

Sasa iko hivi, mimi ni msichana mwezi wa kumi inshwallah natimiza miaka 19 kamili. Mimi nimeanza kuangalia porn tokea niko na miaka 13. Sasa ikafika kipindi nikiangalia hizi porn za jinsia tofauti hata msisimuko nakua Sina. Nikaamia kwa gay porn. Kuna kipindi nilitaka kuacha ila nakuwa naacha kwa muda halafu najikuta nimerudi tena kulekule. Nataka kuacha kabisa lakini nashindwa. Mimi ni wa kawaida tu nina mpenzi wangu sishiriki mapenzi ya jinsia moja lakini mi hivyo niko addicted na hizo videos. Sipendi hii tabia lakini nashindwa kuacha. Nifanye nini ili niache? Naomba tu msinitukane maana nyie hamchelewagi.
Pole sana
Natamani unipe namba zako tuwasiliane kwa simu nikusaidiee taratibu,ila shida naweza kuonekana mimi ni mbabaishaji kama watu wengine.
Kiufupi hapa kwenye comment inakuwa haitoshi,lakini kwanza usiogope kabisaa.
Pili jua kwamba 95% ya mambo ya binadamu yanatawaliwa na ubongo,ubongo unaamua nini mtu afanye na nini asifanye.
Kwa hyo kwaa tatizo lako limeanzia zaidi kwenye ubongo(akili)na huko ndo kunatakiwa kutibiwe.
Huna tatizo lolote la kimwili dada yangu,tatizo lako lipo akilini zaidi.
Lakini pia kama umetumia MIAKA ZAIDI YA 6 KUJENGA TABIA FULANI,BASI USITEGEMEE KUIVUNJA YABIA HIYO NDANI YA MUDA MFUPI,INACHUKUA MUDA KUIVUNJA TABIA.
unatakiwa utumie nguvu kubwa sana kuiwacha tabia hiyo,ukiendelea itakuwa ni tatizo kubwa hasa ukipata mume wa ndoa
"NI BORA KUTUMIA NGUVU ILI UPAMBANE NA VISHAWISHI VINAYOPELEKEA KUIANZA TABIA FULANI,KULIKO KUTUMIA NGUVU KUPAMBANA NA VISHAWISHI VYA KUIWACHA TABIA FULANI.
Nguvu ya kuacha tabia inabidi iwe kubwa sana kuliko nguvu ya kuiepuka tabia ambayo haujaianza.
Asili mia 98% ya tabia ambazo tunajishauri kama tufanye au tusifanye basi mara nyingi tabia hizo tunakuja kuzijutia mbeleni na huwa tunapamvana kuziwacha.
Naomba kama sijaeleweka sehemu niulizwe...