Nikiukana uraia wa Tanzania na kuamua niwe RAIA wa Uingereza; ardhi na mali zangu nitapokonywa Serikali? Au vitabakia kuwa vyangu

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
879
4,109
Natambua kuna sheria ya Uraia inayoniruhusu mimi kama RAIA wa Tanzania kuukataa uraia wangu wa Tanzania na kuwa RAIA wa nchi nyingine niipendayo.

Natambua kwamba katiba ya JMT na sheria za Ardhi zinakataza RAIA wa kigeni kumiliki ardhi isipokuwa kwa masharti maalumu kama uwekezaji na atakabidhiwa umiliki kwa muda flani.

Natambua pia kwamba RAIA wa kigeni anakatazwa na sheria kununua au kujenga nyumba Tanzania isipokuwa kwa kibali maalumu.

ISUES FOR DISCUSION
1. Je,ninapoukana uraia wa Tanzania ninaruhusiwa kisheria kuendelea kumiliki ardhi niliyokuwa nayo kipindi nikiwa RAIA wa Tanzania?

2. Kama siruhusiwi kuendelea kumiliki ardhi hiyo kama Mtanzania namkabidhi nani na kwa sheria gani?

3. Kama sheria na kanuni hazijasema kinapaswa kusurender ardhi na wapi nisarende ardhi; je nikibainika ninaimiliki hiyo ardhi naweza kushtakiwa?

4. Kama natakiwa kuikabidhi ardhi husika serikalini, je hadi sasa wizara ya ardhi ina ardhi kiasi gani ya watanzania walioukataa utanzania?

5. Endapo ardhi iliyopo ni ya urithi, wanapogawa mirathi mimi kama RAIA wa kigeni aliyekuwa Mtanzania naruhusiwa kupewa ardhi kama Sehemu ya mnufaika wa mirathi? Kwa sheria gani?

6. Je, ninaweza kurithisha ardhi yangu au ya urithi kwa mtu mwingine nisipokonywe?

Hii mada ni maalumu kwa waliosoma sheria za Uhamiaji, ardhi na katiba ya Jamuhuri. ..Lipo kundi kubwa la RAIA wa Kigeni wanaomiliki ardhi baada ya kuukana utanzania .Karibuni wajuvi
 
Tanzania ardhi yote ni ya Umma chini ya dhamana ya Raisi. Wageni kama wewe hawamilikiswi ardhi Bali Wana kodishiwa kama wawekezaji chini ya dhamana ya Kituo Cha uwekezaji Tanzania (TIC).

Ukiwa mgeni utapewa idhini ya kutumia ardhi hiyo kwa ajili ya uwekezaji tu, kama unao. Vinginevyo ardhi ni ya Umma na itatudi kwa Umma.
 
Kindeena njoo utupe sheria huku

Hujambo!

Ngoja nieleze kwa ujumla dhana ya wageni kumiliki ardhi Tanzania kwa ujumla.

Ukisoma Sheria ya Ardhi, Katiba na Sheria ya Uwekezaji pamoja na sera za serikali, unaweza ukagundua yafuatayo.

Kimsingi, sheria inakataza raia wa kigeni kumiliki ardhi.

Lakini sheria hii pia inasema raia wa kigeni anaweza kupewa kibali cha kutumia ardhi kwa lengo la uwekezaji.

Pia, sheria inampa nafasi raia wa Tanzania kumiliki ardhi kwa ubia na raia wa kigeni kwa lengo la uwekezaji.

Sasa utaona hapa kuna mambo makuu mawili:

Kwanza, sheria inakataa kwa upande mmoja, lakini upande mwingine inaruhusu raia wa kigeni kumiliki ardhi.

Kwa hiyo basi, raia wa kigeni anaweza kumiliki ardhi kwa kupitia mianya ya kisheria ambayo ni uwekezaji, kumiliki kwa ubia na raia wa Tanzania.

Pia watu wengine, mfano Mtanzania akioana na mgeni, basi hawa wawili wanaweza kumiliki ardhi bila bugudha.

Kwa hiyo kujibu swali lako la msingi, ukiukana uraia wako wa Tanzania, basi unaweza ukaendelea kumiliki ardhi yako kupitia mianya ya sheria niliyoieleza hapo juu ambayo ni NDOA UWEKEZAJI na UBIA

Bila shaka nimejitahidi kujibu!
1703309344009.jpg
 
Ardhi ni mali ya serikali na Rais ndiyo custodian wake. Wewe umekodishiwa tu ardhi hivyo ukiukana uraia wako haki zote za ardhi zinarudi kwa mwenye nayo (Rais), wewe mpangaji huna chako.
 
