Nikaona maiti zao..!

pitisha na michango mtambuzi tutachangia,na litaingia tena kwenye jamii,niliwahi kupata counsceling session moja hivi kutoka kwa Munga,kwa kweli ilibadilisha sana maisha yangu na ya mume wangu.nikisoma post zako huwa nashindwa kujizuia kukumbuka upole na ukarimu wa yule mtu!udongo hula vizuri jamani!R.I.P MUNGA.utaendelea kuishi mawazoni mwetu milele

Ni kweli, hata yeye alilitambua hilo kwamba ipo siku roho yake itaachana na mwili na ndio maana alianzisha madarasa ya kufundisha maarifa hayo ambapo sisi wanafunzi wake tunaendeleza kile alichotuachia.... Madarasa hayo kwa sasa yapo Tabata Kimanga.
Kwa sasa, ninachofanya ni kuendelea kuweka makala mbalimbali za maarifa hayo kupitia hapa JF kwa wale ambao hawana muda wa kuhudhuria madarasa yetu kule Tabata.

Nakumbuka katika makala zake za mwisho mwisho kabla hajafariki Hayati Munga Tehenan aliwahi kuandika hivi:

"Inaonyesha wazi kwamba, binadamu bado ni mjinga sana juu ya maisha yake. Mwili, mwili ni nini, na hadi wapi? Kama mwili ungekuwa na maana sana, baada ya mtu kufariki asingekimbizwa mochuari, usingepakwa asali au usingechomwa sindano ili usiharibike na kuleta usumbufu wa harufu na maradhi. Mwili siyo mimi wala wewe.

Mwili haujawahi kuwa mwenye mwili na hautakuja kuwa. Mwili ni kama tochi tu, ambayo umeiazima ili uweze kukusaidia kufika kijiji cha pili, kutokana na giza na njia ya uchochoro ambayo unatakiwa kuipita ili kufika kijiji hicho cha pili Mwili ni kifaa na siyo wewe, bali wewe unakitumia kifaa hicho. Binadamu anajibainisha kwenye maisha haya ya hapa duniani kupitia mwili wake, lakini yeye siyo mwili. Mwili ni ubainisho, ni chombo cha kutumika kwa kusudi la kidunia tu.

Baada ya muda mwili hukoma kuwepo, hujimaliza wenyewe au kumalizwa, ili binadamu amudu kuingia hatua nyingine ya maisha ambayo haitumii au haihitaji mwili. Tangu ulipozaliwa umeoneshwa na kufundishwa kwamba, wewe ni mwili kwa njia zote. Akili yako imeshika kutu kwa kuamini kwamba, mwili ni wewe na wewe ni mwili. Huna uwezo tena wa kuuona ukweli, kwa sababu vipimo vyako vyote kuhusu maisha vinaishia kwenye akili, ambayo nayo pia haikuhusu, siyo yako umepachikwa tu. Kwa ujinga huu wa kutojua mwili ni nini na sisi ni nani, ndipo ambapo tunaingia kwenye ujinga wa kuendeshwa na miili yetu, hisia zetu na akili. Kila mmoja anaamini kwamba, mwili wake ukipotea, ukishindwa kutumika, yaani akifa, basi huo ndio mwisho wake.

Kama hiyo ni kweli, ina maana binadamu hana maana kabisa, ni upuuzi usiofaa kuelezewa! Yaani binadamu amekuwepo ili awepo kwa mwezi mmoja, miaka kumi, hamsini, sabini, tisini au mia tu. Halafu baada ya hapo basi. Huu ni uongo mkubwa sana, unaoweza kukubaliwa na akili makapi ya kulishwa tu! Anayetafakari zaidi kidogo, atabaini kwamba, mwili ni mwili tu, ni kasha tu. Ni kasha ambalo muda wake wa kutumika ukiisha mtumiaji au (wewe) analiacha kwa sababu haliwezi kukidhi kile kinachohitajika hapa duniani. Mtumiaji anachukua kingine ambacho kinakidhi wakati huo (baada ya kifo).

Kwa hiyo, binadamu hafi bali mwili ndiyo unaofikia ukomo wa muda wake wa matumizi kwa sababu mbalimbali. Anapokufa John au Hamisi, haina tofauti. Anapokufa mkulima hohehahe au tajiri kuliko wote duniani, pia haina tofauti. Wote wanapita kwenye hatua ya mabadiliko, ambapo wanaacha matumizi ya kifaa kilichokuwa ndicho pekee kinachoweza kuwabainisha na wengine hapa duniani na kuchukuwa kingine ambacho hakiwezi kuwabainisha tena na wale wenye miili bado. Anapokufa John au Hamisi, haijalishi kama amezikwa kwa jeneza la dhahabu na mizinga 100 au kwa masululu butu na kaniki."
 
