Salam kwenu wana JF ,
Leo nina tatizo ambalo naomba msaada wenu kimaombi na kimawazo pia.
Nimeolewa miaka 7 iliyopita mwenyezi mungu katujaalia twins wa kike na wa kiume.
Muda wote wa mahusiano yetu tulikuwa tunakaa mbali mbali sababu ya mazingiraya kazi , lakini kila baada ya miezi miwili au mwezi tulikuwa tunaonana na kutembelea familia zetu.
Tatizo langu lilianza miaka mitatu baada ya ndoa yetu , mwanzo sikuwahi kujua kabisa mwenzangu ana imani kubwa sana ya ushirikina ambayo ni chimbuko na imani katika familia yao,tunaenda kanisani pia kusali pamoja kama familia nyumbani.
Ghafla nikaanza kuona vitu vya ajabu ajabu ndani ambayo vilikuwa vimeandikwa maneno ya nisiyojua lugha yake ambavyo kumbe alikuwa anaweka kwenye maji na maandishi yakiyeyuka anakunywa yale maji.
Pia anatembea na vitu visivyojulikana kwenye wallet yake .
Pia malalamiko kuwa anarogwa na baadhi ya ndugu na marafiki ili asifanikiwe yakaanza .
Story za ajabu ajabu kama kuna ndugu yake alifariki miaka sita iliyopita eti alirogwa na mke wake na sasa amepatika kuna mganga alimsaidia kurudi katika hali ya kawaida.
Anasema kijijini kwao bila kujikinga huwezi kuishi maana 85% wote wanajihusisha na uchawi.
Kilichoniogopesha sasa anasema anataka watoto waende kijijini ili wakajue mila za kwao.
Nimekuwa nafunga na kuiombea familia yangu ili mwenyezi mungu aweze kumfungua hiki kifungo,ukimsema kuhusu haya mambo yake ananuna na kuondoka nyumbani.
Sasa nimeanza hali ya kumuogopa mme wangu naweza kushituka usiku na kubaki namtizama tu siamaini matendo yake na hizo story zake. Pia ni msomi wa hali ya juu
Nimeongea na familia yangu wananiambia niendelee kumuombea ,
Nisaidieni mwenzenu
Leo nina tatizo ambalo naomba msaada wenu kimaombi na kimawazo pia.
Nimeolewa miaka 7 iliyopita mwenyezi mungu katujaalia twins wa kike na wa kiume.
Muda wote wa mahusiano yetu tulikuwa tunakaa mbali mbali sababu ya mazingiraya kazi , lakini kila baada ya miezi miwili au mwezi tulikuwa tunaonana na kutembelea familia zetu.
Tatizo langu lilianza miaka mitatu baada ya ndoa yetu , mwanzo sikuwahi kujua kabisa mwenzangu ana imani kubwa sana ya ushirikina ambayo ni chimbuko na imani katika familia yao,tunaenda kanisani pia kusali pamoja kama familia nyumbani.
Ghafla nikaanza kuona vitu vya ajabu ajabu ndani ambayo vilikuwa vimeandikwa maneno ya nisiyojua lugha yake ambavyo kumbe alikuwa anaweka kwenye maji na maandishi yakiyeyuka anakunywa yale maji.
Pia anatembea na vitu visivyojulikana kwenye wallet yake .
Pia malalamiko kuwa anarogwa na baadhi ya ndugu na marafiki ili asifanikiwe yakaanza .
Story za ajabu ajabu kama kuna ndugu yake alifariki miaka sita iliyopita eti alirogwa na mke wake na sasa amepatika kuna mganga alimsaidia kurudi katika hali ya kawaida.
Anasema kijijini kwao bila kujikinga huwezi kuishi maana 85% wote wanajihusisha na uchawi.
Kilichoniogopesha sasa anasema anataka watoto waende kijijini ili wakajue mila za kwao.
Nimekuwa nafunga na kuiombea familia yangu ili mwenyezi mungu aweze kumfungua hiki kifungo,ukimsema kuhusu haya mambo yake ananuna na kuondoka nyumbani.
Sasa nimeanza hali ya kumuogopa mme wangu naweza kushituka usiku na kubaki namtizama tu siamaini matendo yake na hizo story zake. Pia ni msomi wa hali ya juu
Nimeongea na familia yangu wananiambia niendelee kumuombea ,
Nisaidieni mwenzenu