Sheria ziko hivyo lkn kufanya kazi ilishindikana.Ni nani ulimsikia kanyanganywa ardhi kisa kakana uraia wa Tanzania? hayupo, na wapo kibao wamiliki wa namna hiyo.
 
Ardhi ilikuwa mali ya wananchi chini ya tawala za kimila hadi wakoloni walipoitwaa iwe kwa mapatano ya kilaghai au kwa kushinda vita.
Harakati za ukombozi hapo mwanzo zililenga kurudisha ardhi kwa wananchi kutoka kwa wakoloni ili irudi kuwa mali ya wananchi. Vinara wa kudai uhuru walipofanikiwa kupata Dola wakajisahau na kuruhusu wanasiasa waliojichimbia kwenye vyama hapa itamkwe TANU na ASP kuuteka mchakato mzima wa kudai uhuru na kujivika mamlaka ya Dola.
Uhuru tunaojidai kupigania na kuupata ni uhuru wa viongozi na watendaji Serikalini maana wameirithi Serikali ya kikoloni na wanaendeleza ukoloni hadi leo.
Kusema ardhi ni mali ya Umma chini ya uangalizi wa Rais ni kuendeleza mawazo yale yale ya kikoloni. Serikali inapaswa kupata ardhi kutoka kwa wananchi.
 
Natambua kuna sheria ya Uraia inayoniruhusu mimi kama RAIA wa Tanzania kuukataa uraia wangu wa Tanzania na kuwa RAIA wa nchi nyingine niipendayo.

Natambua kwamba katiba ya JMT na sheria za Ardhi zinakataza RAIA wa kigeni kumiliki ardhi isipokuwa kwa masharti maalumu kama uwekezaji na atakabidhiwa umiliki kwa muda flani.

Natambua pia kwamba RAIA wa kigeni anakatazwa na sheria kununua au kujenga nyumba Tanzania isipokuwa kwa kibali maalumu.

ISUES FOR DISCUSION
1. Je,ninapoukana uraia wa Tanzania ninaruhusiwa kisheria kuendelea kumiliki ardhi niliyokuwa nayo kipindi nikiwa RAIA wa Tanzania?

2. Kama siruhusiwi kuendelea kumiliki ardhi hiyo kama Mtanzania namkabidhi nani na kwa sheria gani?

3. Kama sheria na kanuni hazijasema kinapaswa kusurender ardhi na wapi nisarende ardhi; je nikibainika ninaimiliki hiyo ardhi naweza kushtakiwa?

4. Kama natakiwa kuikabidhi ardhi husika serikalini, je hadi sasa wizara ya ardhi ina ardhi kiasi gani ya watanzania walioukataa utanzania?

5. Endapo ardhi iliyopo ni ya urithi, wanapogawa mirathi mimi kama RAIA wa kigeni aliyekuwa Mtanzania naruhusiwa kupewa ardhi kama Sehemu ya mnufaika wa mirathi? Kwa sheria gani?

6. Je, ninaweza kurithisha ardhi yangu au ya urithi kwa mtu mwingine nisipokonywe?


Hii mada ni maalumu kwa waliosoma sheria za Uhamiaji, ardhi na katiba ya Jamuhuri. ..Lipo kundi kubwa la RAIA wa Kigeni wanaomiliki ardhi baada ya kuukana utanzania .Karibuni wajuvi
Ccm ni mavii hakuna watu wengi wenye akili ...nilisema serikali ilitakiwa kuwe na aina 3 za uraia wa tz zenye sifa tofauti ...leo hii msomali au muindi au muarabu au mburundi akipewa uraia wa tz basi moja kwa moja anaweza kuwa mwanasiasa au hata kuwa mgombea ubunge au urais hii ni upumbavu....pia watz watz kuwa na uraia wa nchi mbili ilitakiwa kuwa daraja la chini la uraia ambao ungempa huyo mtz ruhusa ya kuwa mpiga kura tu na siyo mwanasiasa au mgombea wa kisiasa kwa sababu ana uraia wa nchi mbili ...kuzuia uraia wa nchi mbili ni upumbavu wa sisiemu .....DARAJA 3 ZA URAIA ZINGETOSHA KUTATUA KILA AINA YA UPUMBAVU KWENYE ISSUE ZA URAIA NA KULIOKOA TAIFA KUTEKWA NA RAIA FEKI WENYE NIA HOVU KAMA ILIVYO SASA WAKINA ROSTAM AZIZI NI MMOJA WAPO WA RAIA FEKI ...WAPO TZ KUCHUMA KIFISADI BILA KUJALI USALAMA WA TAIFA MAANA KWAO TANZANIA SI KITU ....WANAZO NCHI WANAZO ZITHAMINI MIOYONI MWAO
 
Back
Top Bottom