Jmani hii story imenifundisha sana,inabidi sasa tuwe tunaotesha mbegu kwa kuwasaidia watu wengine ili hali umemwona ana shida na hana msaada wowote.
 
Asprin linapatikana hapa hapa JF mkuu...............
In fact niko katika michakato ya kulifufua na kuliendesha kiufanisi zaidi, nakusanya mikwanja mkuu..................

Ebwana Mtambuzi naomba usinisahau ukilianzisha..
Nitaomba kuwa na safu mkuu....
 
Last edited by a moderator:
mtambuzi thanks alot for the story,kilichonifurahisha zaidi kijana kasema alikua anasoma kwiro sec morogoro,mimi pia ni product ya shule hiyo iliyojengwa enzi za mkoloni.
 
Kisha akaendelea kusema..................
"Kuzikwa ni utaratibu wa kimazoea wa kuhifadhi mwili ambao sasa ni mzoga tu, ili usisumbue watu wengine kwa harufu na maradhi. Kuzika haina maana kwamba, kunambadili aliyekuwa akitumia mwili huo (marehemu), la hasha. Kama unadhani kwamba Mungu anahesabu umezikwa na dini gani, umezikwa na shehe au padri gani, ndiyo afanye uamuzi wa kukupokea mbinguni au hapana, ujue unahitaji msaada wa haraka, kama siyo kupelekwa milembe. Ujue hujui chochote ingawa umekuwa ukijidanganya kwamba unajua.

Mungu wa kweli hahangaiki na mzoga, bali sisi kwa ufinyu wetu ndiyo tunaodhani kwamba, mizoga au (maiti) hii ina maana. Mara nyingi nimekuwa nikiwaambia jamaa zangu, "nikifa mtaangalia ni mazingira gani ni rahisi kwenu kuutupa au kuuhifadhi mwili wangu.

Kwa nini? Kwa sababu, kama sikuwa karibu na Mungu wakati nikiwa na mwili huo, ukaribu utaletwa leo wakati nimeupoteza mwili huo kwa sababu tu, mwili wangu umezikwa kwa dini ya babu yangu? Ukosefu wa ufahamu wa kiwango kikubwa sana. Kama nilikuwa karibu na Mungu wakati wa uhai wangu, basi hata nikitupwa chooni baada ya kufa, ukaribu huo hautakufa.

Mungu hayatazami mambo kama Abdallah Juma au John Maiko! Kwani kuzika hasa ni kitu gani. Hatuziki watu ili waende mbinguni. Kama ni hivyo, walioliwa na wanyama, kuungua na kuteketea kabisa, wao mbinguni hawatafika? Kama hawatafika, watahukumiwa vipi siku ya mwisho? Mwili hautakiwi mbinguni, hauna kazi huko, kwani huko siyo makazi ya miili. Mwili unafaa tu duniani.

Kuna zile jamii ambapo mtu akifa mwili wake huchomwa moto na kuteketezwa kabisa, unadhani hizi jamii hazimjui Mungu kama wewe unavyomjua? Zinamjua, tena pengine vizuri zaidi yako. Lakini, zimeng"amua kwamba, mwili ni kasha tu, likishindwa kufanya kazi, ni sawa na taka nyingine, hutupwa dampo na kuteketezwa kwa moto.

Mtu akishauacha mwili wake (kufa) hana tena uhusiano na mwili huo. Mtu huyo anakuwa ameingia tena kwenye awamu nyingine ya maisha ambayo haihitaji mwili na ambayo haihitaji kujua huo mwili umezikwa na nani na wapi. Ni akili isiosogea ndiyo ambayo inashindwa kufanya mikokotoo midogo kama hii."
 
Asante kwa story nzuri ya kuskitisha na kufunza pia,ndio maana tumeambiwa tenda wema uende zako,pia tumeambiwa kujiwekea hazina zetu mbinguni.
 
Ni kweli, hata yeye alilitambua hilo kwamba ipo siku roho yake itaachana na mwili na ndio maana alianzisha madarasa ya kufundisha maarifa hayo ambapo sisi wanafunzi wake tunaendeleza kile alichotuachia.... Madarasa hayo kwa sasa yapo Tabata Kimanga.
Kwa sasa, ninachofanya ni kuendelea kuweka makala mbalimbali za maarifa hayo kupitia hapa JF kwa wale ambao hawana muda wa kuhudhuria madarasa yetu kule Tabata.

Nakumbuka katika makala zake za mwisho mwisho kabla hajafariki Hayati Munga Tehenan aliwahi kuandika hivi:

"Inaonyesha wazi kwamba, binadamu bado ni mjinga sana juu ya maisha yake. Mwili, mwili ni nini, na hadi wapi? Kama mwili ungekuwa na maana sana, baada ya mtu kufariki asingekimbizwa mochuari, usingepakwa asali au usingechomwa sindano ili usiharibike na kuleta usumbufu wa harufu na maradhi. Mwili siyo mimi wala wewe.

Mwili haujawahi kuwa mwenye mwili na hautakuja kuwa. Mwili ni kama tochi tu, ambayo umeiazima ili uweze kukusaidia kufika kijiji cha pili, kutokana na giza na njia ya uchochoro ambayo unatakiwa kuipita ili kufika kijiji hicho cha pili Mwili ni kifaa na siyo wewe, bali wewe unakitumia kifaa hicho. Binadamu anajibainisha kwenye maisha haya ya hapa duniani kupitia mwili wake, lakini yeye siyo mwili. Mwili ni ubainisho, ni chombo cha kutumika kwa kusudi la kidunia tu.

Baada ya muda mwili hukoma kuwepo, hujimaliza wenyewe au kumalizwa, ili binadamu amudu kuingia hatua nyingine ya maisha ambayo haitumii au haihitaji mwili. Tangu ulipozaliwa umeoneshwa na kufundishwa kwamba, wewe ni mwili kwa njia zote. Akili yako imeshika kutu kwa kuamini kwamba, mwili ni wewe na wewe ni mwili. Huna uwezo tena wa kuuona ukweli, kwa sababu vipimo vyako vyote kuhusu maisha vinaishia kwenye akili, ambayo nayo pia haikuhusu, siyo yako umepachikwa tu. Kwa ujinga huu wa kutojua mwili ni nini na sisi ni nani, ndipo ambapo tunaingia kwenye ujinga wa kuendeshwa na miili yetu, hisia zetu na akili. Kila mmoja anaamini kwamba, mwili wake ukipotea, ukishindwa kutumika, yaani akifa, basi huo ndio mwisho wake.

Kama hiyo ni kweli, ina maana binadamu hana maana kabisa, ni upuuzi usiofaa kuelezewa! Yaani binadamu amekuwepo ili awepo kwa mwezi mmoja, miaka kumi, hamsini, sabini, tisini au mia tu. Halafu baada ya hapo basi. Huu ni uongo mkubwa sana, unaoweza kukubaliwa na akili makapi ya kulishwa tu! Anayetafakari zaidi kidogo, atabaini kwamba, mwili ni mwili tu, ni kasha tu. Ni kasha ambalo muda wake wa kutumika ukiisha mtumiaji au (wewe) analiacha kwa sababu haliwezi kukidhi kile kinachohitajika hapa duniani. Mtumiaji anachukua kingine ambacho kinakidhi wakati huo (baada ya kifo).

Kwa hiyo, binadamu hafi bali mwili ndiyo unaofikia ukomo wa muda wake wa matumizi kwa sababu mbalimbali. Anapokufa John au Hamisi, haina tofauti. Anapokufa mkulima hohehahe au tajiri kuliko wote duniani, pia haina tofauti. Wote wanapita kwenye hatua ya mabadiliko, ambapo wanaacha matumizi ya kifaa kilichokuwa ndicho pekee kinachoweza kuwabainisha na wengine hapa duniani na kuchukuwa kingine ambacho hakiwezi kuwabainisha tena na wale wenye miili bado. Anapokufa John au Hamisi, haijalishi kama amezikwa kwa jeneza la dhahabu na mizinga 100 au kwa masululu butu na kaniki."

We need to think beyond the box mtambuzi to come with such conclusion and we have to remember and know that what we do for ourselves die with us but what we do for others and the world remains and is immortal.
 
Ni kweli, hata yeye alilitambua hilo kwamba ipo siku roho yake itaachana na mwili na ndio maana alianzisha madarasa ya kufundisha maarifa hayo ambapo sisi wanafunzi wake tunaendeleza kile alichotuachia.... Madarasa hayo kwa sasa yapo Tabata Kimanga.
Kwa sasa, ninachofanya ni kuendelea kuweka makala mbalimbali za maarifa hayo kupitia hapa JF kwa wale ambao hawana muda wa kuhudhuria madarasa yetu kule Tabata.

Nakumbuka katika makala zake za mwisho mwisho kabla hajafariki Hayati Munga Tehenan aliwahi kuandika hivi:

"Inaonyesha wazi kwamba, binadamu bado ni mjinga sana juu ya maisha yake. Mwili, mwili ni nini, na hadi wapi? Kama mwili ungekuwa na maana sana, baada ya mtu kufariki asingekimbizwa mochuari, usingepakwa asali au usingechomwa sindano ili usiharibike na kuleta usumbufu wa harufu na maradhi. Mwili siyo mimi wala wewe.

Mwili haujawahi kuwa mwenye mwili na hautakuja kuwa. Mwili ni kama tochi tu, ambayo umeiazima ili uweze kukusaidia kufika kijiji cha pili, kutokana na giza na njia ya uchochoro ambayo unatakiwa kuipita ili kufika kijiji hicho cha pili Mwili ni kifaa na siyo wewe, bali wewe unakitumia kifaa hicho. Binadamu anajibainisha kwenye maisha haya ya hapa duniani kupitia mwili wake, lakini yeye siyo mwili. Mwili ni ubainisho, ni chombo cha kutumika kwa kusudi la kidunia tu.

Baada ya muda mwili hukoma kuwepo, hujimaliza wenyewe au kumalizwa, ili binadamu amudu kuingia hatua nyingine ya maisha ambayo haitumii au haihitaji mwili. Tangu ulipozaliwa umeoneshwa na kufundishwa kwamba, wewe ni mwili kwa njia zote. Akili yako imeshika kutu kwa kuamini kwamba, mwili ni wewe na wewe ni mwili. Huna uwezo tena wa kuuona ukweli, kwa sababu vipimo vyako vyote kuhusu maisha vinaishia kwenye akili, ambayo nayo pia haikuhusu, siyo yako umepachikwa tu. Kwa ujinga huu wa kutojua mwili ni nini na sisi ni nani, ndipo ambapo tunaingia kwenye ujinga wa kuendeshwa na miili yetu, hisia zetu na akili. Kila mmoja anaamini kwamba, mwili wake ukipotea, ukishindwa kutumika, yaani akifa, basi huo ndio mwisho wake.

Kama hiyo ni kweli, ina maana binadamu hana maana kabisa, ni upuuzi usiofaa kuelezewa! Yaani binadamu amekuwepo ili awepo kwa mwezi mmoja, miaka kumi, hamsini, sabini, tisini au mia tu. Halafu baada ya hapo basi. Huu ni uongo mkubwa sana, unaoweza kukubaliwa na akili makapi ya kulishwa tu! Anayetafakari zaidi kidogo, atabaini kwamba, mwili ni mwili tu, ni kasha tu. Ni kasha ambalo muda wake wa kutumika ukiisha mtumiaji au (wewe) analiacha kwa sababu haliwezi kukidhi kile kinachohitajika hapa duniani. Mtumiaji anachukua kingine ambacho kinakidhi wakati huo (baada ya kifo).

Kwa hiyo, binadamu hafi bali mwili ndiyo unaofikia ukomo wa muda wake wa matumizi kwa sababu mbalimbali. Anapokufa John au Hamisi, haina tofauti. Anapokufa mkulima hohehahe au tajiri kuliko wote duniani, pia haina tofauti. Wote wanapita kwenye hatua ya mabadiliko, ambapo wanaacha matumizi ya kifaa kilichokuwa ndicho pekee kinachoweza kuwabainisha na wengine hapa duniani na kuchukuwa kingine ambacho hakiwezi kuwabainisha tena na wale wenye miili bado. Anapokufa John au Hamisi, haijalishi kama amezikwa kwa jeneza la dhahabu na mizinga 100 au kwa masululu butu na kaniki."

hakika hii ni miili tu!mwanadamu ni zadi ya yule unayemuona.nataka kujiunga na hayo madarasa kwa heshima ya MUNGA!
 
dah, imenigusa sana. naomba nikiri kuwa me ni mvivu wa kusoma story ndefu hapa jf kwan natumia simu. ila inapofika kwenye story za Mtambuzi huwa sina budi kusoma. na huwa najifunza mengi sana kupitia story zake!
 
Last edited by a moderator:
hili ni fundisho tosha kwa sisi wanadamu,kutenda wema ni kujiwekea akiba ambayo inanufaisha kama si wewe, kizazi chako!ungeifanya muvi mbona ungeuza kwa JF wengi sana!mradi tu wahusika wawae uhalisia kikwelikweli!IFANYE MUVI PLS
 
MTAMBUZI hi habari imenitoa chozi
kweli huwa kuna nguvu hatuzijui
tunapata fundisho kubwa sana hapa.
 
dah, imenigusa sana. naomba nikiri kuwa me ni mvivu wa kusoma story ndefu hapa jf kwan natumia simu. ila inapofika kwenye story za Mtambuzi huwa sina budi kusoma. na huwa najifunza mengi sana kupitia story zake!

MAra ya kwanza sikuwa nasoma nani ameandika, ila nilikuwa naangalia font style tu nafahamu ni fulani na nikawa navutiwa sana.

LEo nimetambua kuwa ni Mtambuzi!

Story imenitoa machozi!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom