Nasema kama ningekuwa Rais, kipaumbele changu namba Moja ingekuwa kilimo, katika utawala ningehakikisha hakuna kijana asiye na angalau hekari 2 za kilimo, nisingejenga daraja la salendar badala yake ningeagiza matrekta Kwa wingi niyagawe kwenye vijiji vya kimkakati.
Ningehakikisha Kila Kijiji kinakuwa angalau na trekta Tano ambazo watazitumia Kwa ujamaa, kulima lmapori yote yasiyo ya hifadhi na yamekaa tu ningetangaza mtu yeyote anaetaka kulima apewe Bure. Kwa ajili ya kilimo tu,
Viongozi wote wa serikali kuu Kila mtu angejinunulia gari lake kutoka na mshahara anaopata hata Hawa mawaziri, serikali yangu ingewapatia magari ya bei nafuu, pesa yote ningeipeleka kuhudumia kilimo
Kwa mfano kuwatafutia mbegu Bora na mbolea ya mkopo Kwa Kila mkulima, wavuvi wangepewa zana Bure na boti ndogondogo zitakazo wasaidia kuendesha uvuvi bila misuko suko Mikubwa.
Ningejenga viwanda vikubwa vya kuchakata minofu ya samaki na kusafirisha samaki nje ya nchi, ningekuwa Rais maeneo yote ya bonde la Ruvu ningehakikisha nafungua mashamba makubwa ya miwa pamoja na kubuni maeneo mengine mapya yanayostawisha miwa kama Tanga, Kagera, na Mbeya Ili sukari iwe kutosha muda wote. Vijana wengi wangepata ajira na wangelima bila shida,
Ningekuwa Rais reli ya standard gaurge ningeijenga mwisho Dodoma, pesa nyingine yote ningejenga mahospitali makubwa Kila wilaya, ningekuwa Rais cheo Cha mkuu wa wilaya ningekiondoa abaki mkuu wa mkoa, mkurugenzi na RAS.
Ningekuwa Rais ningepunguza misafara kwenye ziara za viongozi badala ya gari kumi na kubaki na mbili tu Ili kupunguza gharama ya mafuta, ningekuwa Rais nisingetoa ajira zinazojirudia Kwa watu wale wale na jamii Ile Ile au Koo zile zile.
Ningekuwa Rais ningeondoa nafasi ya makamu wa Rais ningebaki na waziri mkuu tu. Kama ningekuwa Rais wahitimu wote wa JKT wangejiunga na jeshi Kwa hiari.
Mwisho ningekuwa Rais ningepunguza mishahara ya wabunge na kuelekeza pesa hizo kwenye huduma ya jamii, ningekuwa Rais wajumbe wanyumba kumi wangepewa mshahara hata laki Moja Kwa mwezi na halmashauri zao.