Niko hai sababu ya mtoto wangu

Niko hai sababu ya mtoto wangu

moonlightj12

Member
Joined
Dec 6, 2022
Posts
33
Reaction score
90
Sio mtaalamu sana wa kiingereza, lakini kama nipo hai sasa hivi ni kwa sababu naona hamna mtu atakaelea huyu kiumbe niliemleta Duniani.

Kwa huzuni, majukumu na uchungu niliyobeba ningeweza kumuomba Mungu nife hata leo nipumzike, but ni vile nina jukum la kulea na kumlinda huyu kijana wangu. Basi niseme tu Mungu tusaidie, Mungu tukumbuke.

Nyie mi nimechoka kuwa jasiri.
 
Shida nini mama la mama?
Semelea yaliyo moyoni wadau wakusaidie,ukiyatoa ya moyoni nafkiri ni moja ya tiba nzuri kwa kuanzia

Unaonekana una tatizo/matatizo muda mrefu
 
Wewe ni thamani,
Hapa duniani hujaja kupita Ili mradi,
Umekuja kwa malengo,
Na lazima uyatimize,
Endelea kujitamkia mazuri,
Maana kinywa chako kina nguvu.
 
Jamani pole sana. Mungu azidi kukumbusha kuwa Kuna mtu anakuona una thamani. Kama unahisi kukata tamaa basi basi jikumbushe wewe ni Shujaa na umeweza kukaa na kiumbe na kukileta duniani. Usikate tamaa.

Kama umechoka kuwa jasiri Kwa ajili Yako. Basi kuwa jasiri Kwa ajili ya mwanao.

Sali Kwa imani, omba amani ya nafsi. Omba mwanzo mzuri. Mungu wetu ni mwema sana
 
Shida nini mama la mama?
Semelea yaliyo moyoni wadau wakusaidie,ukiyatoa ya moyoni nafkiri ni moja ya tiba nzuri kwa kuanzia

Unaonekana una tatizo/matatizo muda mrefu
NAKAZIA.
 
Polee sanaa Dear,
Niliwahi kumbwa na hali hiyo 9yrs ago,
Nilikua naomba nife, dunia ipasuke niingie, nipotee machoni pa watu, yaan nilikua najichukia.

Ila nashukuru mtu m1 alinishika mkono na kuwa mkombozi wangu, hadi leo hii nipo hapa nikiwa na ujasiri, ari, nguvu, kasi ya kupambana na lolote linalokuja mbele yangu.

Nawee naomba uondoke ktk hali hiyo, kukawe na wepesi ktk hilo.
 
Polee sanaa Dear,
Niliwahi kumbwa na hali hiyo 9yrs ago,
Nilikua naomba nife, dunia ipasuke niingie, nipotee machoni pa watu, yaan nilikua najichukia.

Ila nashukuru mtu m1 alinishika mkono na kuwa mkombozi wangu, hadi leo hii nipo hapa nikiwa na ujasiri, ari, nguvu, kasi ya kupambana na lolote linalokuja mbele yangu.

Nawee naomba uondoke ktk hali hiyo, kukawe na wepesi ktk hilo.
Mungu ashukuluwe kwa ajili Ako,
But as for me ni mwaka wa Tano and counting kila siku linazaliwa jipya kila leo afadhali ya Jana
Mungu anikumbuke uniombeage my dr Sina ata nguvu ya kuomba tena Mungu tu anihurumie
 
Kama upo hai kwaajili ya mwanao basi hutakiwi kuchoka hata iweje
Endelea kupambana kipenzi
 
Ukiwa Huna neno zuri la kusema kuhusu jambo fulani ni bora ukakaa kimya.
Tambua ya kuwa binadamu tuko tofauti, kila mtu Ana namna yake ya ku cope na changamoto zinazomkabili.
Hujui ni magumu gani anayoyapitia.
kumpa moyo na kumfariji nahis ingekuwa jambo jema zaidi
 
Pole sana
Sio wewe tu,watu wengi wanaishi si kwa sababu wanayapenda maisha au wana maisha mazuri..ni kwa sababu wana watu wanaowaangalia.
 
Ukiwa Huna neno zuri la kusema kuhusu jambo fulani ni bora ukakaa kimya.
Tambua ya kuwa binadamu tuko tofauti, kila mtu Ana namna yake ya ku cope na changamoto zinazomkabili.
Hujui ni magumu gani anayoyapitia.
kumpa moyo na kumfariji nahis ingekuwa jambo jema zaidi
Kuna watu wanazingua, sawa anapitia magumu ila sio kuishia kulaumu tu, kuna wanaopitia magumu zaidi yake na wanaendelea kupambana.

Mtu hasemi shida yake nini anataka tu kuhurumiwa na watu. Angesema tatizo tungeweza kumsaidia sasa mtu anaandika vaguely ili ahurumiwe.

Mimi mtu kama huyu naona anazingua. Angeweka wazi tatizo lake labda angepata msaada. Kwanini anaandika mafumbo?
 
Sio mtaalam sana wa kiingereza, lakini kama nipo hai saivi ni kwa sababu naona hamna mtu atakaelea huyu kiumbe niliemleta Duniani.

Kwa huzuni, majukum na uchungu niliobeba ningeweza kumuomba Mungu nife ata leo nipumzike but ni vile Nina jukum la kulea na kumlinda huyu kijana wangu
Basi niseme tu Mungu tusaidie Mungu tukumbuke

Nyie mi nimechoka kua jasiri
Nilipitia kipindi Kama chako..
Usiwakimbie watoto watakuwa machokolaa..usiwaache..pambana
 
Wewe ni thamani,
Hapa duniani hujaja kupita Ili mradi,
Umekuja kwa malengo,
Na lazima uyatimize,
Endelea kujitamkia mazuri,
Maana kinywa chako kina nguvu.
Kinywa si lazima sana... Lakini mawazo anayowaza ndio yataamua
 
Kumbuka Bata ulilowahi kula hata kama lilikuwa dogo Leo shida kidogo tu ambayo unajua haitadumu inakusumbua kichwa?Hakuna hali idumuyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom