Nikimwangalia raisi Karume napata faraja sana....

Nikimwangalia raisi Karume napata faraja sana....

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2009
Posts
7,472
Reaction score
7,275
Kwa haiba ya uraisi, umakini wa kuongea, kutokumwaga mitabasamu isyokuwa na mpango, kuchagua mahali pa kuweka utani, adabu ya kiti cha uraisi n.k napata faraja sana nikimsikiliza raisi Karume kwani yoote haya anayo ......ananoga kumtazama au kumsikiliza kama kiongozi mkuu wa Dola siyo kama "huyu"!!!
Najipa moyo, kuwa duh, angalau kumbe tuna Raisi........
 
Una matatizo sana ndugu yangu: Hujui kwamba siku nyingine wasaidizi wake humteremsha jukwaani kabla ya kutoa speech wakigundua kaunyaka kisawasawa?
 
Kuna wakati fulani huko nyuma chai Jaba ilipigwa marufuku kuingizwa Zanzibar. Inasemekana watu wa CUF walimpachika jina la Chai Jaba kufuatana na lile tangazo maarufu la TV la bidhaa hiyo.
 
Kuna wakati fulani huko nyuma chai Jaba ilipigwa marufuku kuingizwa Zanzibar. Inasemekana watu wa CUF walimpachika jina la Chai Jaba kufuatana na lile tangazo maarufu la TV la bidhaa hiyo.

Hahaha!mkuu umenikumbusha mbali sana na hili tangazo la chai jaba.Siku zile bongo kuna mshkaji mtaani ilibidi arushe ngumi alipoona hili jina limeanza kumzoea!
 
Raisi........

Raisi tunaye kweli......lakini sio Rais!!!!!!!!!!!
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Raisi na Rais! Maraisi wetu ni wale wanaowekwa madarakani kwa nguvu ya chama! Miaka mitano inapita hakuna kipaumbele hakuna jipya! Sana sana utawasikia wanafungua Zahanati madarasa mawili ya sekondari ya kata katika kijiji cha mchambawima kazi inayopaswa kufanywa na madiwani! Wakiugua utawasikia wameenda ujerumani kutibiwa wakati hawataki kujenga hospitali nyumbani! Badala ya kutuchangisha pesa angalau tuwe na hospital moja ya kisasa na yenye uwezo wa kufanya operation kama za mioyo, tunachangiswa pesa ya kupigia campaign ili warudi madarakani na baada ya hapo watusahau tena miaka mingine mitano!

Siami hata kidogo kwamba Tanzania hatuwezi jenga chuo kikuu wenyewe mpaka Saudi Arabia waje kutujengea! Siami hata kidogo kwamba Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru hatuna hospital hata moja inayoweza kufanya operation hata ya moyo? Thanks to Dr Masau!
Nadhani viongozi wetu wana mtindio wa ubongo! Maana suala sio pesa, ni utashi!!! ni kuthubutu!
 
Lakini mantiki hasa ya kuweka thread hii ni nini? Mzizi wa Mbuyu nawe unakuwa kama MS!
 
Lakini mantiki hasa ya kuweka thread hii ni nini? Mzizi wa Mbuyu nawe unakuwa kama MS!

JK hamna kitu bwana, kiongozi gani huyu!? kuhusu jamaa wa znz kupiga maji haina neno kwani haviingiliani, mbona Obama aliwahi kuvuta bangi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom