwa zaidi nakusisitizia watii wazazi wako
 
Kati yenu hakna mkristo wala muislam wa kweli kwali kila mmoja wenu tayari keshavunja misingi ya imani yake.(wewe sabudi umezaa kabla ya ndoa,mwenzi wako halikadhali,kuhusu zinaa wote mmefanya)
Sasa cha kukushauri kama unaipenda dini yako na unampenda mzazi mwenzako;chagua kinachougusa moyo wako zaidi."mbingu au nchi"baada ya hapo mtafte MUNGU kwelikweli.
 
Back
Top Bottom